Waziri Dkt. Mwigulu ataka sheria zitafsiriwe kwa lugha ya Kiswahili

Waanzie huko vyuoni wanakofundishia Sheria kwa lugha ya kingereza.
 
Hii nchi hii,
Itoshe kusema viongozi wetu wanaturudisha sanaa nyuma
unarudishwa nyuma kwa kutumia kiswahili🙄🙄??
kizungu chenyewe utakuta hukijui ni ulimbukeni tu kutaka kuonekana unajua 😏😏
 
Rafiki sheria ya Tz haiishi hapa Tanzania tu, kuna nchi za jumuia ya madola nao wanaziangalia pia na kuzitumia.

Zaidi ya yote, sheria ni taaluma na lugha ya taaluma Tz ni kiingereza

Usisahau kiswahili ni lugha ya taifa na si lugha ya taaluma.
ukitaka hukatazwi kujifunza lugha ya kiingereza kwa ajili ya mawasiliano inapo bidi, hata taifa la urusi lugha yao ni kirusi na inapo bidi wana wasiliana kwa kiingereza kupitia mkalimani.
waziri amewazungumzia watanzania ambao ndio wengi wanatafuta haki zao kila kukicha wapo mahakamani na polisi..kuwa sheria na Hukumu zinazo tolewa ziwe kwa lugha ya taifa lao,
 
Official languages za Tanzania ni mbili:
1) English
2) Swahili

Kama lugha yetu rasmi ya kwanza ni English, kwa nini kusifanyike utaratibu utakaowezesha Watanzania kuzijua vizuri lugha zet zote mbili zilizo rasmi.

Hapo zamani Watanzania hawakuwa na lugha ya Kiswahili lakini kwa jitihada mbalimbali, leo sote tunajua. Kwa nini isifanyike hivyo hivyo kwa Kiingereza? Mtu mmoja kushindwa kukimudu Kiingereza isiwe sababu ya kubadilisha mfumo mzima wa matumizi ya lugha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Huo mfumo wa matumizi ya lugha ya Kiingereza ktk shughuli za kiserikali ulikuwa ni mfumo/utaratibu ulio wekwa navwakoloni Kwa faida ya wakoloni Kwa sasa hakuna haja ya kutumia kiingereza ktk shughuli zote ZA serikali hiyo haimaanishi kuwa umekatazwa kujifunza kiingereza bali utajifunza tu kama ilivyo Kichina au kifaransa, ila ktk matumizi ya serikali haswa ktk utoaji haki hakuna sababu yoyote ya kutumia lugha ya kigeni/kiingereza au Kichina au kifaransa wakati tuna lugha yetu iliyo jitosheleza kiswahili.
Hata hivyo lazima wapo "watumwa" wachache watapinga na kubeza kwa masilahi yao binafsi lkn hatua iliyo fikiwa na serikali ni safi sana
 
Na hapa Afrika ni nchi gani inayotumia lugha yao ya asili?
 
Imepita miaka mingapi mnatumia Kiingereza kama Official language kwenye idara nyeti na maisha yakasonga upambavu wenu unawafanya mjione wajuaji wakati ni zero brained huyo ncheba aliiba pesa huko EPA leo anataka kuihujumu sheria.
 
Kabudi na Mwakyembe ni wanasheria wabobezi lakini wameshindwa kulinda taaluma zao kwa kisingizio cha kuokotwa majalalani shem on them hata tutumie lugha zetu za kuzaliwa kama kuna mtu anadharau sheria haisaidii kitu ataendendelea tu kutupumbaza kwa sababu mamlaka anayo,hela anayo,dola anayo,mahakama ni za kwake,polisi ni wake,jeshi ni lake nk.hapo hakuna ahueni jitahidini kutumia akili Kikwete alishasema.
 
Ukweli mtupu, mbumbumbu watakupinga.
 
Unaweza kumpeleka ng'ombe mtoni, lakini huwezi kumlazimisha kunywa maji.

Pia, ukweli kwamba huwezi kumlazimisha ng'ombe kunywa maji, hauondoi umuhimu wa kumpeleka ng'ombe mtoni.

Uko sahihi kwamba Watanzania wengi sana hawaelewi sheria hata zilizoandikwa Kiswahili. Hata katiba.

Lakini pia, kuna wengine wengi hawaelewi kwa sababu sheria hazijaandikwa Kiswahili.

Serikali inatakiwa kufanya sheria ziweze kueleweka na watu wasiojua Kiingereza. Kama baada ya kutafsiri watu bado hawataelewa sheria, hilo ni tatizo lingine. Ama utashi, ama elimu. Lakini tatizo la lugha linakuwa limeondolewa.

Mimi nashangaa mpaka leo, miaka 59 baada ya uhuru wa Tanganyika, kuna sheria hazijatafsiriwa Kiswahili.

Kutafsiri sheria si kujenga mtambo wa nyuklia!

Wana kisingizio gani kutokuwa na sheria hizi katika Kiswahili?
 
Ni vizuri kutumia Kiswahili nchini.
Lakini hiyo haindoi ukweli kwamba English ni muhimu kwa kila mtu.

Au utajifungia tanzania milele kwenye kila kitu.
 
....Sheria ina lughà yake ngumu sana kuelewa kwenye lughà yoyote hata kwa wanasheria wenyewe ndo maana Katiba na Sheria hata kwenye matumizi ya kawaida tafsiri halisi hutolewa na Mahakama Kuu baada ya kupitiwa na jopo la Majaji.
Huu ndo ukweli mchungu ambao wengi hawajui au wanafumbia macho makusudi.

Matumizi ya kiswahili hayawezi kufanya sheria iwe rahisi. Hata majaji na maprofesa wa sheria ambao pia ni wajuzi wa lugha, hutofautiana ktk tafsiri ya vifungu vya sheria, na ndo sabb kunakuwa na rufaa nyingi.

Hivyo, hata ukiondoa "kikwazo" cha lugha, utata wa tafsiri za sheria utasalia.
 
Na hapa Afrika ni nchi gani inayotumia lugha yao ya asili?
usipo enzi lugha yako iko siku tutatumia lugha hata lugha ya kiarabu ktk shughuli za serikali kwa sababu tu eti kiarabu pia ni lugha ya kimataifa. Usipo kuwa na msimamo na kitu chako ukubali kuendeshwa kama gari bovu.
Lugha ya Taifa ni kielelezo cha utamaduni wa taifa letu na ni uthibitisho wa uzalendo.

kiswahili ni lugha pekee inayo kuwa kwa kasi sana...inazungumzwa na zIdi ya mataifa 10, mfano, Kenya, Burundi, Uganda, DRC Kongo, Rwanda, Malawi, Zambia, Djibuti, Somalia, Sudani, comoro, shelisheli n.k
Usikidharau kiswahili...na bado kila kukicha kinazidi kusambaaa kila kona ya dunia, nawashangaa sana wale wanao beza matumizi ya kiswahili ktk utoaji wa haki ktk mahakama zetu, Bunge n.k, wanao pinga wana maslahi binafsi na wabia wao mabeberu.
 
Mwigulu alivyo na akili finyu Law School siyo watunga sheria wala siyo wenye mamlaka ya kuzitafsiri hizo sheria.

Kama anataka kufanikisha hilo si aziamuru taasisi zinazohusika zifanye kazi ya kuzitafsiri hizo sheria na sheria mpya zinazotungwa ziwe na Swahili na English version.

Wao ndiyo wanatunga sheria huko bungeni kwanini wanazitunga kwa kingereza ?
 
Mwigulu angekuwa mwanasheria angeelewa kwanini miaka yote hii tumezitumia kwa kingereza na kiratini, yaache tuu yatukute haya ndo mambo ya siasa kuingilia taaluma akataze Sasa na wanasheria kuitwa wasomi
 
Unaweza kujifanya unajua sana lakini hiyo haitaondoa ukweli wa usichokijua.

Lugha ni kielelezo cha mambo mengi. Kulazimisha kutumia Kiswahili wakati Sheria zenyewe zinafundishwa kwa Kiingereza, mfumo wenyewe wa Sheria tunaoutumia ni wa UK (jumuia ya Madola), fani nyingine zote, na mfumo wote wa sheria ni wa Kiingereza, ni kukurupuka kwa hali ya juu.

Huwezi kuwa na uhuru wa lugha kama huna uhuru wa tekinolojia na uchumi. Ukilazimisha kutumia lugha yako, unajitesa mwenyewe. Dunia imekuwa hivyo tangu enzi za Yesu. Wayahudi walikuwa na lugha yao lakini kutokana na uduni wa tekinolojia, lugha iliyokuwa inatumika kwenye mambo yote ya kitaalam ilikuwa Kigiriki. Imekuwa hivyo kwa mataifa mengi.

Ni nchi gani maskini inayotumia lugha yake ya asili? Hakuna anayekukataza lakini ukifanya hivyo, utajitesa mwenyewe.

Huyo mkurupukaji Mwigulu, anayesema sheria zote zitafsiriwe kwa Kiswahili, atatafsiri na marejeo yote ya hukumu kutoka jumuiya ya madola kwenda kwenye Kiswahili? Atawapeleka wanasheria wote masomoni ili wakapate uoanishi mzuri wa walichojifunza toka Kiingereza kwenda Kiswahili?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kugeuza mfumo wote wa sheria kwenda kiswahili ni jambo jepesi lilitakiwa liwe limefanyika siku nyingi sana tangu uhuru wa nchi yetu. Ila nikuelezeni hakuna watu wenye kuathirika na ubeberu wa lugha kama wanasheria. Wanapenda mtuhumiwa aone mahakama kama mazingaumbwe tu halafu wauze haki. Pia wanaona kingereza ndio usomi na ni mikogo.
Lakini haki ndio taifa. Mwananchi ana haki kuelewewa shauri lake mwanzo hadi hukumu.
Mwingulu asiwe na yeye mtu wa maneno. Wanasheria wanahitaji kibano ili kukamilisha kiswahili kwenye sheria na usikilizaji wa kesi. Uanasheria ni usomi hata kwenye kiswahili wasiwe na shaka wataweza kuonesha mikogo yao.
 
Safi saana waziri,nakupongeza sana kwa kuliona hili.
ombi langu kwako ni kwamba tunaomba hao wataalam waanze na sheria za kazi ili tuweze kujipambania kwa mujibu wa sheria.
Maana tunashuhudia viongozi wetu watukufu mnaongea na wananchi kwenye maeneo mbalimbali ya nchi.
Lkn hata siku moja sijawaona mnapotembelea sehemu za kazi mkiongea na wafanyakazi kujua matatizo yao na kuwapa nafasi kueleza kero zao.
Tunatamani na sisi wafanyakazi mnapokuja viwandani,maofisini muongee na wafanyakazi wote badala ya kuongea na watawala tuu.
Sheria nyingi za kazi hazifuatwi,lakini pa kuongelea hakuna,ukizingatia waajiri wengi hawataki kusikia kitu inaitwa VYAMA VYA WAFANYAKAZI
ukirudi kwenye sheria unakutana na '' As per section(2)....'' nyingi.
hivyo wafanyakazi kubaki kama yatima.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…