Waziri Jenister Mhagama: Tumebaini Uwepo wa Cake, Juisi na Biskuti Zenye Bangi

Waziri Jenister Mhagama: Tumebaini Uwepo wa Cake, Juisi na Biskuti Zenye Bangi

Watumiaji wa bangi nchini Tanzania wameibuka na mbinu mpya ya kuchanganya kilevi hicho na vyakula mbalimbali kama vile majani ya chai, keki, biskuti, juisi pamoja na asali.

Kutokana na hilo serikali kupitia kwa Waziri wa nchi ofisi ya Waziri mkuu Jenista Mhagama akiwasilisha taarifa ya hali ya dawa za kulevya kwa mwaka 2022, amesema serikali imeanza operesheni nchi nzima kwenye viwanda vinavyozalisha biskuti na bidhaa nyingine za vyakula.

"Kuna dada Arusha yeye na mume wake raia wa kigeni tulikuta wanatengeneza bidhaa zikiwemo biskuti, keki na asali zote zikiwa zimewekwa bangi kwa asilimia kubwa na zikiwa zimeshafungwa kwaajili ya kusafirishwa kwenda nje ya nchi" ameongeza Waziri Jenista.

View attachment 2640961View attachment 2640962View attachment 2640964
Mbona hamkutoa taarifa.
 
Mkuu, kwa maslahi mapana ya umma itakuwa vizuri ukaiweka wazi hiyo kampuni na hicho kinywaji ili kuokoa wengi. Tunamshukuru Mungu serikali imeshtukia vinywaji vya energy drinks na kuvipiga marufuku baada ya uchunguzi wa TFMDA.

Wakati umefika serikali iweke mkazo kupima kiasi cha kilevi au bangi kilichomo kwenye vyakula vya viwandani ili kuliokoa taifa kutumbukia kwenye ulevi na uraibu.
Ni kampuni kubwa tu mkuu watu wengi wanaipenda sana
 
Bangi hizo za kwenye biskuti na asali haziendi kuliwa au kuvutwa, zinakwenda kwenye viwanda vya madawa ya Binadam yenye "extracts" za bangi.

Bangi iruhusiwe tu iwe inalimwa kwa uhuru na isafirishwe kihalali, ina faida kubwa sana kuliko madhara.

Sigara na pombe zina madhara zaidi ya bangi.
Hata hizo soda na juisi ambazo vijana wetu wanapenda kunywa zina madhara makubwa zaidi ya bangi. Ni afadhali kunywa gongo kuliko kunywa vinywaji hvi. Vina madhara makubwa sana mwilini.
 
Ni kampuni kubwa tu mkuu watu wengi wanaipenda sana
Basi kama ni hiyo inajulikana, hakuna haja ya kuitaja. Wanajifanya waislamu safi kumbe wauaji wakubwa! Serikali inapaswa kuwachukulia hatua wapuuzi hawa.
 
Watu wanachangia bila hata kujiridhisha. Je bangi inalewesha Kwa kuliwa au kunywa au kuvuta. Siyo Kila habari ni ya kuaamini
Wewe unadhani waziri amekurupuka kutoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu uwepo wa bangi kwenye vyakula tajwa? Haya, wewe tuambie unachofahmu kuhusiana na sakata hili.
 
Ni hatari. Wengi watakuwa wamekula bila kujua. Mimi situmii vitu hivyo miaka mingi sana
Wewe unadhani wenye viwanda wataongeza gharama na risk ya kukamatwa kwa kuweka bangi kwenye kila biskuti? Ili iwasaidie nini sasa? Hapa huyu waziri hakuelezea yote na ameacha hivyo makusudi ili aonekane amefanya kazi kubwa ya kuokoa taifa isiangamie. Wanaoweka bangi watakuwa vi wenye viwanda wenye order special na bila shaka hata biskuti zake zitakuwa na bei na faida zaidi.
 
Mkuu itabidi niache......vingine vyote vilivyotajwa hapo situmii ila hapo kwenye keki ndo waliponikea bangi! Binadamu tuna tamaa za ajabu. Kisa pesa tunawekeana bangi kwenye vyakula
Lengo lao ni kukufanya uwe teja ili uwe unanunua kila siku. Ni mbinu mojawapo ya kupanua soko la bidhaa.
 
Bangi hizo za kwenye biskuti na asali haziendi kuliwa au kuvutwa, zinakwenda kwenye viwanda vya madawa ya Binadam yenye "extracts" za bangi.

Bangi iruhusiwe tu iwe inalimwa kwa uhuru na isafirishwe kihalali, ina faida kubwa sana kuliko madhara.

Sigara na pombe zina madhara zaidi ya bangi.
Upewe maua yako
 
Kuna soda kampuni fulani nilizoea kunywa ilikuwa ikifika muda ninaokunywaga nguvu mwilini zinaisha/kama sijala kwa siku mbili
Baada ya hali hiyo niliamua kupunguza mpaka sasa hali hiyo haipo.
Nadhani hata kwenye soda hasa zenye gesi hayo madawa yapo. Hii dunia ni ngumu sana
Mmh kwamba bangi ni depressant drug kwamba inakufanya unanyongea na kukosa nguvu?really???
 
Kwa mujibu wa Gazeti la Nipashe la leo 31/5/2023, imedhahadharishwa kwa walaji wa vyakula tajwa kupunguza ulaji wake kwani imebainika bidhaa hizo zinatiwa bangi ndani yake. Lengo hasa la watengenezaji bidhaa hizi kutia bangi ndani yake ni kuwajengea wateja uraibu ili kuongeza mauzo kwa kuwa wateja wakishakuwa waraibu watakuwa wana hamu ya kununua kila siku. Ikipita siku mtu hajala keki, biskuti chocolate au majani ya chai atakuwa anajisikia kuwa na uraibu mkubwa hadi atakapoipata bidhaa husika.

MAONI YANGU
Naishauri serikali ichukue tahadhari kukomesha vitendo hivi kwa kuwa wanunuzi wakubwa wa bidhaa zinamowekwa bangi ni watoto wadogo. Tusipokuwa makini tutakuwa tunakuza kizazi cha mateja. Miaka michache ijayo taifa litakuwa limejaa waraibu kila kona.

Niliwahi kupata tetesi kuwa akina mamalishe wanaouza maandazi, chapati, kacholi na mihogo kwenye maeneo ya shule za msingi nao hutia dawa za kulevya kwenye vyakula ili kuwajengea wanafunzi uraibu. Ikiwa tutaenda namna hii bila kuchukua hatua za kukomesha vitendo hivi viouvu taifa lijalo litakuwa la walevi, mateja na waraibu. Tunapaswa kuziba ufa kabla ya kujenga ukuta.

Chanzo: Wasafi FM kipindi cha mapitio ya magazeti.

Nawasilisha.
wamesikia wapi kuwa bangi ina uraibu,waache kupotosha watu
 
Bangi hizo za kwenye biskuti na asali haziendi kuliwa au kuvutwa, zinakwenda kwenye viwanda vya madawa ya Binadam yenye "extracts" za bangi.

Bangi iruhusiwe tu iwe inalimwa kwa uhuru na isafirishwe kihalali, ina faida kubwa sana kuliko madhara.

Sigara na pombe zina madhara zaidi ya bangi.
Kibibi, leo umenikosha sana. Ungekua karibu ningekupa mabusu kadhaa!
 
Wauza mayai na karanga barabarani wawekwe mstari wa mbele kabisa pamoja na energy drinnk
 
Eti jamani! Kila siku inasemwa halafu hakuna muafaka unaofikiwa nini kifanyike kuihusu nayo haikomi ipo tu
Muafaka ni wewe mwenyewe uache kutumia hizo bidhaa ili kuepuka kujiingiza kwenye ulevi na uraibu. Kama ilivyo kwenye sigara, watengenezaji wanakuambia kabisa UVUTAJI WA SIGARA NI HATARI KWA AFYA YAKO. Ni juu yako kuamua kuacha kuvuta au uvute at your own risk bila kumlaumu mtu yeyote kwa kuwa umepewa tahadhari mapema.
 
Muafaka ni wewe mwenyewe uache kutumia hizo bidhaa ili kuepuka kujiingiza kwenye ulevi na uraibu. Kama ilivyo kwenye sigara, watengenezaji wanakuambia kabisa UVUTAJI WA SIGARA NI HATARI KWA AFYA YAKO. Ni juu yako kuamua kuacha kuvuta au uvute at your own risk bila kumlaumu mtu yeyote kwa kuwa umepewa tahadhari mapema.
Sigara ina nicotine ambayo ndio inaleta uraibu,bangi haina uraibu jamani mjielimishe maana ya uraibu
 
Bangi ilifaa ichanganywe na vitu vichachu vichachu na siyo vitamu kama biskuti na asali.
[emoji16]
 
Back
Top Bottom