Waziri Bashungwa atoa siku 7 mabasi yote ya mikoani yawe yanaingia Magufuli Bus Terminal, si Shekilango

Waziri Bashungwa atoa siku 7 mabasi yote ya mikoani yawe yanaingia Magufuli Bus Terminal, si Shekilango

Stendi ya Magufuli ni Ndogo mbona viongozi wa kisiasa hawa wagumu kuelewa!?

Hivi abood, Alsaedy, Shabiby wakaleta gari zao kwa wakati mmoja si wanajaza stendi yote! Tuwe na busara
Wanasiasa hawana kauli za ukweli hata kama ukweli wanujua
Basi za kusini nyongibzinaondokea temeke na mbagala , kama hili nalo linawahusu hapo magufuli stand itakuwa ni kero
 
Stendi ya Magufuli ni Ndogo mbona viongozi wa kisiasa hawa wagumu kuelewa!?

Hivi abood, Alsaedy, Shabiby wakaleta gari zao kwa wakati mmoja si wanajaza stendi yote! Tuwe na busara
Kwa hiyo wanataka watu wote kupandia na kushuka stendi ya Magufuli wakati bus linaelekea mjini mpaka Shekilango au Mbagala likiwa tupu. Halafu wale abiria walioshuka stendi ya Magufuli waanze kuhangaika tena na usafiri wa kwenda Mbagala kwa pesa nyingine tena!!!!

Aliyewaloga viongozi wa CCM alishakufa!!! Hata mtoto wa darasa la 4 atashangaa!!!
 
Maamuzi mengine kama haya waziri anatakiwa akutane na wadau wa usafirishaji kwanza si kukurupuka tu. Mabasi yote yaingie magufuli, patatosha? Yaani gari la kwenda mtwara, kwa mfano liko temeke na abiria wote wanajua hilo kisha liende mbezi kwanza?

Hiyo magufuli bus terminal in ukubwa gani kuweza kubeba mabasi 200-300 kwa wakati mmoja? au ndiyo bado waziri anaishi zama za kumwabudu mtu na hivyo anadhani jina limeanza kufifia>
 
Waziri wa Tamisemi Mhe. Bashungwa leo amesisitiza mabasi yote yaendayo Mikoani pamoja na nchi jirani lazima yapakie na kushushia abiria katika kituo kikuu cha Mabasi cha Magufuli ameyasema hayo leo wakati akizungumza na wadau wa usafirishaji.

Ni vyema waziri kalizungumzia hilo maana hali ilipo kuwa imefikia ilikuwa ni vurugu yaani kama vile hakuna wasimamizi wa sheria au hakuna viongozi maana kila basi illikuwa inaamua ikapakie abiria wapi na ikashushie wapi!! askari wapo! wanaangalia jinsi watu wanavyo vunja sheria!!

Hapana, lazima kituo chetu cha Magufuli kitumiwe kama ilivyo kusudiwa, hivyo ni vyema wenye mamlaka wakasimamia hilo.

===

Waziri Bashungwa atoa siku saba Stendi Kuu ya Magufuli-Dar​


WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Innocent Bashungwa ametoa siku saba kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla kukutana na LATRA, Wadau na Wamiliki wa Mabasi kuweka uratibu mzuri wa kusimamia maelekezo ya Serikali kwa mabasi yote kushusha na kupakia abiria ndani ya Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli jijini Dar es Salaam.


Bashungwa ametoa maelekezo hayo leo Mei 30, 2022 wakati akikagua mradi wa Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli (Magufuli Bus Terminal) kilichopo Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam.

Amesema, Serikali imetumia kiasi cha shilingi bilioni 50 kujenga kituo hicho, hivyo Serikali haitakubaliana na watu ambao hawazingatii utaratibu uliowekwa katika kituo hicho.

“Ninafahamu kuwa Mkuu wa Mkoa, Amos Makalla ameshapokea changamoto ya Mabasi kutoingia ndani ya kituo hiki cha Magufuli na mimi nimekuta changamoto bado iko pale pale, sasa kwa sababu ameshanza kulifanyia kazi nampa siku saba awe amekutana na LATRA pamoja na wadu wa mabasi (TABOA) kuangalia utaratibu wa mabasi yote kuingia ndani ya kituo kushusha na kupakia abiria,”amesema Bashungwa.

Pia Mheshimiwa Bashungwa amemuagiza Mkuu wa Wilaya Ubungo, Kheri James kuweka utaratibu wa kukutana mara kwa mara na Wadau wa Kituo cha Magufuli, Mawakala na Makalani ili kusikiza na kuweka utaratibu wa kutatua changamoto ambazo zimekuwa zikijitokeza katika kituo hicho na kuzifanyia kazi kwa ushirikiano.
Hiyo stend haiwezi kuhimili mabasi yote Kwa Muda wa Asubhi aache utani
 
Ingawa waziri amechelewa kutoa hilo tamko wasiwasi wangu watamtii? Watu wa mabasi ni wakorofi sana. Kuna makampuni kama Dar Express hata Arusha hawaingii stand kuu, Dar wanashusha na kupakia pale Shekilango walinipa shida sana siku moja wakati huo nilitakiwa niunganishe safari kwenda kusini Tunduru kumbuka una mizigo nilipata gharama ya ziada. Hata mabasi yayotoka kusini km Lindi, Mtwara, Masasi, Tnduru, Songea yanaishia Temeke mwisho. Fikiria kesho yake unatakiwa uunge kwenda kaskazini Arusha una mizigo unafikaje stand ya Magufuli. Nawashangaa LATRA ni mpaka waziri awaboost? na Jeshi la Polisi je? Taasisi nyingi za nchi hii zina shida sana.
Hawakufikiri kabla ya kujenga
 
Mkuu, Kuna magari hayaingii kabisa pale. Mfano, tahmeed, Kilimanjaro, bm, etc.

Kifupi gari nyingi za kwenda kaskazini zinazopaki Shekilango hazipiti Mbezi(asubuhi) na haziingii(kwa zinazotoka mkoani).
Sasa kama hakuna ulazima, kwanini mlazimishe zipite?
 
Mtoa mada unafurahia ujinga tu bila kutumia Busara, Basi likianzia Mbagala halafu likaingia hapo Magufuli likalipa ushuru kama kawaida nini kitapungua? Kuna abiria wanatoka mbali sana kumbuka.
Well said. Hii serikali inalazimisha kufanya maisha ya wana Dar es Salaam kuwa magumu sana bila sababu ya msingi. Ili mtu atoke Chanika/ Vikindu, Kisarawe II, au Mgeni Nani awahi basi saa 12:00 asubuhi kituo cha Magufuli inabidi alale stendi. Kama atalala nyumbani kwake atalazimika kukodi usafiri ambao utamgharimu fedha nyingi sana. Baadhi ya makampuni ya mabasi yameweka utaratibu wa kuanzia maeneo mbalimbali na abiria, na baadaye ayanapita Stendi ya Magufuli yanachukua abiria wanapandia hapo, hayapitizi kabisa. Vile vile mabasi yanayoanzia Urafiki yanachukua abiria wa maeneo ya karibu na hapo yanaondoka nao hadi stendi ya Magufuli yanalipa ushuru, shida iko wapi?
 
Mtoa mada unafurahia ujinga tu bila kutumia Busara, Basi likianzia Mbagala halafu likaingia hapo Magufuli likalipa ushuru kama kawaida nini kitapungua? Kuna abiria wanatoka mbali sana kumbuka.
Hii ni kutaka kuwatesa abiria tu, Abiria anayetokea mbagala akodishe taxi kutoka mbagala mpaka stendi ya Magufuli atatozwa bei gani ??!! Au waziri amesahau kuwa watu wengi nchi hii hawana magari ya kutembelea !! Na Madaladala asubuhi huwa ni vurugu tu na kuibiana !! Kuna tatizo gani abiria wakipandia sehemu nyingine baadhi yao na kisha Bus lipitie hapo Stendi ya Magufuli ??
 
Kweli kabisa !! Huwa wanasahau kuwa watu wengi nchi hii wana hali ngumu za maisha !! Waswahili husema " ALIYESHIBA HAMJUI MWENYE NJAA "
Well said. Hii serikali inalazimisha kufanya maisha ya wana Dar es Salaam kuwa magumu sana bila sababu ya msingi. Ili mtu atoke Chanika/ Vikindu, Kisarawe II, au Mgeni Nani awahi basi saa 12:00 asubuhi kituo cha Magufuli inabidi alale stendi. Kama atalala nyumbani kwake atalazimika kukodi usafiri ambao utamgharimu fedha nyingi sana. Baadhi ya makampuni ya mabasi yameweka utaratibu wa kuanzia maeneo mbalimbali na abiria, na baadaye ayanapita Stendi ya Magufuli yanachukua abiria wanapandia hapo, hayapitizi kabisa. Vile vile mabasi yanayoanzia Urafiki yanachukua abiria wa maeneo ya karibu na hapo yanaondoka nao hadi stendi ya Magufuli yanalipa ushuru, shida iko wapi?
 
Waziri wa Tamisemi Mhe. Bashungwa leo amesisitiza mabasi yote yaendayo Mikoani pamoja na nchi jirani lazima yapakie na kushushia abiria katika kituo kikuu cha Mabasi cha Magufuli ameyasema hayo leo wakati akizungumza na wadau wa usafirishaji.

Ni vyema waziri kalizungumzia hilo maana hali ilipo kuwa imefikia ilikuwa ni vurugu yaani kama vile hakuna wasimamizi wa sheria au hakuna viongozi maana kila basi illikuwa inaamua ikapakie abiria wapi na ikashushie wapi!! askari wapo! wanaangalia jinsi watu wanavyo vunja sheria!!

Hapana, lazima kituo chetu cha Magufuli kitumiwe kama ilivyo kusudiwa, hivyo ni vyema wenye mamlaka wakasimamia hilo.

===

Waziri Bashungwa atoa siku saba Stendi Kuu ya Magufuli-Dar​


WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Innocent Bashungwa ametoa siku saba kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla kukutana na LATRA, Wadau na Wamiliki wa Mabasi kuweka uratibu mzuri wa kusimamia maelekezo ya Serikali kwa mabasi yote kushusha na kupakia abiria ndani ya Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli jijini Dar es Salaam.


Bashungwa ametoa maelekezo hayo leo Mei 30, 2022 wakati akikagua mradi wa Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli (Magufuli Bus Terminal) kilichopo Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam.

Amesema, Serikali imetumia kiasi cha shilingi bilioni 50 kujenga kituo hicho, hivyo Serikali haitakubaliana na watu ambao hawazingatii utaratibu uliowekwa katika kituo hicho.

“Ninafahamu kuwa Mkuu wa Mkoa, Amos Makalla ameshapokea changamoto ya Mabasi kutoingia ndani ya kituo hiki cha Magufuli na mimi nimekuta changamoto bado iko pale pale, sasa kwa sababu ameshanza kulifanyia kazi nampa siku saba awe amekutana na LATRA pamoja na wadu wa mabasi (TABOA) kuangalia utaratibu wa mabasi yote kuingia ndani ya kituo kushusha na kupakia abiria,”amesema Bashungwa.

Pia Mheshimiwa Bashungwa amemuagiza Mkuu wa Wilaya Ubungo, Kheri James kuweka utaratibu wa kukutana mara kwa mara na Wadau wa Kituo cha Magufuli, Mawakala na Makalani ili kusikiza na kuweka utaratibu wa kutatua changamoto ambazo zimekuwa zikijitokeza katika kituo hicho na kuzifanyia kazi kwa ushirikiano.
Wamiliki wa mabasi pamoja na wananchi hawapendi jina la kituo hicho, hawakutaka kiitwe magufuli, wanamchukia sana
 
Naamini Jeshi la Polisi ndio jukumu lao kusimamia utekelezaji wa sheria na taratibu, hivyo watakuwa imara zaidi.
ni aibu kuona sheria zinavunjwa wakati wasimamizi wapo, viongozi wapo!

Stendi ya Kimataifa ya Magufuli imekuwa Gumzo ktk nchi zingine kwa kuwa kituo kikubwa na cha kisasa, hivyo ni muhimu viongozi wetu wakaelewa kuwa STENDI YA MABASI YA MAGUFULI ni UCHUMI wa NCHI.

SERIKALI imewekeza 50Billion sasa tunaanza kufanya mzaha na kupuuza kwa nini? Hapana hii haikubaliki.
CAG akikagua hiyo bilioni 50, tutarudi hapa tumeshikana masharti, bilioni 50 na bado stendi haijaisha
 
Waziri wa Tamisemi Mhe. Bashungwa leo amesisitiza mabasi yote yaendayo Mikoani pamoja na nchi jirani lazima yapakie na kushushia abiria katika kituo kikuu cha Mabasi cha Magufuli ameyasema hayo leo wakati akizungumza na wadau wa usafirishaji.

Ni vyema waziri kalizungumzia hilo maana hali ilipo kuwa imefikia ilikuwa ni vurugu yaani kama vile hakuna wasimamizi wa sheria au hakuna viongozi maana kila basi illikuwa inaamua ikapakie abiria wapi na ikashushie wapi!! askari wapo! wanaangalia jinsi watu wanavyo vunja sheria!!

Hapana, lazima kituo chetu cha Magufuli kitumiwe kama ilivyo kusudiwa, hivyo ni vyema wenye mamlaka wakasimamia hilo.

===

Waziri Bashungwa atoa siku saba Stendi Kuu ya Magufuli-Dar​


WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Innocent Bashungwa ametoa siku saba kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla kukutana na LATRA, Wadau na Wamiliki wa Mabasi kuweka uratibu mzuri wa kusimamia maelekezo ya Serikali kwa mabasi yote kushusha na kupakia abiria ndani ya Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli jijini Dar es Salaam.


Bashungwa ametoa maelekezo hayo leo Mei 30, 2022 wakati akikagua mradi wa Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli (Magufuli Bus Terminal) kilichopo Wilaya ya Ubungo jijini Dar es Salaam.

Amesema, Serikali imetumia kiasi cha shilingi bilioni 50 kujenga kituo hicho, hivyo Serikali haitakubaliana na watu ambao hawazingatii utaratibu uliowekwa katika kituo hicho.

“Ninafahamu kuwa Mkuu wa Mkoa, Amos Makalla ameshapokea changamoto ya Mabasi kutoingia ndani ya kituo hiki cha Magufuli na mimi nimekuta changamoto bado iko pale pale, sasa kwa sababu ameshanza kulifanyia kazi nampa siku saba awe amekutana na LATRA pamoja na wadu wa mabasi (TABOA) kuangalia utaratibu wa mabasi yote kuingia ndani ya kituo kushusha na kupakia abiria,”amesema Bashungwa.

Pia Mheshimiwa Bashungwa amemuagiza Mkuu wa Wilaya Ubungo, Kheri James kuweka utaratibu wa kukutana mara kwa mara na Wadau wa Kituo cha Magufuli, Mawakala na Makalani ili kusikiza na kuweka utaratibu wa kutatua changamoto ambazo zimekuwa zikijitokeza katika kituo hicho na kuzifanyia kazi kwa ushirikiano.
Nchi ya matamko

Mama anaridhika na matamko na usingizi mzuri anaupata[emoji1787]
 
Huyu Waziri hajui kwamba anazipunguza kwa wingi kura za CCM mwaka 2025 kwa amri anazotoa.
 
We
Stendi ya Magufuli ni Ndogo mbona viongozi wa kisiasa hawa wagumu kuelewa!?

Hivi abood, Alsaedy, Shabiby wakaleta gari zao kwa wakati mmoja si wanajaza stendi yote! Tuwe na busara
Wenye kupambana na Hali Yao wanatamani Mabasi yawachukue karibia na wanakoishi, ila wanasiasa wasiojua ukubwa WA dar, na ambao wanawachanganya wenye mabasi waliotoa huruma kuwasaidia wananchi wao wapo dodoma wanasababishia Dar matatizo, huyu Waziri sijui anatafakari vipi!?
 
Huyu Waziri hajui kwamba anazipunguza kwa wingi kura za CCM mwaka 2025 kwa amri anazotoa.
Hajui analolifanya Kwa kweli sijui kinamuwasha nini huyu Mtu, alizuia boda boda kuwekewa utaratibu na kuvuruga Jiji lote na Bado anazidi kufanya mambo yake ya kuchefua watu
 
Back
Top Bottom