Waziri Gwajima, kuna haki za watoto zinakiukwa wazi wazi. Hatua za kuwanusuru zinahitajika

Waziri Gwajima, kuna haki za watoto zinakiukwa wazi wazi. Hatua za kuwanusuru zinahitajika

Naiweka hii hoja hapa kama angalizo.

Wataalam wa usalama wachunguze ama wafuatilie hili suala la homeless hususan watoto na vijana. Wapo hatua moja kuingia kwenye makundi hatarishi hususan ya kigaidi kwani ni rahisi kwa watu wasio wema kupanga mashambulizi ya kushtukiza kwenye foleni, madhara yanaweza kuwalenga viongozi ama raia.

Tuwe na mpango mzuri wa kupunguza hali hii kwa kuwaondoa watoto barabarani wwpelekwe shule. Serikali inaweza endapo NIA itakuwepo
 
Serikali iandae Kambi Maalum za Ombaomba, ambazo zitakuwa kama Gereza. Yawepo majengo ya Shule kwa watoto kuanzia Darasa la kwanza mpaka Form Four. Wale Omba Omba watu wazima wapelekwe kwenye mashamba ya Serikali walime, wafuge, na pia wapewe ufundi Stadi na kutengeneza bidhaa kwa nembo ya Serikali iwe biashara yao. Yani Inshort iwe Taasisi inayojitegemea.
 
1. Serikali inaweza kuwa suluhisho kwa kuboresha huduma za elimu na kijamii. Kwa kuboresha mfumo wa elimu na kuhakikisha upatikanaji wa elimu bora kwa watoto wote, serikali inaweza kupunguza idadi ya watoto wanaoacha shule na kuishia kuomba hela mitaani. Pia, kwa kutoa huduma za kijamii kama vile afya na ustawi wa jamii, serikali inaweza kusaidia familia zenye mahitaji na hivyo kupunguza shinikizo la watoto kuomba hela mitaani ili kusaidia familia zao.

2. Serikali inaweza pia kuhakikisha upatikanaji wa ajira kwa familia za watoto. Kwa kuanzisha miradi ya ujasiriamali na kuwekeza katika sekta ambazo zinaweza kuajiri watu wengi, serikali inaweza kupunguza umaskini na hivyo kupunguza idadi ya watoto wanaoomba hela mitaani.

3. Kutoa msaada wa kifedha kwa familia zenye mahitaji. Serikali inaweza kuweka mikakati ya kutoa misaada ya kifedha kwa familia zenye watoto ili kusaidia katika mahitaji yao ya msingi. Hii itapunguza shinikizo la watoto kuomba hela mitaani ili kukidhi mahitaji yao ya kila siku.

4. Mashirika ya kiraia yanaweza kusaidia kwa kutoa msaada wa kisaikolojia na kijamii kwa watoto. Kupitia programu za ushauri nasaha na msaada wa kijamii, mashirika ya kiraia yanaweza kuwasaidia watoto wa mitaani kutambua njia nyingine za kutatua matatizo yao badala ya kuomba hela mitaani.

5. Mashirika ya kiraia yanaweza pia kuwezesha miradi ya elimu na stadi za maisha. Kwa kutoa mafunzo ya stadi za maisha na ujuzi wa kiufundi, mashirika ya kiraia yanaweza kuwasaidia watoto wa mitaani kupata njia mbadala za kujipatia kipato.

6. Mashirika ya kiraia yanaweza pia kushirikiana na serikali katika kutoa huduma za msingi kwa watoto wa mitaani. Kwa kuweka mikakati ya pamoja na serikali, mashirika ya kiraia yanaweza kusaidia katika utoaji wa huduma za afya, elimu, na malazi kwa watoto wa mitaani.

7. Jamii inaweza pia kuwa sehemu ya suluhisho kwa kuwajumuisha watoto wa mitaani katika mipango ya kusaidia watoto walio katika mazingira hatarishi. Kwa kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa kuwasaidia watoto wa mitaani na kuwajumuisha katika shughuli za kijamii, jamii inaweza kupunguza ubaguzi na unyanyapaa dhidi ya watoto hao na hivyo kuwapa fursa ya kuishi maisha Bora. Hili suala si la kukomeshwa na upande mmoja TUU, NI LETU SOTE. YAANI MIMI NA WEWE.
 
Maigizo ni mengi kuna watoto wanapita kuomba mitaani wengine wamekaa na vikongwe na walemavu hawapati haki ya kupata elimu na makuzi bora kwa mtoto hakuna hatua yoyote inayochukuliwa sasa sijui sheria ya mtoto ipo kimya au wizara kwenye usimamizi wa haki za watoto imeshindwa kusimamia kuhusu watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu ni namna gani wanasaidiwa.
 
Tunapoongelea mafanikio ya awamu ya 6.
Hatuwezi kuacha kumpongeza Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassa kwa Moyo wake Mtulivu wa kufikiria kuunda hii Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na makundi maalum, pamoja na kumteua Mhe Dr Dorothy Gwajima kuwa engine ya wizara hii.

Kwa wakazi wa Dar es Salaam na maeneo jirani wanajua vizuri tatizo la watoto waishio mitaani wanaotumikishwa kuombaomba jinsi lilivyokuwa kubwa hasa maeneo ya City Centre.

Miaka mitatu iliyopita kuanzia Fire [emoji91] ukiwa unapita Morogoro Road unaenda posta ama K/koo, Utakutana na kundi kubwa la watoto wanaoomba barabarani.

Ukipita hii barabara ya Ally Hassan Mwinyi Road, kuanzia Namanga, St Peter, Salenda Bridge mpaka posta mpya kuelekea Ferry utakutana na rundo la watoto wetu wa Tanzania.

Vile vile ukiwa unapita barabara ya Uhuru, kuanzia Ilala Boma, Congo - K/koo, Mnazi mmoja, mchafu koge, Kitumbini/Kiautu, CBE kwenda mpaka Ferry unakutana na kundi kubwa la watoto wakiwa wamechoka wanaomba omba barabarani.

Vilevile ukiwa unatokea Pugu Road /Nyerere Road, mpaka makutano ya Bibi Titi Road na Lumumba, Clock Tower, ukiwa unaelekea Posta ama Station kote huku utakutana makundi ya watoto
Waliokata tamaa na keaho yao[emoji24]

Mbaya zaidi ukiingia posta mpya pale tu Benjamin Tower ukishuka kwa daladala ama gari yako unapokelewa kwa kuzungukwa na mikono ya watoto wengi wa kitanzania waombaomba wengine wakiwa wamelala pale kwenye Korido za Mkapa tower.

Watakupokea kwa shikhamoo za kulipia huku wananyoosha mikono yao, wakiwa wamekuzunguka na kukusindikiza kwa mita mia.
Maeneo yoote mpaka Chuo cha Ifm Ocean Road Hospital, Jimkhana Beach
Kule kote kulikuwa na watoto hao wanaotumikishwa na kujitumikisha kuchafua taswira ya taifa pamoja na kuutweza utu wao bila wenyewe kujua.

Mara tu baada ya wizara ya Maendeleo kuundwa, waziri Gwajima haraka aliunda Kamati Maalum ya Taifa (TASK FORCE). Ya kumtengamanisha huyo anayetumikishwa mtaani, huku akiwa anakosa haki zake nyingi za msingi kama binadamu.

Mara baada ya kamati hii ya taifa leo tunaona hata kule Ferry kwenye mabanda ya kukaanga samaki na kule wanapifanya mnada wa samaki wale watoto waliokuwa wakitumikishwa kupaa magamba ya samaki hawapo tena baada ya kampeni mbalimbali za uelimishaji kwa jamii.
Kamati hii inafanya kazi nyingi ikiwemo kuvijengea uwezo vituo vya kulea watoto, pia kuwajengea uwezo wazazi na walezi ili kupunguza tatizo la udumavu wa malezi, pamoja na kuwapa watoto wahanga nafasi mpya ya kurudi shule kupata haki ya elimu, watoto waliovuka umri wa miaka 14 - 16 wanapelekwa vyuo vya ufundi kupata taaluma yeyote ya ufundi kama Veta na vyuo vingine stadi.
Leo tunashuhuda za watoto wengi walionusuliwa na kamati hii kupelekwa pale kurasini kwenye makao ya Serikali ya kulea watoto.

Kuhusu wale watoto watano pale ferry kwenye banda la abiria,
Watoto wawili wanatumika na wazazi wao baba na mama yao.
Watoto wawili wanatumikishwa na Shangazi yao na mtoto mmoja anatumikishwa na Dalali ambaye analipa elfu 30000 kila jumamosi kwa mama mdogo wa mtoto huyo, ambaye yeye ndiye mlezi wa mtoto huyo wa kiume mwenye umri wa miaka 10 aliyefiwa na mama yake mzazi.

Kamati ipo kazini chini ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii
Ikiongozwa na Jemadari wetu Dr Dorothy Gwajima Wazir.

Lkn SISI SOTE KAMA WANA JAMII TUNATAKIWA TUUNGANE KWA UMOJA WETU KUKEMEA MATENDO YOOTE YA UVUNJIFU WA HAKI ZA WANAWAKE NA WATOTO PAMOJA NA KUKEMEA UKATILI KWA BINADAMU WOOTE.
 
Back
Top Bottom