Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Well elaborated mkuu!
 
Tuta za iringa hazina migongo mikali!!
Ilikuwa ni 2006 kama sikosei matuta hayakuwa mengi kama sasa hivi,uyole tulitoka sita kamili mchana ubungo saa tatu dk20,tulipokaribia kufika karibu na comfort hotel,kuna hardtop cruiser ikatuchomekea akijua tuko slow,baadae alipoona kila akikimbia tupo nyuma yake akatupisha.
 
Kwa coaster ina utata...sijui huyo jamaa alikuwa anaendeshaje especially vile vipande vyenye matuta, maana mitaa ya Iringa barabara imewekwa tutaz za kutosha
Huyo dereva Dullah nadhani bado yupo pale biafra ulizia mkuu,wengi wamebisha ila ukweli utabaki pale pale,tuliondoka kyela saa 3 badala ya saa 12 tuliyopanga,kusimama kulikuwa kwingi tukafika uyole saa 5:30,saa 6 tukaondoka ambulance iliyoondoka alfajiri tuliikuta vigwaza jamaa amepaki akidai kachoka,konda ikabidi amsaidie tukaongozana hadi ubungo p-station saa3+.Anaebisha abishe ila ndo ukweli.
 
Hizi na gari za jeshi ni safi sana kwa kuchangamsha safari.
😀😀😀 Gari za jeshi huwa ni bati bati, kuna siku tulikuwa tunaenda mahala na gari yao, tulikuwa nje ya mda, fujo yake ni noma na mwendo mkali kishenzi, kupita upande usio wetu ilikuwa kawaida tu 😀😀😀😀 na hatimae tukawai
 
Njia ya Dar mpk Arusha nimepita mara 3 tu, na kiukwel nilikuwa natembea mwendo wa kitalii maana nilikuwa na wageni nimetoka kuwapokea.

Ila njia ya kuanzia Shelui(Singida) mpaka Dodoma almost (338 KM) huwa natumia masaa 3 tu wakat wa usiku.
😀😀😀 kuna siku nilikuwa natoka Dom naenda Singida, nimetoka zangu babalanga pale saa moja nampigi boss simu asubuhi natoka hapa dodoma nakuja hapo kumalizi kazi, hakuamini saa mbili na nusu nipo Singida nilitumia saa moja na nusu 😀😀😀😀 hakuna mahala nilisimama hadi natia nanga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…