Waziri Kijaji: Tanzania ina viwanda 13 vya kuunganisha Magari

Waziri Kijaji: Tanzania ina viwanda 13 vya kuunganisha Magari

Kasema viwanda:

1.Juzi Raisi Dr Mama Yetu SSH kafungua assembly plant kubwa ya dump truck mkoa wa pwani yenye uwezo wa kuunganisha maroli hayo kwa dakika 45.

2.Carmatec ipo Arusha inaunganisha na kuunda matrector ya bei nafuu,mradi wa wizara za viwanda na kilimo.

3.Kibaha kuna assembly plant ya matracor makubwa kutoka Ulaya.

4.Yapo makampuni tena ya miaka mingi yanatengeneza semitraler za malori,kampuni zaidi ya tatu.

5.Battery za magari Yuasa Battery.

6.Ongezea.
Mimi natengeneza body za trailer na mabasi,pia mashine za kilimo kama maize huller,vinu vya kusaga na kukoboa nafaka,pre fab godowns nk, ila sina hakika kama mimi ni kiwanda, nadhani bado nime miss some standard ili niitwe kiwanda, safari hatua,labda kweli tuna viwanda vya magari,sema hatuvioni popote.
 
kabla ya kuongea fanya utafiti, elewa muktadha wa kauli husika, sadly unajikuta una akili sana halafu kuna vitu vidogo vidogo kama hivi vya elimu ya sekondari unashindwa kung'amua mwisho wa siku unakuja kuthibitisha the way fanatic christians are very poor in thinking critically.

Tatizo ni kuwa unachuki na wasiokuchukia, watu waliobize kwenye maisha yao we unataka kuanzisha chokochoko za kijinga.

Kwani hakuna kiongozi wa kikristo aliyewahi kuongea kwa malengo ya kisiasa zaidi??? Jibu ni kwamba wapo wengi zaidi kuliko hata viongozi wa waislamulamu kama umesahau kuna mwamba mmoja alishawahi kumuita mkuu kwa nomino Mungu nanukuu maneno yake kwa uchache "Mheshimiwa Mungu" na alikuwa mkristo lakini waislamu hawakureply kwa namna ambayo wengi wenu mna fanya.

Tuombe kwa Mungu amani itawale ila nyi jamaa ni watu mliokosa ustaarabu na mpo nje ya mafundisho ya biblia.

Acheni ujinga
Sasa kuna shida gani kama mtu ameamua kuwa na mungu wake ambae wewe humwamini? Muache amwabudu mungu wake,na wewe muabudu unaye mwabudu, case closed.
 
Mh! tukisema mnasema tunatukana. huyu atakuwa madrasa graduate1 au natukana jamani?
Ungetoa sababu za kusema hivyo, ingetusaidia na sisi tusiomjuwa. Lakini ulivyo acha hivyo hivyo ilivyokaa, wengi watakuona wewe kuwa na tatizo lileeee.....! La udini. Jambo ambalo si jema hata kidogo kwa nchi yetu.

Labda niulize tu swali, huyo mama ana 'doctorate' ya mambo gani hasa; yaani taaluma yake ni katika mambo gani?
 
Tiorodhesheeni viwanda hivyo kwa majina,na pia kazi zinazofanywa na viwanda hivyo ili tusio na ajira tujue wapi pakuomba ajira katika viwanda hivyo.
Tambua kuwa trailer pia ni gari, viwanda vya kutengeneza Matrailer ndo vipo vingi,mfano super doll,simba trailer n.k,
 
Magari aina gani? Mbona hayaingii sokoni? Au ni haya ya kuchezea watoto??
 
Taarifa hii iwafikie wabishi wote popote walipo, kwamba, ndani ya Tanzania kuna viwanda vya magari 13

Waziri wa Viwanda Dkt Kijaji amethibitisha
---

Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Ashatu Kijaji amesema kuwa Tanzania ina jumla ya viwanda 13 vya magari, kati ya viwanda hivyo, viwanda viwili (2) vinaunganisha magari ambavyo ni GF Trucks and Equipment Ltd kilichopo Kibaha, Pwani na Saturn Corporation Limited kilichopo Kigamboni, Dar es Salaam.

Dkt. Ashatu ameyasema hayo Leo Mei 21, 2024 Jijini Dodoma wakati akiwasilisha Hoja ya Bajeti ya Makadirio ya mapato na matumizi ya mwaka wa fedha 2024/2025 ya Wizara ya Viwanda na Biashara.

Dkt. Ashatu amesema kuwa Viwanda 11 vilivyosalia vinatengeneza matrela huku Kiwanda cha GF Vehicle Assemblers(GFA) sio GF Trucks & Equipment kina uwezo uliosimikwa wa kuunganisha magari 200 kwa mwezi na kimewekeza kiasi cha shilingi bilioni 10.752 na
kimetoa ajira 300.

Aidha Waziri huyo amefafanua kuwa . Ashatu Mradi wa Kiwanda cha Saturn Corporation Limited umegharimu mtaji wa kiasi cha shilingi bilioni 64.3 na kina uwezo uliosimikwa wa kuunganisha vichwa vya magari 900 na tipa 270 kwa mwezi huku kiwanda kikiajiri wafanyakazi 250.

PIA SOMA
- Waziri Kijaji: Tanzania ina viwanda vya chuma 28 vyatoa ajira 25,358 kwa Watanzania
Punguani wa Chadema lazima wabishe 😆😆😆😆

Na wakati wakibosha hawana hata takwimu,ni looser sana nyie watu nimewaona huko Twitter mnatokwa mapovu 😁😁😁😁
 
Mimi natengeneza body za trailer na mabasi,pia mashine za kilimo kama maize huller,vinu vya kusaga na kukoboa nafaka,pre fab godowns nk, ila sina hakika kama mimi ni kiwanda, nadhani bado nime miss some standard ili niitwe kiwanda, safari hatua,labda kweli tuna viwanda vya magari,sema hatuvioni popote.
Hongera umethubutu,kuna watu wanapinga kila kitu bila kujiongeza au kufanya tafiti za msingi.Na sampuli hizo kula kulala akina pangu pakavu tia mchuzi wako wengi magharasa.
 
Back
Top Bottom