Waziri Kamwelwe atangaza mkakati wa kupambana na ugonjwa wa Coronavirus kwenye vyombo vya usafiri

Waziri Kamwelwe atangaza mkakati wa kupambana na ugonjwa wa Coronavirus kwenye vyombo vya usafiri

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi a mawasiliano ameitaka mamlaka ya udhibiti usafiri wa ardhini ( Latra) kukutana mara moja na kutoa mwongozo juu ya idadi ya abiria wanaoruhusiwa kusimama ndani ya daladala na Mwendo kasi ili kupunguza msongamano.

Waziri Kamwele ameyasema hayo mjini Dodoma alipokuwa anaelezea hatua zinazochukuliwa na wizara yake ili kujikinga na virusi vya korona.

Chanzo: ITV habari
-----

March 18, 2020

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mh.Eng. Isack Kamwelwe atoa tamko kufuatia Coronavirus Covid-19.

Tamko hilo la Waziri Isack Kamwelwe linahusu sekta ya usafiri wa barabara, reli, anga na majini linataka wenye vyombo vya usafiri na watumiaji kuchukua tahadhari kubwa kufuatia ugonjwa huo kufuatia tangazo la Wizara ya Afya kuthibitisha ugonjwa huo upo Tanzania.



  1. Kampuni za usafiri wafungue vituo zaidi vya kukatia tiketi nje ya vituo vikuu vya usafiri.
  2. Tiketi za kieletroniki ziamzishwe kupunguza msongamano.
  3. Wafanyakazi na abiri watumie sanitizier mara kwa mara kusafisha viganja vyao washikapo nauli, chenji, kushika viti n.k
  4. LATRA, TBS, na wizara ndani ya siku tatu waamue ni idadi gani ya abiria wawemo katika chombo cha usafiri ili kupunguza uwezekano wa maambukizi.
  5. TAZARA na TRC wahakikishe vifaa vya kusafisha mikono viwepo stesheni na katika treni.
  6. Mamlaka za usimamizi wa bandari na zile za viwanja vya ndege kwahakikishe kuwapo na vifaa vya kusafisha mikono n.k katika maeneo yao.
  7. Taasisi zote za usafiri zishirikiane na wizara ya Afya ili kuweza kuchapisha na kubandika matangazo yenye habari sahihi juu ya namna ya kuwa safi na pia kuzuia kusambaa ugonjwa wa Covid19 Coronavirus.

Source: Global TV online

Mh Waziri achana na siasa. Magari yote ya kusafirisha abiria idadi ya abiria inajulikana na pale wanaporuhusiwa kusimamisha pia idadi inajulikana. Latra hawahitaji kuitamka kwa sababu tayari iko katika ruhusa yao ya biashara. Kinachotakiwa Mh Waziri ni kutekeleza, kitu ambacho kimetushinda wakati wote. Nchi zinazotuzunguka abiria katika daladala zao ni level seating.
 
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi a mawasiliano ameitaka mamlaka ya udhibiti usafiri wa ardhini ( Latra) kukutana mara moja na kutoa mwongozo juu ya idadi ya abiria wanaoruhusiwa kusimama ndani ya daladala na Mwendo kasi ili kupunguza msongamano.

Waziri Kamwele ameyasema hayo mjini Dodoma alipokuwa anaelezea hatua zinazochukuliwa na wizara yake ili kujikinga na virusi vya korona.

Chanzo: ITV habari
-----

March 18, 2020

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mh.Eng. Isack Kamwelwe atoa tamko kufuatia Coronavirus Covid-19.

Tamko hilo la Waziri Isack Kamwelwe linahusu sekta ya usafiri wa barabara, reli, anga na majini linataka wenye vyombo vya usafiri na watumiaji kuchukua tahadhari kubwa kufuatia ugonjwa huo kufuatia tangazo la Wizara ya Afya kuthibitisha ugonjwa huo upo Tanzania.



  1. Kampuni za usafiri wafungue vituo zaidi vya kukatia tiketi nje ya vituo vikuu vya usafiri.
  2. Tiketi za kieletroniki ziamzishwe kupunguza msongamano.
  3. Wafanyakazi na abiri watumie sanitizier mara kwa mara kusafisha viganja vyao washikapo nauli, chenji, kushika viti n.k
  4. LATRA, TBS, na wizara ndani ya siku tatu waamue ni idadi gani ya abiria wawemo katika chombo cha usafiri ili kupunguza uwezekano wa maambukizi.
  5. TAZARA na TRC wahakikishe vifaa vya kusafisha mikono viwepo stesheni na katika treni.
  6. Mamlaka za usimamizi wa bandari na zile za viwanja vya ndege kwahakikishe kuwapo na vifaa vya kusafisha mikono n.k katika maeneo yao.
  7. Taasisi zote za usafiri zishirikiane na wizara ya Afya ili kuweza kuchapisha na kubandika matangazo yenye habari sahihi juu ya namna ya kuwa safi na pia kuzuia kusambaa ugonjwa wa Covid19 Coronavirus.

Source: Global TV online
Huyu bado hajatumbuliwa tu jamani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo waziri hajawai kuwa serious vikao vya nn tena wakati hapo ni ishu ya kutoa maagizo ya level seat !!

Waziri wa Kazi naye ajaribu kuongea na waajiri watoe likizo ya mwezi kwa baadhi ya wafanyakazi ili kupunguza mrundikano maeneo ya kazi na public transport mfano mzuri Google na Facebook wamepunguza wafanyakazi kwa kuwapa likizo na baadhi ya kazi zinfanywa majumbani sio maofisini.
Mkuu unapotoa mifano,au kulinganisha vitu uwe unatafakari kwanza!
 
Mamlaka ya Kudhibiti usafiri wa ardhini nchini (Latra) imetoa maelekezo kwa wamiliki wa mabasi ya abiria kuhakikisha abiria wote wanakaa yaani "level seat"

Source: Mwananchi
 
Bro!! johnthebaptist Hilo agizo umeolionaje? Hawa viongozi wenu wa Lumumba Wana akili za kuvukia barabara tu
Bwashee level seat ni kwa mujibu wa sheria na imeelezwa bayana kwenye kadi ya gari idadi ya abiria.

Hata kwenye mlango wa dereva huandikwa idadi ya abiria wanaoruhusiwa kisheria.

Maendeleo hayana vyama!
 
Wakitaka ivyo walete mabasi yao hao Latra,lakini kwa hawa wenye daladala biashara kwao itakuwa ngumu sana,Sipati picha iyo asubuhi ama jioni kwa gari za Mbagara ama Gongo la Mboto wataweza iyo level seat
Nimekuelewa sana!
 
Sidhani kama ili linahusiana na Corona maana sheria ipo ila utekelezaji wake ndio ulikuwa hafifu. Bado serkali haijajua namna ya kuwakinga watu na corona au wanafanya kusudi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom