LGE2024 Waziri Bashungwa aongoza uhamasishaji Wananchi wa Karagwe kujiandikisha Daftari la Wapiga Kura

LGE2024 Waziri Bashungwa aongoza uhamasishaji Wananchi wa Karagwe kujiandikisha Daftari la Wapiga Kura

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
WhatsApp Image 2024-10-15 at 17.00.47_9bf461b8.jpg
Waziri wa Ujenzi na Mbunge wa Jimbo la Karagwe, Innocent Bashungwa ameongoza zoezi la uhamasishaji kwa Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe kuendelea kujitokeza katika vituo vya kujiandikisha kwenye Daftari la Wapiga Kura ili waweze kutimiza haki yao kikatiba ya kushiriki katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika tarehe 27 Novemba, 2024.

Bashungwa ameongoza uhamasishaji huo leo tarehe 15, Oktoba, 2024 mara baada ya kujiandikisha katika Daftari la Wapiga Kura katika Kituo cha Ahakishaka Kata ya Nyabiyonza Wilayani Karagwe, Mkoani Kagera ambapo zoezi hilo lilianza rasmi tarehe 11 Oktoba, 2024 na litamalizika tarehe 20 Oktoba, 2024.
WhatsApp Image 2024-10-15 at 17.04.21_511534f5.jpg

WhatsApp Image 2024-10-15 at 17.04.22_27d2413e.jpg
“Nichukue nafasi hii kupaza sauti kwa kile ambacho Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na viongozi wengine wameendelea kusisitiza wananchi kujitokeza kwa ajili ya kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura, Nendeni mkajiandikishe na tuwakumbushe wenzetu ambao bado hawajajiandikisha kufanya hivyo kwa siku zilizobakia“, amesisitiza Bashungwa.

Bashungwa ametoa wito kwa Wananchi kuendelea kudumisha umoja na mshikamano kwa kuwa ndio msingi wa kuleta maendeleo katika Vijiji na kata zote za Wilaya ya Karagwe.

Aidha, Bashungwa ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan tayari imetoa kiasi cha Shilingi Milioni 647 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya katika katika ukanda wa Bushangaro ambacho kitajengwa Ahakishaka.
WhatsApp Image 2024-10-15 at 17.00.46_3f38521e.jpg
“Kama mnavyofahamu Wilaya ya Karagwe ina tarafa tano (5) na tayari tarafa ya Nyaishozi, Bugene, Kituntu zimeshapata vituo vya afya na sasa ni zamu ya Nyabiyonza, kituo cha afya kinajengwa na fedha zishaletwa na kwa tarafa ya Nyakakika mipango inaendelea”. ameongeza Bashungwa.

Kwa upande wake, Katibu wa Jumuiya ya Kufa na Kuzikana (Tupendane) ya Ahakishaka Kata ya Nyabiyonza, Bw. Festo Mtele amemshukuru Mbunge kuungana na wananchi wa Wilaya ya Karagwe kujiandikisha kwenye Daftari la Wapiga Kura na kuhamasisha wananchi kujitokeza kujiandikisha ili kuchagua viongozi wa Serikali za Mitaa.
 

WhatsApp Image 2024-10-15 at 17.04.22.jpeg

Waziri wa Ujenzi na Mbunge wa Jimbo la Karagwe, Innocent Bashungwa ameongoza zoezi la uhamasishaji kwa Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe kuendelea kujitokeza katika vituo vya kujiandikisha kwenye Daftari la Wapiga Kura ili waweze kutimiza haki yao kikatiba ya kushiriki katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika tarehe 27 Novemba, 2024.

Bashungwa ameongoza uhamasishaji huo leo tarehe 15, Oktoba, 2024 mara baada ya kujiandikisha katika Daftari la Wapiga Kura katika Kituo cha Ahakishaka Kata ya Nyabiyonza Wilayani Karagwe, Mkoani Kagera ambapo zoezi hilo lilianza rasmi tarehe 11 Oktoba, 2024 na litamalizika tarehe 20 Oktoba, 2024.

“Nichukue nafasi hii kupaza sauti kwa kile ambacho Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na viongozi wengine wameendelea kusisitiza wananchi kujitokeza kwa ajili ya kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura, Nendeni mkajiandikishe na tuwakumbushe wenzetu ambao bado hawajajiandikisha kufanya hivyo kwa siku zilizobakia“, amesisitiza Bashungwa.


Bashungwa ametoa wito kwa Wananchi kuendelea kudumisha umoja na mshikamano kwa kuwa ndio msingi wa kuleta maendeleo katika Vijiji na kata zote za Wilaya ya Karagwe.

Aidha, Bashungwa ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan tayari imetoa kiasi cha Shilingi Milioni 647 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya katika katika ukanda wa Bushangaro ambacho kitajengwa Ahakishaka.

“Kama mnavyofahamu Wilaya ya Karagwe ina tarafa tano (5) na tayari tarafa ya Nyaishozi, Bugene, Kituntu zimeshapata vituo vya afya na sasa ni zamu ya Nyabiyonza, kituo cha afya kinajengwa na fedha zishaletwa na kwa tarafa ya Nyakakika mipango inaendelea”. ameongeza Bashungwa.

WhatsApp Image 2024-10-15 at 17.04.24.jpeg

Kwa upande wake, Katibu wa Jumuiya ya Kufa na Kuzikana (Tupendane) ya Ahakishaka Kata ya Nyabiyonza, Bw. Festo Mtele amemshukuru Mbunge kuungana na wananchi wa Wilaya ya Karagwe kujiandikisha kwenye Daftari la Wapiga Kura na kuhamasisha wananchi kujitokeza kujiandikisha ili kuchagua viongozi wa Serikali za Mitaa.

WhatsApp Image 2024-10-15 at 17.04.21(1).jpeg
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2024-10-15 at 17.04.23.jpeg
    WhatsApp Image 2024-10-15 at 17.04.23.jpeg
    517 KB · Views: 5
  • WhatsApp Image 2024-10-15 at 17.04.21.jpeg
    WhatsApp Image 2024-10-15 at 17.04.21.jpeg
    548.5 KB · Views: 4
  • WhatsApp Image 2024-10-15 at 17.04.20.jpeg
    WhatsApp Image 2024-10-15 at 17.04.20.jpeg
    618.2 KB · Views: 4
  • WhatsApp Image 2024-10-15 at 17.00.50.jpeg
    WhatsApp Image 2024-10-15 at 17.00.50.jpeg
    453.5 KB · Views: 6
  • WhatsApp Image 2024-10-15 at 17.00.47.jpeg
    WhatsApp Image 2024-10-15 at 17.00.47.jpeg
    403 KB · Views: 4
  • WhatsApp Image 2024-10-15 at 17.00.46.jpeg
    WhatsApp Image 2024-10-15 at 17.00.46.jpeg
    756.9 KB · Views: 3
  • WhatsApp Image 2024-10-15 at 17.00.45.jpeg
    WhatsApp Image 2024-10-15 at 17.00.45.jpeg
    391.4 KB · Views: 3
Back
Top Bottom