Waziri Jafo umekosea kulazimisha watu wenye taaluma kufanya kazi za propaganda

Waziri Jafo umekosea kulazimisha watu wenye taaluma kufanya kazi za propaganda

Watu hujionyesha peupe wako vipi kwa matendo yao.

Aidha kumfurahisha bila aibu yule aliye mteua, hawa ndio boot lickers, au kufanya kazi kwa maadili yenye kuonyesha dhamana ya uongozi.

Jafo kapewa wizara ambayo vyatu ni vikubwa kwake.

Hatujasahau singeli aliyotoa na ku-rap mpaka mkandarasi SKOL akazimia kule Dodoma.

Leo kazi imefanyika kule Arusha sasa anataka kazi ikimalizika watu wa kusifu na kuabudu waitwe kumsifu hadharani.

Jafo hafai. Jafo kijana mdogo mwenye wake wanne nasikia, yeye weledi wa kazi hakuna, anaona sifa ni kumpa aliye mteua.

Wananchi wa Kisarawe tupeni mtu mwingine, huyu Jafo heri achukue nafasi ya Polepole kwenye chama.

Msimchague Jafo, mtu ambaye anaona heri punda afe, mzigo wa sifa za bwana zifike.
Hawa wanachaguliwa na tume ya uchaguzi na siyo wananchi
 
Huyu dogo nimemdharau Sana Kuna TISS mmoja aliniambiaga ni mmojawapo wa watu wanaofatiliwa au anaandaliwa kuteuliwa uraisi. Baadae yeye na lukuvi wako kwenye kapu moja wanapikwa lkn kwa tukio la Jana nimemdharau kabisa
Jafo ni dogo mtu alizaliwa 1973? basi sisi ni wachanga
 
Kuna kipengele kinasema utafanya na kazi ingine ambayo utapangiwa na mwajiri wako,hicho kipo mpaka China utakikuta
Waliokitunga si wajinga,ndio maana wengine tumeamua kujiajiri tu
Mkuu acha kujitoa ufahamu basi.
 
Viongozi wa Taifa hili ni hovyoooh tyuuh, hasa kutoka chama cha [emoji1637]
 
Sikutegemea wajitokeze watu wa kutetea alicho fanya waziri. Lakini watu ndivyo tulivyo.
Nilikuwa makini kuona mhandisi kakosea nini, sababu niliyoisikia nilishangaa.

Bora hizo hatua angemchukulia nje ya camera za waandishi. Bila shaka hata wana CCM wengi makini wamesikitika.
Nikiwa kada mkongwe nimesikitishwa sana na college mate wangu Jafo
 
Unajua hata mimi nilishangaa sana Waziri anamlaumu Mhandisi wa TARURA kuwa hajatimiza wajibu kuwaleta au kuwaalika wananchi washuhudie Uwekezaji Mkubwa wa Serikali Arusha. Sasa sijui Mhandisi ndiyo amekuwa Afisa Habari wa Arusha na viunga vyake. Yaani kwa maelezo yake anafikiri Mhandisi ni Mpinzani wa Juhudi za Serikali, wakati Mwamba ametimiza majukumu yake vizuri tuu.

Halafu anasema kabisa huyu hawezi kuongoza Jiji kama la Arusha mpelekeni Buhigwe au Kakonko huko(Kwa maana nyingine kumbe ukiwa huko Kakonko na Buhigwe ni kama ADHABU umepewa). Waziri anashindwa kujua kuwa watu ni waelewa juu ya Maendeleo na haihitaji kutumia nguvu kuuubwa kuyanadi.
 
Ndio maana mwana taaluma ukiomba kazi kwenye usaili watataka kuona how flexible you are! Hao kina Pompeo ni mabobezi kwenye taaluma zao,lakin inabidi waende sambamba na Trump.

Kama unaona huwezi fuata maelekezo ya mkubwa wa kazi, acha tu kazi. Tarura kazi kubwa ni kusimamia barabara za wilaya ambazo zinawagusa wananchi wapiga kura.

Kwa kipindi hiki cha uchaguzi. Hakuna serikali ilio tayari kuwakosa wapiga kura,kwenye eneo gumu kama Arusha,kisa tu wewe ni mwana taaluma.

kunywa maji alafu relax, alafu soma tena ulichoandika, then tafakari kwa makini, tumia medula sio tumbo mkuu utaelewa kuwa umekosea sana...ovaa
 
Mh. Jafo sio tu kachukua maamuzi ya ovyo na ya uonevu. Pia hajalitendea haki hili neno ' sabotage'
Nilimshangaa sn alipomuuliza "Wewe ni mpinzani? Unataka wananchi waseme Raisi hajafanya kitu huku Arusha? n.k". Ni aibu kubwa kulazimisha mioyo ya watu kufanya jambo wasilolipangilia. Kazi inaonekana hakuna haja ya kuforce watu kuimba mapambio. Waache kujitafutia riziki wakasimame barabarani? Aliwaandalia ujira? Jafo kajishusha kwa speed ya kutisha.
 
How far are you willing to kutetea madhaifu ya viongozi wa serikali? Inasikitisha kuona tuna wananch Aina yako!

Yan kuna mtu akiabdika kitu kumkadiria level ya elimu yake ni rahis sana aisee hivi mtu kweli anaona sawa yani ukiwa mtumish wa serikali ni mtumish wa CCM?
 
NI Ujinga Sana; Kama umefanya Kazi imeonekana inakuwaje Mpaka watu wawepo kwenye uzinduzi? Kama kazi imefanyika what i know ni kwamba Output inaongea; Huitaji Kutumia Nguvu Kubwa sana kuwaaminisha watu.

Suala kama Barabara inaonekana, hata watu wasipokuja watapita na wataifurahia tu; pasi na wao kuwepo kwenye uzinduzi. Sasa kweli Mtu aache shughuli za uzalishajai mali aende kwenye uzinduzi? Yeye Jffo ilikuwa ni sehemu yake ya Kazi, lakini wananchi wana kazi za uzalishaji mali mahalai pengine.

Duuh, nawaza hata kutokurudi mwaka huu; Maana Nchi yangu imekuwa na mambo ya Ajabu kweli kwenye Uongozi.
 
Ndio maana mwana taaluma ukiomba kazi kwenye usaili watataka kuona how flexible you are! Hao kina Pompeo ni mabobezi kwenye taaluma zao,lakin inabidi waende sambamba na Trump.

Kama unaona huwezi fuata maelekezo ya mkubwa wa kazi, acha tu kazi. Tarura kazi kubwa ni kusimamia barabara za wilaya ambazo zinawagusa wananchi wapiga kura.

Kwa kipindi hiki cha uchaguzi. Hakuna serikali ilio tayari kuwakosa wapiga kura,kwenye eneo gumu kama Arusha,kisa tu wewe ni mwana taaluma.
Kwani huo ulikuwa mkutano wa ccm!? Mwishoni mtawalazimisha wasomi kwenye vitengo wawe wanaanza na salamu ya "ccm hoyee" kwenye mikutano au hafla za uzinduzi wa miradi. Kama namuona vile Daktari wa Mkoa akiwasalimia wananchi kwa "ccm hoyee" kwenye uzinduzi wa wodi mpya.
 
Huyu jamaa sijawahi kuona utendaji wake zaidi ya maneno ya vitisho na kufokafoka , the way he talks unagudua tu anaigiza
 
Alitakiwa amkomalie Diwani wa Kata husika wala siyo Meneja wa TARURA hata kidogo.
Unaweza kukuta diwani alifanya kazi yake lakini alipoenda kwa meneja was TARURA kuhitaji fedha za kuandaa ubwabwa kwa wananchi (I mean wanaccm maana hao ni ubwabwa tuu) meneja akamtolea nje.
Ndio chanzo cha mgogoro
 
Members,

Siri aliyoitoa Selemani Jafo huko Arusha inafikirisha sana na kutoa picha halisi ya Chama cha Mapinduzi.

Mosi, kumbe watu wanakusanywa na kulazimishwa wajitokeze waonekane wengi wakati wa uzinduzi wa miradi na kampeni za CCM.

Hili jambo la kukusanya watu wasiojielewa kama mifugo ili waje kupiga makofi uzinduzi wa barabara ya lami halina afya hata kidogo kwa mustakabali wa taifa.

Leo hii watu wengi wanafahamu ni kazi ya serikali kuweka lami na kujenga miundombinu, hili sio ombi ni lazima kwa kuwa wanatuumiza kwenye kodi.

Jambo baya zaidi unalazimisha watumishi wenye taaluma zao wakakusanye watu ili waje kukushangilia wewe na barabara ya lami

Pili, watendaji wenye taaluma zao mfano engineers, waganga wakuu wa hospital za wilaya na afya na wengine wanalazimishwa kujiingiza kwenye siasa kwa nguvu ili kusifu na kupiga makofi. Nini kosa la yule mtendaji wa serikali?

Je, yule mtendaji anayelazimishwa kukusanya watu Arusha na Selemani Jafo alipewa pesa za mafuta na vipaza sauti ili ashawishi wananchi kuja kushangilia barabara ya lami.

Kwa hili Jafo kubali umekosea na omba msamaha watu watakusamehe, kubali umeteleza.

Yule mtumishi anayesimamia barabara Arusha hukutaka kumsikiliza uliona hoja zake zina mashiko. Ulikuwa na hasira na frustration zako na mihemko isiyokuwa na maana kama Waziri.

Selemani Jafo ukiwa na hasira jaribu kunywa maji mengi na kutulia kwanza. Ulevi wa madaraka ulioonyesha kwa mtumishi Arusha mwenye taaluma yake kumlazimisha akaswage watu kama mifugo halikubariki kabisa.

Propaganda fanyeni nyie wanasiasa. CCM Arusha ilikuwa wapi kukusanya hao watu waje kukushangilia wewe na barabara ya lami.

Je, Arusha hakuna katibu wa chama cha mapinduzi au Mwenyekiti wa CCM Arusha.

Umetumia madaraka yako vibaya sana. Watu walikuamini lakini sasa wanapata picha yako halisi kuwa wewe ni katili, mpenda sifa na usiyetaka kusikiliza hoja za watumishi wa umma.

Yule mtumishi aliyesimamia barabara Arusha kama engineer ulipasa kumsifu na kumpa hongera yake. Kitendo cha kumlazimisha engineer akatafute watu waje kukupigia makofi wewe na barabara ya lami ni aibu kubwa. Hata bosi wako hawezi kukubaliana na ulichokifanya Arusha kumuondoa mtumishi wa uma kisa hajatafuta watu wa kukupigia makofi wewe na kupigia makofi barabara ya lami.
Viongozi wamepagawa ni mwendo wa sifà vifijo na nderemo ili wasitumbuliwe
 
Back
Top Bottom