Wazir Ummy Mwalimu analeta siasa kwenye elimu; ni sampuli ya viongozi ambao hawana uchungu na elimu ya watoto wa maskini

Wazir Ummy Mwalimu analeta siasa kwenye elimu; ni sampuli ya viongozi ambao hawana uchungu na elimu ya watoto wa maskini

MR TOXIC

Senior Member
Joined
Jun 4, 2019
Posts
190
Reaction score
525
Bila aibu Ummy Mwalimu amesema ajira 1360 za walimu wa physics na 599 za walimu wa hesabu kwamba zimemaliza tatizo la uhaba wa walimu wa masomo ya sayansi nchini.

Kwangu kauli hiyo ya Ummy naona inalenga kutafuta umaarufu wa kisiasa kwani alichokisema ni uongo unaofaa kupuuzwa na kila mtu mwenye akili timamu.

Na , mawaziri kama hawa ni sampuli ya viongozi ambao Antony mtaka anasema hawana uchungu na elimu ya watoto wa watanzania maskini isipokuwa wapo kwaajili ya maslahi yao binafsi na familia zao.

Huku kwetu kila mwezi wazazi tunachanga elfu tatu kwaajili ya kulipa walimu wa temporary kufundisha watoto wetu kutokana na shule kutokuwa na walimu wa sayansi lakini waziri huyu bila hata hiyana anasema hakuna uhaba wa walimu wa sayansi. Hivi waziri kama huyu anafaa kuendelea kuwa msimamizi wa elimu yetu?

Au kwakuwa mtoto wake hasomi shule za kata ndio maana analeta siasa kwenye elimu kwakuwa anajua wanaoathirika sio watoto wake?

Huyu dada ni miongoni mwa mawaziri niliokuwa naona wana vision ya kiuongozi lakini kidogo kidogo ameanza kupotoka kupitia kauli na matamko yake ya kutafuta sifa za kisiasa kwenye mambo ya msingi.

Again, I stand with Antony Mtaka kwenye elimu
 
Acha porojo kijana.Kati ya mawaziri bora kabisa wa awamu ya sita ni Waziri Ummy Mwalimu.Tena aweza kuwa kinara wa ubora.Nina maono kuwa huenda akawa kiongozi wa ngazi za juu katika nyakati zijazo.

Bila Ummy,walimu masomo ya Sanaa ajira wangezisikia mitandaoni. Walimu wapya masomo ya sayansi wamepangwa kwenye shule ambazo hazijawahi kabisa kuwa na walimu wa masomo hayo tangu kuanzishwa kwake.

Usipotoshe, hakuna drastic changes zinazoweza kufanywa ndani ya siku au mwaka mmoja. Mwendazake alituharibu tusiuone uzuri wa wengine isipokuwa yeye.Kata hangover kaka mkubwa.
 
Hiyo wizara bora akapewa Mtaka maana ndo ameonyesha hadharani kuguswa na shida za wananchi ambao wapo chini kabisa.
 
Acha porojo kijana.Kati ya mawaziri bora kabisa wa awamu ya sita ni Waziri Ummy Mwalimu.Tena aweza kuwa kinara wa ubora.Nina maono kuwa huenda akawa kiongozi wa ngazi za juu katika nyakati zijazo.

Bila Ummy,walimu masomo ya Sanaa ajira wangezisikia mitandaoni. Walimu wapya masomo ya sayansi wamepangwa kwenye shule ambazo hazijawahi kabisa kuwa na walimu wa masomo hayo tangu kuanzishwa kwake.

Usipotoshe, hakuna drastic changes zinazoweza kufanywa ndani ya siku au mwaka mmoja. Mwendazake alituharibu tusiuone uzuri wa wengine isipokuwa yeye.Kata hangover kaka mkubwa.
Yes, Ummy yuko vizuri.

Kama CCM watataka Waziri Mkuu mwanamke, Ummy anastahili kabisa.
 
Waziri Tamisemi na Waziri wa elimu hawajui unyeti wa wizara zao,kimsingi mawaziri hawa wamepwaya,upungufu wa walimu bado ni mkubwa sana,baadhi ya maeneo upungufu huo unazibwa na uhaba wa vyumba vya madarasa,mfano unakuta shule ina vyumba 7/8/9 vya madarasa form 1_4,idadi ya wanafunzi ni 1000+,mgawanyo wa wanafunzi per class ni wanafunzi 100 hadi 120 katika shule hizo,ilhali muongozo wa wizara darasa linapaswa liwe na wanafunzi 40 na lisizid 60,ufanisi wa ufundishaji ni mdogo mno kwenye shule nyingi za kata mwalimu anafundisha darasa la zaidi ya wanafunzi 100,ni ngumu Kuwasimamia,kubaini slow learners n.k, so ajira nyingi za ualimu zmefichwa na uhaba wa miundo mbinu.
Mh. Anthony Mtaka anayajua kiundani matatizo ya hz shule kuliko waziri mwenye dhamana,amebeba jukumu la mzazi,anajua nini kifanyike ili kumkwamua mwanafunzi wa shule ya kata.
 
Kwanza mwambieni Ummy haache udini ,ametuletea walimu walimu wanaovaa dontouch matokeo yake wanafunzi wanaogopa kwenda shule. Mwambieni tumeshajua
 
Acha porojo kijana.Kati ya mawaziri bora kabisa wa awamu ya sita ni Waziri Ummy Mwalimu.Tena aweza kuwa kinara wa ubora.Nina maono kuwa huenda akawa kiongozi wa ngazi za juu katika nyakati zijazo.

Bila Ummy,walimu masomo ya Sanaa ajira wangezisikia mitandaoni. Walimu wapya masomo ya sayansi wamepangwa kwenye shule ambazo hazijawahi kabisa kuwa na walimu wa masomo hayo tangu kuanzishwa kwake.

Usipotoshe, hakuna drastic changes zinazoweza kufanywa ndani ya siku au mwaka mmoja. Mwendazake alituharibu tusiuone uzuri wa wengine isipokuwa yeye.Kata hangover kaka mkubwa.
Ummy alikuwa bora kwenye afya huku tamisemi ana boronga kwa sababu anaendekeza sana siasa kuliko uhalisia unless aache kuleta siasa kwenye mambo ya msingi anaweza kuwa kiongozi mzuri
 
Back
Top Bottom