Waziri Bashe hakutakiwa kuukataa msaada wa mchele kutoka Marekani na kama alikuwa na mashaka yoyote angewatumia TBS

Waziri Bashe hakutakiwa kuukataa msaada wa mchele kutoka Marekani na kama alikuwa na mashaka yoyote angewatumia TBS

Kwa hiyo tukatae bila sababu? Kwa hiyo tukikumbwa na baa la njaa na ukahitajika msaada wa dharula , Marekani ikawa tayari mtagoma au mtakubali? Wengi nayaona mashaka waliyonayo ni juu ya usalama na sio nia na dhamira ya msaada huo
Subiri tupate njaa ndio tuombe huo misaada,sasa hivi hatuna shida na Michele,na sababu Mh. Bashe alizitoa,kaangalie alichosema maana unakurupuka
 
Mada hii ni kuelezea mashaka makubwa niliyonayo kwa Waziri wetu wa kilimo namna maamuzi yake yanavyoweza kuharibu mahusiano ya kimataifa kama asipojirekebisha.

Kwanza kabisa nianze Kwa 'declare interest' ,Sina mahusiano ya aina yoyote na NGO iliyoleta mchele wa msaada wenye virutubisho kutoka nchini Marekani chini ya kampeni ya wizara ya kilimo ya Marekani inayoitwa "Pamoja tuwalishe" na 'interest' pekee niliyonayo ni Kwa maslahi mapana ya nchi yangu .

Siku zote mjumbe hauawi na hiyo NGO inabaki kuwa ni mjumbe tu wa wizara ya kilimo ya Marekani ,kitendo Cha Waziri kuonesha kukasirishwa na kitendo Cha mjumbe kinaleta picha isiyopendeza.

Kwa mtazamo wangu badala ya Waziri Bashe kuonesha kukasirishwa na kuletwa Kwa mchele na hiyo NGO angetumia nafasi hiyo kufanya "formal communication" na wizara ya kilimo ya Marekani juu ya mambo tunayohitaji.

Kwa kuwa mchele huo ni msaada sikuona ulazima wowote wa Waziri kusema kwamba mchele tunao ,Kwa kuwa lengo la kampeni hiyo ni zuri ,tunatakiwa kuupokea msaada huo na kushukuru na wizara ingetumia TBS kuchunguza ubora wa mchele huo kimya kimya kabla haujaanza kutumika na kama kungekuwa na mashaka yoyote Serikali ingekataa baada ya kufanyika Kwa uchunguzi na ubora na sio Kwa hoja za Waziri.

Mashaka niliyonayo kwa Waziri Bashe ni kuwa:

Kama Waziri hajui athari za kimahusiano zinazoweza kuibuka kutokana na kauli tu. Kitendo Cha Waziri Bashe kudai Kwa nini wasingeleta virutubisho wachanganye tukiwaona ,sio rafiki Kwa afya ya diplomasia. Kitendo hicho kinaweza kufikirika kama tuhuma ya usalama. Kabla ya kauli hiyo alitakiwa kuwatumia TBS kuuchunguza mchele.

Marekani ni Moja ya nchi zinazozalisha nataka ( mchele na mahindi) Kwa wingi duniani na kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa ,nchi yetu inaweza kukumbwa na baa la njaa na tukahitaji msaada wa Chakula kutoka nje. Je, tutapata wapi nguvu za kuomba msaada kutoka Marekani kama tumeamua kukataa msaada Sasa ?

Pengine kulikuwa na Cha zaidi ambacho hatukijui lakini kama ni hiki kilichopo ,ni vema Waziri Bashe angeliendea suala Hilo Kwa busara, angejiridhisha kwanza na angejua hatua Kwa busara ili tuendelee kuimarisha mahusiano na nchi nyingine.

Kila siku Rais anasisitiza mifumo kusomana ili kuepusha migogoro , na kama mifumo ingekuwa inasomana kusingekuwa na kauli za namna Ile kutoka Kwa Waziri.

Ahsante
Waziri huyu amekosea sana kutoa kauli ya namna hii, inaharibu mahusiano mema ya kidiplomasia ya kimataifa.Alipaswa kuziagiza Mamlaka za nchi zinazohusika na masuala ya Uhakiki na Udhibiti ubora na Usalama wa Chakula ili kuchunguza ubora wa mchele huo. Je, huo mchele umeingia hapa nchini kutoka huko ulikotoka nje ya nchi kupitia njia gani? Je, ulipofika mpakani (border post) katika nchi yetu haukukaguliwa ubora wake?????
Akumbuke kwamba: Tanzania inaihitaji sana Marekani, washirika wake pamoja na Misaada yao, Tawala za Nchi zetu hizi za ki-Afrika kamwe haziwezi kutawala watu wala kuendesha Serikali katika nchi zao bila ya kupata Misaada kutoka kwa Marekani na washirika wake.
 
Nchi ombaomba tulishazoea misaada ya kila aina tangu enzi na milele yote.
 
Waziri huyu amekosea sana kutoa kauli ya namna hii, inaharibu mahusiano mema ya kidiplomasia ya kimataifa.Alipaswa kuziagiza Mamlaka za nchi zinazohusika na masuala ya Uhakiki na Udhibiti ubora na Usalama wa Chakula ili kuchunguza ubora wa mchele huo. Je, huo mchele umeingia hapa nchini kutoka huko ulikotoka nje ya nchi kupitia njia gani? Je, ulipofika mpakani (border post) katika nchi yetu haukukaguliwa ubora wake?????
Hakuna sehemu Bashe aligusia usalama wa huo Michele,acheni uwongo
 
Namuunga mkono Bashe. Kukubali msaada wa mchele kutoka marekani ni matusi na fedheha kwa wakulima wa Tanzania.

Wakulima wapewe hizo fedha wa_supplay mchele kwenye hizo shule
 
Kuomba kupewa msaada au kupewa msaada bila kuomba yote hayaondoi maana halisi ya neno msaada. Ni jukumu la msaidiwa kuangalia ubora wa msaada na hapa kwenye suala la mchele, tungewatumia TBS
Issue wala hata sio Ubora wala TBS.
Issue ni kuwa wameleta kitu ambacho kipo na Kubaki.
Hatuhitaji mchele kutoka nje kwa sasa.
Kama wanahisi mchele wetu hauna virutubisho waje waweke hapahapa.

Kingine ni kuwa Bashe kakataa akiwa anaelewa ni kina nani wapo nyuma ya hiyo NGO.
 
Hakuna sehemu Bashe aligusia usalama wa huo Michele,acheni uwongo
Tatizo lako umejazwa upofu wa kutokusoma katikati ya mstari. Bashe amesema kama ni virutubisho Kwa nini visingeletwa hapa vichanganywe tukiona. Hiyo kauli kwako unamaanisha nini?
 
Mada hii ni kuelezea mashaka makubwa niliyonayo kwa Waziri wetu wa kilimo namna maamuzi yake yanavyoweza kuharibu mahusiano ya kimataifa kama asipojirekebisha.

Kwanza kabisa nianze Kwa 'declare interest' ,Sina mahusiano ya aina yoyote na NGO iliyoleta mchele wa msaada wenye virutubisho kutoka nchini Marekani chini ya kampeni ya wizara ya kilimo ya Marekani inayoitwa "Pamoja tuwalishe" na 'interest' pekee niliyonayo ni Kwa maslahi mapana ya nchi yangu .

Siku zote mjumbe hauawi na hiyo NGO inabaki kuwa ni mjumbe tu wa wizara ya kilimo ya Marekani ,kitendo Cha Waziri kuonesha kukasirishwa na kitendo Cha mjumbe kinaleta picha isiyopendeza.

Kwa mtazamo wangu badala ya Waziri Bashe kuonesha kukasirishwa na kuletwa Kwa mchele na hiyo NGO angetumia nafasi hiyo kufanya "formal communication" na wizara ya kilimo ya Marekani juu ya mambo tunayohitaji.

Kwa kuwa mchele huo ni msaada sikuona ulazima wowote wa Waziri kusema kwamba mchele tunao ,Kwa kuwa lengo la kampeni hiyo ni zuri ,tunatakiwa kuupokea msaada huo na kushukuru na wizara ingetumia TBS kuchunguza ubora wa mchele huo kimya kimya kabla haujaanza kutumika na kama kungekuwa na mashaka yoyote Serikali ingekataa baada ya kufanyika Kwa uchunguzi na ubora na sio Kwa hoja za Waziri.

Mashaka niliyonayo kwa Waziri Bashe ni kuwa:

Kama Waziri hajui athari za kimahusiano zinazoweza kuibuka kutokana na kauli tu. Kitendo Cha Waziri Bashe kudai Kwa nini wasingeleta virutubisho wachanganye tukiwaona ,sio rafiki Kwa afya ya diplomasia. Kitendo hicho kinaweza kufikirika kama tuhuma ya usalama. Kabla ya kauli hiyo alitakiwa kuwatumia TBS kuuchunguza mchele.

Marekani ni Moja ya nchi zinazozalisha nataka ( mchele na mahindi) Kwa wingi duniani na kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa ,nchi yetu inaweza kukumbwa na baa la njaa na tukahitaji msaada wa Chakula kutoka nje. Je, tutapata wapi nguvu za kuomba msaada kutoka Marekani kama tumeamua kukataa msaada Sasa ?

Pengine kulikuwa na Cha zaidi ambacho hatukijui lakini kama ni hiki kilichopo ,ni vema Waziri Bashe angeliendea suala Hilo Kwa busara, angejiridhisha kwanza na angejua hatua Kwa busara ili tuendelee kuimarisha mahusiano na nchi nyingine.

Kila siku Rais anasisitiza mifumo kusomana ili kuepusha migogoro , na kama mifumo ingekuwa inasomana kusingekuwa na kauli za namna Ile kutoka Kwa Waziri.

Ahsante
Umatumwa!? Nchi hii haijafikia hatua hiyo ya kupokea misaada ya chakula, tuna mahitaji mengi zaidi ya mchele wa maabara so waambie mabwana zako hatuhutaji misaada hatarishi. Wapeleke Congo na Somalia kwenye janga la vita na njaa.
 
Back
Top Bottom