Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Hujui usemalo sijui kwanini unakuwa kama mtu asie na ABC za magari. Watu wanatoka SA mpaka Tz na kurudi na hizo gari kila miezi michache. Dogo mmoja namjua ana Golf mk5 huwa anaenda na kurudi mwanza kila mwezi mara mbili au tatu.
Hahahah lengo ilikuwa ni kuchangamsha genge tu bro 😀😀😀 hakuna gari isiotembea non stop ikiwa cooling system iko freshi
 
Hahahah lengo ilikuwa ni kuchangamsha genge tu bro 😀😀😀 hakuna gari isiotembea non stop ikiwa cooling system iko freshi
Sasa mkuu trip hii nimeona gari nyingi za kijapan zimechemka hasa harrier tako la nyani. Nilichoona wengi wamefungua bonnet wanajaza maji. Wengi wanajisahau kukagua radiator. Katika vitu muhimu usisahau kukagua radiator. Hakikisha radiator yako iko vizuri.
 
Tuna carelessness sana watanzania. Na mentality hiyo ndiyo inatufanya tunazipa gari fulani repuration mbaya kwasababu hatuna umakini wa kuzitunza zinavyotaka.
 
Mkuu wewe upo Safi,inabidi tuungane tufanye road trip ya kwenda kwa Madiba, maana hizo 2700km for 4days, ukiongeza hapo 800km tayari upo joberg
Sasa hizo inabidi ipigwe kwa siku 2 au 3.

Kila siku ukiendesha masaa 16 unaweza kucover 1000 - 1300 km kutegemeana na kipande cha barabara. Masaa 8 unapumzisha fuvu
 
Hao ndio wale anatembelea gari ilimradi akiwasha inawaka tu 😀! Mie huwa nafuatilia sana gari hasa radiator na oils. Toka utotoni sijui sababu nimekulia kwenye gari nyingi. Ila kuna kruza mkonge ilikuwa inapoteza maji so kila siku lazma niwashe
 
Sasa hizo inabidi ipigwe kwa siku 2 au 3.

Kila siku ukiendesha masaa 16 unaweza kucover 1000 - 1300 km kutegemeana na kipande cha barabara. Masaa 8 unapumzisha fuvu
Yes mkuu ukipiga T1 overnite asubuhi kuanzia saa 11am Zambian time unaianza ile nakonde by 2200 hrs mnaweka kambi Serenje, around 4am mnaanza Serenje by 2100 hodi Livingstone ,next morning by 5am mnaelekea kazungula border by 7am mnavuka then ni mkeka wa nguvu ikifika 1900hrs mpo Martin drift border mnavuka,rest kidogo, 2100 hrs mnaanza 4am good morning Joberg, yes tuifanye hii road trip mkuu
 
[emoji1787]

Mkuu Nkanini

Mkitoka nakonde zero five (05:00)

Kulala Kapiri mposhi au Kabwe ni uhakika

Ila muwe makini na zile handaki pale

Danger hill na kule bwawa la samaki

Sent from my TECNO BD4h using JamiiForums mobile app
 
Inshallah mkuu mipango ikikaa sawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…