Waziri Aweso: Tatizo la Tokeni za Maji za Prepaid, latatuliwa BUWASA

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Hivi karibuni Mdau wa JamiiForums.com alitoa wito kwa Mamlaka ya Maji Bukoba - BUWASA, kushughulikia changamoto ya Wateja wa Mita za Maji za Prepaid kukosa Tokeni.


Wafanyakazi wa BUWASA wakiwa wanakagua Mita za maji za Prepaid

Ni kweli hii changamoto ilikuwepo na sio changamoto ya BUWASA bali ni changamoto ya kimataifa baada ya mabadiliko ya kimfumo kwa viwango vya ISO (International Standard Organisation), mabadiliko hayo ndio yameleta changamoto hii.

Baada ya kuitambua changamoto hii BUWASA kwa kushirikiana na Supplier (e-joy) wameweza kuitatua changamoto hii na sasa mteja akinunua TOKEN ya maji atapokea TOKEN TATU, ambazo anatakiwa aziingize zote kama zinavyojieleza kisha mita yake ya Maji itafunguka.

Wafanyakazi wa BUWASA wakiwa wanakagua Mita za maji za Prepaid

Pia BUWASA wanaendelea kuwatembelea wateja wote wa prepaid ili kuweza kutambua kama kuna changamoto nyingne wamekutana nayo baada ya hayo mabadiliko ya kimfumo.

Kwa mawasiliano zaidi, Wapigie BUWASA kwa Namba +255767539330 na 0800 110 1461

Mh. Jumaa Aweso
Waziri wa Maji.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…