Waziri Jafo atamani Halmashauri zijitegemee baada kutembelea mradi wa Government City Complex wa jijini Dodoma

Waziri Jafo atamani Halmashauri zijitegemee baada kutembelea mradi wa Government City Complex wa jijini Dodoma

Elisha Sarikiel

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2020
Posts
905
Reaction score
1,540
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe, Selemani Jafo amesema ndani ya miaka mitatu ijayo matamanio yake ni kuona Halmashauri zinajitegemea zenyewe kupitia mapato ya ndani na kwamba ifike muda ziwe zinalipa watumishi wake mishahara.

“Nikiangalia hoteli kubwa ilivyo kuwa mjini ya ghorofa 11 nikiangalia soko lenu la Dodoma nikiangalia eneo la maegesho ya magari Nala, eneo la mapumziko na michezo Chinangali, Stendi ya Dodoma, ninapata uhakika kwamba halmashauri ya jiji la Dodoma inaenda kujitegemea,”.

Mheshimiwa Waziri Jafo ameonyesha matamanio hayo leo wakati alipotembelea ujenzi wa mradi wa Government City Complex katika eneo la Mji wa Serikali Mtumba unaogharimu kiasi cha shilingi Bilioni 59.3 hadi kukamilika kwake ambapo ametumia nafasi hiyo kulipongeza jiji la Dodoma kwa kutekeleza kwa kutumia mapato yake ya ndani na si fedha za serikali.

Pia alisisitiza “Hakuna halmashauri yoyote iliyofanya uwekezaji mkubwa kama huu hivyo nawapongeza jiji la Dodoma, nataka jengo hili liwe kielelezo na kama nilivyosema mimi matamanio yangu nataka nione halmashauri zinazoweza kujitegeme zenyewe ifike muda halmashauri iseme hata nikiwa na watumishi wangu nitawalipa mimi mwenyewe natamani itokee ndani ya miaka mitatu ijayo,” amesema Waziri Jafo.


1609276981049.png


Pia fahamu miradi ya majengo makubwa inayotekelezwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma; kwa mapato ya ndani kwa kutazama video kupitia Youtube kwa kubofya link >>>



Jiji kuwa na majengo yatakayotoa huduma mbalimbali kama malazi, vyakula, makazi, Ofisi na kumbi za mikutano:-

1. Jengo la hoteli ya kisasa itakayokuwa na ghorofa 11 na vyumba 117 katikati ya jiji ni "Dodoma City Hotel'’.
2. Jengo lenye ghorofa pacha jirani na viwanja vya Nyerere litakalojulikana kama ‘'Nyerere Square Plaza'’.
3. Jengo la ‘Dodoma City Complex’ ni ghorofa nne, eneo la Dodoma Makulu Barabara ya kuelekea Chuo Kikuu cha Dodoma.
4. Mradi wa ‘Nunge Investment’ ni jengo la ghorofa 9, huku likiwa na migahawa mingi ya kisasa ndani yake”.
5. Jengo lingine la ‘Dodoma City Plaza’ katika eneo ambapo kuna ukumbi wa ‘NK’ Jijini humo.
6. Pentagon Tower la ghorofa 10 la kisasa katika jiji la Dodoma;linalotarajiwa kuwa chanzo cha mapato kama miradi mingine.
7. Mradi wa jengo la ‘Government City Complex’ ni kitega uchumi cha jiji la Dodoma uliopo mji wa serikali.

Tufahamu kuwa mji wa Serikali kwa upande wa magharibi unapakana na kambi ya Jeshi ya Ihumwa, Kaskazini-Mashariki unapakana na kata ya Mtumba na upande wa Kusini unapakana na barabara kuu iendayo Dar es salaam.



1609281201297.png

1609281236970.png

 
Ile miradi ya Dar es Salaam Development Cooperation (DDC) iliishia wapi? Walikua na majengo, band ya mziki, kikundi cha ngoma.

Hakuna serikali nyingine iliyowahi kutawala zaidi ya CCM.
 
Nzuguni mbona hawajengi hotels ambapo ndipo kwenye stendi mpya na soko watu kibao au wanataka watu walale kwenye vigodoro na chini na baridi hili huku wakikosa mapato? Jafo angalia hili kwa jicho la 3
 
Huu upuuzi kabisa, shida ya mwanasiasa hasa wa tz, huwa wanasahau kuwa watumishi ndio wanawaweka madarakani.
 
Kwa ukuaji wa jiji la Dodoma kuna upungufu mkubwa wa majengo kupangisha na hasa ofisi katikati ya jiji zenye gharama nafuu.
unajua siku hizi hata frames watu wanazikimbia?mtu alikuwa anauza nguo leo anauzia kwenye gari au nyumbani au wanachukua kaduka uchwara wanachanga,mmoja naweka vi glasses nje mwingine ndania na bidhaa nyingine, time will tell akili yao yote iko kwenye kufanya biashara siyo kufacilitate watu wafanye bishara
ule mpnago wa kujenga petrol stations uliihsia wapi?mana naskia zipo tattu tayari za serikali,ushaona akili ya hawa jamaa?juzi waziri wa burudani anakuambia anataka Netflix ya taifa usije shangaa wakataka iwe ya serikali
Agh mambo ni mengi sana yanashangaza,jengeni tu anyway ..sawa pigeni business
 
Nzuguni mbona hawajengi hotels ambapo ndipo kwenye stendi mpya na soko watu kibao au wanataka watu walale kwenye vigodoro na chini na baridi hili huku wakikosa mapato? Jafo angalia hili kwa jicho la 3
1609306502647.png

Viwanja vilivyopimwa na kuthibitishwa na mamlaka ya jiji la Dodoma kwa makazi salama na biashara; unaweza kuuliza ofisi ya ardhi jiji Dodoma au kampuni kama Infinity Real Estate ziliko Dodoma. Tayari wadau wamenunua viwanja na wanatajiwa kuanza ujenzi na eneo lote hakutakuwa pori mji wa kisasa.
 
View attachment 1662634
Viwanja vilivyopimwa na kuthibitishwa na mamlaka ya jiji la Dodoma kwa makazi salama na biashara; unaweza kuuliza ofisi ya ardhi jiji Dodoma au kampuni kama Infinity Real Estate ziliko Dodoma. Tayari wadau wamenunua viwanja na wanatajiwa kuanza ujenzi na eneo lote hakutakuwa pori mji wa kisasa.
hujaelewa points zangu au hutaki kuzielewa ,sehemu nyingi nchini haya ma frames na ma ofisi ni mapambo tu kwa sasa mazingira ya hizo biashara ni HOVYOOOO kabisa serikali iliyotakiwa kuweka mazingira mazuri ya bishara ndo kwanza inayavuruga inatamani kufanya biashara ,usishangae hata wakafungua na baa zao sasa
 
Mnaua uwekezaji, mnaua biashara, mnategemea hizo halmashauri zenu zitapata wapi mapato?
Tatizo kubwa la Halmashauri nyingi ni baraza la madiwani kukosa watu wabunifu wa vyanzo vya mapato ndani. Je ! wakuu wa idara na Vitengo mbalimbali ambao ni wataalamu washauri wanatekeleza jukumu lao katika Baraza la madiwani; na wanatimiza wajibu kama wataalamu kuwasaidia wakurugenzi katika utekelezezaji wa shughuli mbalimbali katika kila idara na vitengo kwa mafanikio ya halmashauri ? Vema halmashauri nyingine kujifunza kwa jiji la dodoma
 
Halmashauri ya chato,chemba iliyo Dodoma, siha, mwanga, iramba, urambo, kakonko, Hadi yesu arudi hazitakaa zijitegemee. Jaffo unakuwa Kama mahoka kumdanganya mkuu wa nchi. Uliosoma Home economics SUA hukua muongo ,umeharibika lini?
Inaelekea haujamwelewa mhe.Jafo hoja yake kwa halmashauri.
 
Ile miradi ya Dar es Salaam Development Cooperation (DDC) iliishia wapi? Walikua na majengo, band ya mziki, kikundi cha ngoma.

Hakuna serikali nyingine iliyowahi kutawala zaidi ya CCM.


(i) DDC Kariakoo
Mradi huu una ghorofa tatu, vibanda vya maduka, ofisi, migahawa na baa ambavyo vinakodishwa kwa watu na taasisi binafsi kwenye jengo hili ndipo yalipo Makao Makuu ya DDC. Pia Shirika lina mpango wa kujenga jengo la kisasa lisilo pungua ghorofa kumi ili kufanya biashara mbalimbali; ikiwemo vibanda vya maduka, migahawa, benki, kumbi mbalimbali, supermakerts, bureau de change, ofisi n.k. Shirika linakaribisha taasisi binafsi na za umma kuwekeza kwa pamoja katika eneo hili lenye mvuto wa kibiashara zaidi jijini Dare s Salaam na Tanzania.

(ii) DDC Mlimani
Katika mradi huu shughuli kuu ni baa na majiko, vibanda vya biashara na ofisi ambavyo vimekodishwa kwa watu binafsi.
Shirika lina mpango wa kujenga jengo la ghorofa zipatazo kumi kwenye eneo hili lenye mvuto mkubwa wa kibiashara na kihistoria ya burudani mkabala na Mlimani City Barabara ya Chuo Kikuu, Makongo. Kutakuwa na maduka zaidi ya 200, kumbi za burudani kubwa na za kati kwa ajili ya muziki, sherehe na mikutano, ofisi za makampuni na watu binafsi, baa na migahawa na maegesho.

(iii) Perval Garage
Mradi huu ni wa ghorofa moja na bohari mbili ambao upo eneo la banda la ngozi Barabara ya Nyerere. Majengo yote yamepangishwa kwa mpangaji mmoja aitwaye JAMBO FREIGTH anayefanya biashara ya usafirishaji wa mizigo.

(iv) DDC Keko
Mradi huu upo kwenye ukarabati wa kumbi za burudani, kwa sasa vibanda vya biashara na ofisi pekee ndivyo vinafanya kazi.
Hapo baadae Shirika litajenga jengo la ghorofa zaidi ya tano kwa ajili ya bohari, gereji, kumbi za burudani, baa, migahawa, ofisi za makampuni na vyumba vya biashara.

(v) DDC Magomeni
Mradi huu upo sehemu maarufu kwa shughuli za burudani na muziki jijini Dar es Salaam eneo la Magomeni Barabara ya Kondoa kwa sasa mradi upo kwenye uwekezaji na shughuli kuu zinazolengwa ni kumbi za burudani, baa, migahawa, ofisi na vibanda vya biashara.
Shirika lipo katika mchakato wa kujenga jengo la ghorofa tisa (9) lenye matumizi mbalimbali ya vibanda vya biashara, mabenki, ofisi, kumbi za mikutano na sherehe/ burudani. Shirika linakaribisha taasisi binafsi na za umma tuwekeze kwa ubia katikati ya Jiji la Dar es Salaam.

(vi) Shamba la Malolo
Shamba hili lina ukubwa wa hekari 5,000 lipo eneo la Mabwepande Manispaa Kinondoni na Ubungo jijini Dar es Salaam. Shirika limebadilisha matumizi ya shamba hili na kulenga kufanya eneo la viwanda vidogodogo na kutengeneza miji ya kisasa (Satellite Town) na kupima viwanja vya makazi.

(vii) Shamba la Ruvu
Shamba hili lenye ukubwa wa hekari 10000 lipo mkoa wa Pwani kijiji cha Magindu. Mradi huu ni kwa ajili ya kunenepesha mifugo na kutoa huduma kwa wafugaji. Kwenye mradi huu kuna mabwawa makubwa ya kunyweshea mifugo na Shirika limetengeneza majosho ya kuoshea wanyama.

(viii) Uwekezaji DDC Mlimani Mlalakuwa
Shirika lina mpango wa kujenga jengo la ghorofa tano la kitega uchumi cha hosteli. Jengo hili litakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi wapatao elfu tano.
 
Back
Top Bottom