Waziri Jafo umekosea kulazimisha watu wenye taaluma kufanya kazi za propaganda

Waziri Jafo umekosea kulazimisha watu wenye taaluma kufanya kazi za propaganda

Sikutegemea wajitokeze watu wa kutetea alicho fanya waziri. Lakini watu ndivyo tulivyo.
Nilikuwa makini kuona mhandisi kakosea nini, sababu niliyoisikia nilishangaa.

Bora hizo hatua angemchukulia nje ya camera za waandishi. Bila shaka hata wana CCM wengi makini wamesikitika.
 
Members,Siri aliyoitoa Selemani Jaffo huko Arusha inafikirisha sana na kutoa picha halisi ya chama cha mapinduzi

Mosi,Kumbe watu wanakusanywa na kulazimishwa wajitokeze waonekane wengi wakati wa uzinduzi wa miradi na kampeni za ccm
Hili jambo la kukusanya watu wasiojielewa kama mifugo ili waje kupiga makofi uzinduzi wa barabara ya lami halina afya hata kidogo kwa mustakabali wa Taifa
Leo hii watu wengi wanafahamu ni kazi ya serikali kuweka lami na kujenga miundombinu ,hili sio ombi ni lazima kwa kuwa wanatuumiza kwenye kodi
Jambo baya zaidi unalazimisha watumishi wenye taaluma zao wakakusanye watu ili waje kukushangilia wewe na barabara ya lami

Pili,Watendaji wenye taaluma zao mfano engineers,Waganga wakuu wa hospital za wilaya na afya na wengine wanalazimishwa kujiingiza kwenye siasa kwa nguvu ili kusifu na kupiga makofi,Nini kosa la yule mtendaji wa serikali
Je?Yule mtendaji anayelazimishwa kukusanya watu Arusha na Selemani Jaffo alipewa pesa za mafuta na vipaza sauti ili ashawishi wananchi kuja kushangilia barabara ya lami

Kwa hili Jaffo kubali umekosea na omba msamaha watu watakusamehe,Kubali umeteleza

Yule mtumishi anayesimamia barabara Arusha hukutaka kumsikiliza uliona hoja zake zina mashiko ,Ulikuwa na hasira na frustration zako na mihemko isiyokuwa na maana kama Waziri

Selemani Jaffo ukiwa na hasira jaribu kunywa maji mengi na kutulia kwanza ,Ulevi wa madaraka ulioonyesha kwa mtumishi Arusha mwenye taaluma yake kumlazimisha akaswage watu kama mifugo halikubariki kabisa

Propaganda fanyeni nyie wana siasa,ccm Arusha ilikuwa wapi kukusanya hao watu waje kukushangilia wewe na barabara ya lami

Je Arusha hakuna katibu wa chama cha mapinduzi au Mwenyekiti wa ccm Arusha

Umetumia madaraka yako vibaya sana ,Watu walikuamini lakini sasa wanapata picha yako halisi kuwa wewe ni katili ,mpenda sifa na usiyetaka kusikiliza hoja za watumishi wa uma

Yule mtumishi aliyesimamia barabara Arusha kama engineer ulipasa kumsifu na kumpa hongera yake,Kitendo cha kumlazimisha engineer akatafute watu waje kukupigia makofi wewe na barabara ya lami ni aibu kubwa,Hata bosi wako hawezi kukubaliana na ulichokifanya Arusha kumuondoa mtumishi wa uma kisa hajatafuta watu wa kukupigia makofi wewe na kupigia makofi barabara ya lami
Jafo mwanza nilikuwa namkubali sana toka uchaguzi wa serikali za mitaa nikaona ni hopeless kabisa
 
Sikutegemea wajitokeze watu wa kutetea alicho fanya waziri. Lakini watu ndivyo tulivyo.
Nilikuwa makini kuona mhandisi kakosea nini, sababu niliyoisikia nilishangaa.

Bora hizo hatua angemchukulia nje ya camera za waandishi. Bila shaka hata wana CCM wengi makini wamesikitika.
CCM ya zamani ungeona anajitokeza hata kiongozi chamani akipinga ule uonevu. Shida ni CCM ya sasa, wao kazi yao ni kuunga mkono udhalimu wowote ule. Watapinga pale mwenyekiti akijitokeza kupinga tu.
Very pathetic
 
Kuna kipengele kinasema utafanya na kazi ingine ambayo utapangiwa na mwajiri wako,hicho kipo mpaka China utakikuta
Waliokitunga si wajinga,ndio maana wengine tumeamua kujiajiri tu
Alipangiwa kazi iyo na mwajiri wake?? Fichaga upumbavu wako ndugu
 
Alipangiwa kazi iyo na mwajiri wake?? Fichaga upumbavu wako ndugu
Mwisho wa siku ni weww na huyo jamaa yako mtaonekana wapumbavu kwa kung'ania kazi isioendana na taaluma
Kumshambulia Jaffo hakuwasaidii,mwambie jamaa yako aache kazi
 
1594356482685.png
Watu hujionyesha peupe wako vipi kwa matendo yao.

Aidha kumfurahisha bila aibu yule aliye mteua, hawa ndio boot lickers, au kufanya kazi kwa maadili yenye kuonyesha dhamana ya uongozi.

Jafo kapewa wizara ambayo vyatu ni vikubwa kwake.

Hatujasahau singeli aliyotoa na ku-rap mpaka mkandarasi SKOL akazimia kule Dodoma.

Leo kazi imefanyika kule Arusha sasa anataka kazi ikimalizika watu wa kusifu na kuabudu waitwe kumsifu hadharani.

Jafo hafai. Jafo kijana mdogo mwenye wake wanne nasikia, yeye weledi wa kazi hakuna, anaona sifa ni kumpa aliye mteua.

Wananchi wa Kisarawe tupeni mtu mwingine, huyu Jafo heri achukue nafasi ya Polepole kwenye chama.

Msimchague Jafo, mtu ambaye anaona heri punda afe, mzigo wa sifa za bwana zifike.
 
Ndio Tanzania hii.
Nakumbuka nikiwa form five Lindi secondary school, alikuja waziri mkuu Mizengo Pinda mkoa wa Lindi kwenye ghafla fulani. Headmaster alitupa Uhuru wa kwenda mjini viwanjani bila kuandika kwenye daftari la departure. Pia akatuambia tusivae uniform ilhali pale shule nguo za nyumbani ni marufuku hata kuzihifadhi kwenye tranka au begi.
Bwana weee tulitupia na kufurahi sana ile siku kumbe ilikuwa ni issue ya propaganda ya kumpamba waziri mkuu aone Lindi tunaipenda serikali .
CCM hii tabia ya kuzoa wanafunzi na watumishi kwenye ghafla hawajaanza leo
 
Mtanisamehe, ngoja nilisema kama mnatukana tukana! Nipige madongo yoyte mnataka. Mzaramo kazi anayoijua ni kucheza mdundiko. Sishangai Jafo kufanya ushenzi kama huu! sishangai katu! mtu ambaye hana mdundiko kichwani hawezi kum- victimise mwanadamu mwenzake kama alivyofanya kwa kijana wa TARURA! Shetani amlaani jafo!
 
Back
Top Bottom