Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Duh leo nimetenda dhambi roho imeniuma sana. Nilikuwa na gari sijaizoe. Taa ya mafuta imewaka range inanionesha nina km20 tu. Nikaamua niweke mafuta ya kunifikisha home tu nikaweka 10,000 nilijua itaongeza range hadi km60 hivi. Baada ya kuweka mshale haukusogea wala range haikubadilika. Nikaenda ninapoenda range inashuka.
Kurudi nikapita njia ile ile range iko 14, nikapita pale kituo cha mafuta nikamwambia Yule dada nimeweka mafuta hapa kwako lakini gauge haikupanda wala kuonesha kuna mafuta yameingia, umeniibia! Dada Yule akasema sijakuibia nimekuwekea hela ulionipa nikamwambia haiwezekani kusiwe na mabadiliko kwenye gauge, ikabidi niende kituo kingine nikaweka 10, aisee gauge ikakurupuka ikapanda sana na range ikaja kwenye 110km. Hapo nikajua ni kweli aliweka mafuta nimemsingizia tu. Nimejisikia vibaya sana.
Ilishawahi nitokea kama hii.

Gari ilikuwa harrier tako la nyani ya mshkaji.

Niliweka mafuta kama ya 50K. Nikajua gauge itapanda mbeleni.

Namrudishia gari akalalamika nimerudisha bila mafuta. Ikabidi nimrushie 50 ingine aweke. Akaenda kuweka mzigo ukaruka mpaka full.

Akajisikia vibaya kinoma. Akataka kurudisha mpunga, nikamwambia akaushe.
 
Sidhani. ...

Tena wa kike ndio laini, sister angu alishamsaundisha traffic wa kike mm nilikuwa sijafunga mkanda na akaeleweka. Traffic aliishia kusema next time asirudie
Traffic wa kike watu poa sana.

Niliwahi mpita traffic wa mmama njia ya moro. Akanisimamisha nikasimama mbele sana. Ikabidi nirudi. Akaniongelesha vizuri sana jinsi ilivyo hatari kukimbiza gari. Nikampa 30 ya kumuonea huruma.

Ndo traffic pekee mpaka sasa aliewahi hata kuongea vizuri na mimi.
 
Traffic wa kike watu poa sana.

Niliwahi mpita traffic wa mmama njia ya moro. Akanisimamisha nikasimama mbele sana. Ikabidi nirudi. Akaniongelesha vizuri sana jinsi ilivyo hatari kukimbiza gari. Nikampa 30 ya kumuonea huruma.

Ndo traffic pekee mpaka sasa aliewahi hata kuongea vizuri na mimi.
Duh 30,000 nzima! Kuna mwenzio mwingine humu alitoa 50,000/-. Mimi sometime wananiomba namuachia 5,000/- tu
 
Duh 30,000 nzima! Kuna mwenzio mwingine humu alitoa 50,000/-. Mimi sometime wananiomba namuachia 5,000/- tu
Yule alikuwa mama mtu mzima kidogo.

Nika-assume atakuwa na majukumu ya kifamilia.

Alikuwa porini kidogo halafu peke ake.

Na cha zaidi aliongea na mimi vizuri sana. Kama mama ananipa mawaidha.

30k nikaona hata haikutosha.

Mara nyingi traffic wa kike nawamudu sana. Sijawahi andikiwa faini na traffic wa kike.

Wengine naomba namba kabisa.
 
Bongo hii hii
IMG_20210114_125832_821.jpg
 
Oh mashimo yameongezeka? Na usiku kuona mbali ni issue. Mara ya mwisho nilisafiri jioni nikapata msala saa 12 ndio ilikuwa pona yangu vinginevyo ningelala barabarani hadi asubuhi. Sisafiri tena usiku.
Ukisafiri usiku nidhamu ya mwendo inahitajika, ukizoea myendo ya magari ya Ulaya inakuwa tabu kwelikweli.

VW Gt uliiuza?
 
Back
Top Bottom