Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Bashungwa ameongoza uhamasishaji huo leo tarehe 15, Oktoba, 2024 mara baada ya kujiandikisha katika Daftari la Wapiga Kura katika Kituo cha Ahakishaka Kata ya Nyabiyonza Wilayani Karagwe, Mkoani Kagera ambapo zoezi hilo lilianza rasmi tarehe 11 Oktoba, 2024 na litamalizika tarehe 20 Oktoba, 2024.
Bashungwa ametoa wito kwa Wananchi kuendelea kudumisha umoja na mshikamano kwa kuwa ndio msingi wa kuleta maendeleo katika Vijiji na kata zote za Wilaya ya Karagwe.
Aidha, Bashungwa ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan tayari imetoa kiasi cha Shilingi Milioni 647 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya katika katika ukanda wa Bushangaro ambacho kitajengwa Ahakishaka.
Kwa upande wake, Katibu wa Jumuiya ya Kufa na Kuzikana (Tupendane) ya Ahakishaka Kata ya Nyabiyonza, Bw. Festo Mtele amemshukuru Mbunge kuungana na wananchi wa Wilaya ya Karagwe kujiandikisha kwenye Daftari la Wapiga Kura na kuhamasisha wananchi kujitokeza kujiandikisha ili kuchagua viongozi wa Serikali za Mitaa.