Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Shukrani

Daah sasa huwa najiuliza wale wanaosafiri usiku kwenye hizo speed huwa wanawezaje aiseee

Mimi nina tatizo la kutokuona mbali na huwa nawaza kusafiri usiku kwenye high speed hasa peke yangu

Ila huwa nasoma humu naona watu wanasema wanasafiri usiku kwenye high speed hadi nawaonea wivu
Pima macho upewe miwani iwapo itakuwa ndio suluhisho.
 
Mungu amuepushe na vishawishi maanake umri huo kutulia si kazi ndogo.

Ila kiukweli umasikini ulaaniwe! Kuna gari unaingia mpaka unajiuliza...wewe una fail wapi?

Ulishajaribu kufungua mlango wa Mercedes GLE? au VW Touareg? mzee mlango una kilo kumi..nenda sasa kwa zile gari za akina Masanja..mlango kilo moja na nusu...

Yaani umasikini ni adui mkubwa 🙂
 
All the best...uangalie speed..hawa jamaa humu usiwasikilize sana aisee...

bado tunakuhitaji tulipe wote deni la taifa .....hahahahaha
Mkuu hizi ndio mambo hutaki kusikia?

20210526_101546.jpg
20210526_094954.jpg


Mbona hatuna ushauri mbovu mkuu tunamwambia vitu practical kabisa. Hizi spidi hatupangi mkuu, zinatokea tu.
 
Ila kiukweli umasikini ulaaniwe! Kuna gari unaingia mpaka unajiuliza...wewe una fail wapi?

Ulishajaribu kufungua mlango wa Mercedes GLE? au VW Touareg? mzee mlango una kilo kumi..nenda sasa kwa zile gari za akina Masanja..mlango kilo moja na nusu...

Yaani umasikini ni adui mkubwa 🙂
Acha tu kuna gari simple tu ya 2013/14 Mercedes E class kama anayoitamani Holy Man ukiigusa unaona kabisa dunia mbili tofauti na gari za 2007 kushuka chini.
Gari yoyote kuanzia 2014 kwa level zetu Bongo ni nzuri sana acha hizo za 2019/20
 
Hahah!
Tupo pamoja boss wangu .


Mimi sipendi Safari ila huu uzi unanivutia,taratibu najikuta naanza kutamani kutembea.

Sent using Jamii Forums mobile app
Barabara inakukaribisha sana.
Njoo tulambe lami mkuu... tuione nature ikipita pembezoni kwa kas, tuone kila aina ya greenish.
Njoo tuexperience hali ya hewa ya mikoa mitano tofauti ndani ya siku moja. Tuisikie sauti ya upepo.
Njoo tuone mazingira ambayo watanzania wenzetu wanaishi mbali na mijini.
Njoo tuenjoy.
 
Hapo kwenye suala la miwani sasa hapo ndipo mtihani ulipo. Sijui kwanini pamoja na kujigundua kuwa nina hili tatizo ila bado sipendi kujizoesha kuvaa miwani.
Basi itakuwa ishu ndogo. Wenzio tukivua miwani hatuwezi kusoma plate namba ya gari iliyoko mita 20 mbele!! Natembea na miwani ya spea kwenye gari ili ikivunjika hii nisije kushindwa kuendelea na safari!

Tatizo lako lingekuwa kubwa ungetafuta solution. Ama miwani, ama contact lenses, ama surgery. Ila usingeweza kuishi nalo, lingekuzuia vingi.
 
Back
Top Bottom