Waziri Aweso: Familia yangu ni masikini, nimepata Uwaziri kutokana na elimu

Waziri Aweso: Familia yangu ni masikini, nimepata Uwaziri kutokana na elimu

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, amezungumza na wahitimu kwenye Mahafali ya 48 ya Chuo cha Maji, yaliyofanyika leo tarehe 13 Novemba 2024, kwenye Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam, akiwa mgeni rasmi.

Akizungumza katika hafla hiyo, Aweso amesema: "Mimi familia yangu ni masikini, nimefikia uwaziri kutokana na elimu. Naamini kupitia elimu mtoto wa Mama Ntilie anaweza kuwa mhandisi tegemezi katika taifa hili. Katika nafsi yangu naamini mtoto wa maskini kabisa anaweza kuwa mkuu wa chuo cha maji kupitia elimu. Wazazi na walezi hamjakosea na hautapata hasara kuwekeza katika elimu. Leo mnaniita Waziri wa Maji, familia yangu ni masikini kabisa, mtoto wa Mama Ntilie, lakini nimesoma, nimekuwa mkemia, nimekuwa naibu Waziri, na leo nimekuwa Waziri kwa sababu ya elimu."
Soma, Pia: Waziri wa Maji Jumaa Aweso ameahidi kuendelea kuzitafutia ufumbuzi changamoto katika Chuo cha Maji
 
Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, amezungumza na wahitimu kwenye Mahafali ya 48 ya Chuo cha Maji, yaliyofanyika leo tarehe 13 Novemba 2024, kwenye Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam, akiwa mgeni rasmi.

Akizungumza katika hafla hiyo, Aweso amesema: "Mimi familia yangu ni masikini, nimefikia uwaziri kutokana na elimu. Naamini kupitia elimu mtoto wa Mama Ntilie anaweza kuwa mhandisi tegemezi katika taifa hili. Katika nafsi yangu naamini mtoto wa maskini kabisa anaweza kuwa mkuu wa chuo cha maji kupitia elimu. Wazazi na walezi hamjakosea na hautapata hasara kuwekeza katika elimu. Leo mnaniita Waziri wa Maji, familia yangu ni masikini kabisa, mtoto wa Mama Ntilie, lakini nimesoma, nimekuwa mkemia, nimekuwa naibu Waziri, na leo nimekuwa Waziri kwa sababu ya elimu."
Soma, Pia: Waziri wa Maji Jumaa Aweso ameahidi kuendelea kuzitafutia ufumbuzi changamoto katika Chuo cha Maji
Muongo!!

Elimu bila connection au kuuza nafsi Kwa Lucifer au Maombi makubwa ya sadaka Kwa mtumishi sahihi ukibahatisha ndio silaha!!

Asikudanganye mtu,zaidi ya 90% ya wanasiasa nchini ni washirikina au wameuza nafsi zao kwenye secret societies kupata walichopata!!!

Elimi pekee haitoshi !"mwambieni aseme ukweli,kwanini walemavu wa ngozi wanakua wahanga nyakati za uchaguzi!!!?
 
20241112_191640.jpg
 
Back
Top Bottom