Waziri azuia majaribio ya mbegu za GMO

Waziri azuia majaribio ya mbegu za GMO

Mbona hizi mbegu zinazoitwa za kisasa (hybrid) vimetokana na technolojia ya kuboresha gene?kwa maana nyingine ni G.M.O
 
Hizo mbegu za GMO ni mpango wa kampuni ya Mosanto kuiingiza duniankwenye utumwa wa chakula, hii ni kwa sababu mbegu zao ukishalima awamu ya kwanza, mbegu zinazozaliwa za kizazi cha pili zinakuwa tasa na haziwezi tena kutumika kwenye kilimo cha msimu ujao, hivyo inabidi ukanunue tena mbegu kwao kwa bei yao, na kwakuwa GMO zinastahimili zaidi basi mbegu za asili zitapotea na ndio tunaingia utumwani mazima; mtaambiwa mtuhusu uxhoga vinginevyo mnanyimwa mbegu mfe njaa
 
Kitu kingine ni kuwa kiafya haya mazao hayana shida yoyote, labda yawe modified kutengeneza sumu. Hata kiasili genetic modification huwa zinafanyika. Mahindi tunayolima leo siyo yaliyokuwa yanalimwa miaka 1000 au 2000 iliyopita. Pole kwa pole yanabadilika.

Hata wakulima wenyewe wa kienyeji hufanya hii kitu. Unapokula mahindi madogomadogo na kuweka makubwa kuwa mbegu ujue unafanya genetic modification, baada ya miaka kadhaa utakuwa na mahindi makubwa tu. Kinachofanyika huko maabara ni kuharakisha tu.
Tofautisha hybridization na genetic modification, tumiaga akili wakati unaandika, sawa?
 
Mbona hizi mbegu zinazoitwa za kisasa (hybrid) vimetokana na technolojia ya kuboresha gene?kwa maana nyingine ni G.M.O
Tofautisha hubridization na Genetic mofification, sawa? Mzungu akizaa na Mwafrika hiyo tunaita hybridization, ila ukichukua vinasaba vya mbwa ukavipandikiza kwenye yai la binadamu ili azaliwe binadamu mwenye uwezo wa kunusa kama mbwa hiyo ni generic modification, umeelewa?
 
Tofautisha hybridization na genetic modification, tumiaga akili wakati unaandika, sawa?
Wewe ndiyo huelewi hybridization ni nini na genetic modification ni nini? Kwanza hybridization inaingiaje hapa kama siyo kuchanganya mambo?
 
Ukitaka kupiga marufuku GMO maana yake upige marufuku ufugaji wa kuku wa kisasa, ng'ombe wa kisasa, mazao wanayosemwa yanastahimili ukame, yanayokuwa muda mfupi, miwa inayozaa sana nk.

Tukatae suala watu kupatent mbegu au tusitumie mbegu ambazo ziko patented lakini si kukataa na kupiga marufuku GMO, hii kitu hata kwenye nature inatokea.
 
Hicho kinachofanya uharaka ndicho kibaya. Mkulima anapukuchua mbegu zake anahifafhi mahala salama kusubiri msimu ujao

Waziri amesahau kutoa elimu ya Sheria ya mbegu...
Ni marufuku kulima kwa kutumia mbegu ambayo haijathibitishwa...
 
Hayo mazao hayatakuwa na ladha ndio maana wazungu wanahangaika na viungo! Unakula nyanya haina ladha mdomoni.

Unakuta chungwa au limao halina hata mbegu ndani [emoji3]. Yani unakula chungwa mwanzo mwisho hukutani na mbegu hata moja [emoji23]
 
Katika vitu ambavyo naweza kusifia kwenye serikali hii ni Jambo hili. Ingawa mengine wanapuyanga sana.

Every package [emoji403] has got some issues. Mengine wanapatia mengine wanakosea, ndo kibinadamu ilivyo.
 
Wewe ndiyo huelewi hybridization ni nini na genetic modification ni nini? Kwanza hybridization inaingiaje hapa kama siyo kuchanganya mambo?
Hybridization ni kama kuchukua mbwa aina ya german shepherd ukampandisha na mbwa aina ya bulldog, hapo ni umechanganya mbegu ambazo zipo tayari kwenye nature kama zilivyo kwenye viumbe ili kupata zao bora zaidi.

Ila Genetic modification ni kung’oa vinasaba toka kwenye viumbe tofauti tofauti ambapo vingine hata sio vya species moja na kuunga unga kama tu anaetia viraka kwenye nguo, mfano kuna mchele wa GMO ambapo wamechukua vinasaba vya binadamu na kwenda kuviunganisha kwenye vinasaba vya mpunga ili kuikinga dhidi ya magonjwa fulani fulani, katika hali ya kawaida binadamu asingeweza kufanya mapenzi na mpunga ili kuzaa mtoto, lakini kwa GMO inafanyika, na hiyo ndio tofauti kubwa ya GMO na hybridization
 
Mimi sio mtaalam sana wa masuala ya baiolojia, lakini sidhani kama unaweza kupata "hybrid" bila "genetic modification".
Hybridization haihusishi genetic modification at all, ila ni unachanganya vinasaba ambavyo vipo tayari in nature kwenye viumbe aina ile ile ili kupata kiumbe kipya na bora. Hybridization ni kama kuchukua mbwa aina ya german shepherd ukampandisha na mbwa aina ya bulldog, hapo ni umechanganya mbegu ambazo zipo tayari kwenye nature kama zilivyo kwenye viumbe ili kupata zao bora zaidi. Ila Genetic modification ni kung’oa vinasaba toka kwenye viumbe tofauti tofauti ambapo vingine hata sio vya species moja na kuunga unga kama tu anaetia viraka kwenye nguo, mfano kuna mchele wa GMO ambapo wamechukua vinasaba vya binadamu na kwenda kuviunganisha kwenye vinasaba vya mpunga ili kuikinga dhidi ya magonjwa flani flani, katika hali ya kawaida binadamu asingeweza kufanya mapenzi na mpunga ili kuzaa mtoto, lakini kwa GMO inafanyika, na hiyo ndio tofauti kubwa ya GMO na hybridization.

Kwenye GMO vinasaba vya konokono vinaweza kuunganishwa na vinasaba vya michungwa, kwenye hybridization kitu kama hicho hakiwezekani. Umenielewa?
 
Back
Top Bottom