Waziri Lugola: Wizara haihusiki na kupotea kwa Mwandishi wa Kampuni ya Mwananchi Communication Limited, Azory Gwanda

Waziri Lugola: Wizara haihusiki na kupotea kwa Mwandishi wa Kampuni ya Mwananchi Communication Limited, Azory Gwanda

Kangi Lugora yuko sahihi na jinsi swali liliulizwa na huyo Mwandisha wa habari.....Maana mwandishi aliyepotea wala hakukuwa na purukushani wakati anachukuliwa katika ya mji tena mchana kweupe na akaenda kuchukua fungua wa nyumba yake shambani alikokuwa mkewe sasa hapo unataka Waziri aongee nini.
Kwa hiyo mtu akitoweka kwa namna hiyo na familia wakaripoti polisi, si kazi ya polisi kusaidia kumtafuta? kazi ya polisi ni nini sasa!! hadi wapate ushahidi kuwa ametekwa ndio wamtafute?
 
Hayo unayoyaongea yanaweza kuwa yanatokea Tanzania, lakini hayatakiwi yawe hivyo. Wizara ya mambo ya ndani ipo responsible kikatiba kutafuta na kudeal na issue zote zinazohusiana na missing persons.

Kwa kuwa Tanzania zimejaa skwata kila mahali haina maana kuwa hivyo ndivyo inavyotakiwa iwe.
Ndo hivo mkuu!kawaida ni kama sheria, hatujawah kuwa na utaratibu wa polis kutafuta waliopotea Bali ni kutoa taarifa polisi na ndugu au wahusika wenyewe kuendelea kumtafuta ndugu yao.Ila kama ni swala la kutekwa hapa polisi inatakiwa ipambane kuhakikisha wanajua nani kafanya hivo.Kupotea sio uhalifu kama kutekwa na ndo nafikir ni sababu kwanini police huwa hawaangaiki kutafuta watu waliopotea zaid huwa naona kwenye magazeti,TV na sehem mbalimbali watu wakiwatafuta ndugu zao.Kwa kesi ya Azory kama kaondoka nyumbani na haijulikani kaenda wapi au katekwa sioni hoja za mcng za kutaka ufafanuzi kutoka serikalini.Kama alitekwa basi serikali inatakiwa ije na majibu nani wamemteka.Niulize swali Azory katekwa au kapotea?
 
Kwa hiyo mlitaka Waziri aseme mnayotaka nyie kuyasikia? ameongea fact kuwa mtu katoka kwake akiwa na suti yake, katelekeza familia kakimbia. Mnataka wizara ifanye nini sasa? Kuweni na akili mapoyoyo nyie
Umeamua kujitoa ufahamu kwa makusudi
 
Kuandika jina la mtu kwa usahihi ni ishara muhimu ya heshima. Nikushauri tu, uandishi ni kigezo kikubwa cha kupima ueledi na hekima.

Ninarudia tena, kazi ya jeshi la polisi ni kuhakikisha usalama wa kila raia ndani ya mipaka ya Tanzania. Kutokufanikisha wajibu huu, haimaanishi siyo wajibu wao. Ni kama mwalimu asipofundisha au kusahihisha mitihani mara kwa mara halafu hawajibishwi ukasema ni kawaida yake. Hilo ni kosa na halitakiwi kuzoeleka. Kuna taratibu za kuwajibisha serikali na ndio maana tuna Mahakama na Bunge ambazo zinatakiwa kusimamia serikali na taratibu zake. Kama hili halitendeki, basi tukubali tuna ombwe la uongozi. Swali, je tulikabili vipi hilo ombwe, ikiwa lipo?

Tukija kwa mwandishi Azory Gwanda: Ikiwa familia na mwajiri wametoa taarifa ya kutoonekana kwake, Polisi inawajibu wa kumtafuta. Aidha yuko salama au la, ni jambo la kutatua akishapatikana. Ikiwa ametekwa au la, hilo pia ni jukumu la Jeshi la Polisi kufuatilia. Ndio wenye mamlaka, ujuvi na wajibu.
Lini ulisikia polisi wanafanya kazi ya kuwatafuta waliopotea? Mara kibao wanawatangaza kwenye ITV waliopotea, Je ushawah ona polisi wanawatafuta?Huu utaratibu wa polis kutafuta wanaopotea umeanza Lini?Mimi mwenyewe ni mhanga wa hili,mdogo wangu alitoweka tu nyumbani tukatoa taarifa polisi basi na sisi ndugu kuendelea kumtafuta sio polis kumtafuta.Huu ni utaratibu ambao upo na unajulikana,huku kwa Azory mnaleta siasa UCHWARA kutaka kufanya hili ni jukum la polis kumtafuta aliyepotea.Pita huko mitaani kuna mabango kibao ya watu wakiwatafuta ndugu zao na hili halijaanza awam hii,ni miaka nenda rudi iko hivo.Mngekua na hoja za mcng kama mngesema katekwa coz Huu sasa ni uharifu na hapa polisi ilitakiwa iwajibike kuhakikisha inagundua ni akina nani wamefanya Huu uharifu.Sio kazi ya serikali kutafuta waliopotea
 
Jeshi la polisi kazi yake ni nini??

Na jeshi la polisi lipo chini ya wizara gani?
Elewa hoja,huyo hajapotea na hilo tukio sio la kiuharifu.serikali haiwez deal na mambo binafsi ya watu.Ungesema katekwa sawa.
 
Taarifa ya kupotea ndugu yako ulitoa Polisi, na polisi iko chini ya wizara gani? Kama hivyo vyombo havihusiki kwa nini tunaripoti huko?
Nilitoa taarifa sio kwamba wanisaidie kumtafuta,inaweza kapotea na akapatikana sehem kauawa au kajinyonga so hii taarifa inaweza kusaidia hata ktk upelelezi lkn usipotoa taarifa na huyo aliyepotea akapatikana sehem na yuko ktk mattz basi ndugu kuna namna mtawajibika tu.So hatuendi polisi kutoa taarifa kwa lengo la polis wawajibike kumtafuta.
 
Kwa hiyo mtu akitoweka kwa namna hiyo na familia wakaripoti polisi, si kazi ya polisi kusaidia kumtafuta? kazi ya polisi ni nini sasa!! hadi wapate ushahidi kuwa ametekwa ndio wamtafute?
Yah sio kazi ya polisi kumtafuta.Ila kama taarifa ni kuwa katekwa hapa polisi lzm wawajibike kuwatafuta watekaji.
 
Yah sio kazi ya polisi kumtafuta.Ila kama taarifa ni kuwa katekwa hapa polisi lzm wawajibike kuwatafuta watekaji.
Utajuaje kama katekwa au kaamua kuondoka mwenyewe bila ya uchunguzi. Nini kinafanya polisi wajue mtu katekwa. Niikiitwa kwenye dili na wafanyabiashara wenzangu, then wakanigeuka kunipoteza kwa sababu ya tofauti zetu za kibiashara polisi hawatofatilia kwa kuwa niliondoka mwenyewe nyumbani?
 
Utajuaje kama katekwa au kaamua kuondoka mwenyewe bila ya uchunguzi. Nini kinafanya polisi wajue mtu katekwa. Niikiitwa kwenye dili na wafanyabiashara wenzangu, then wakanigeuka kunipoteza kwa sababu ya tofauti zetu za kibiashara polisi hawatofatilia kwa kuwa niliondoka mwenyewe nyumbani?
Taarifa iliyopo ni kapotea
 
Kwa hiyo mtu akitoweka kwa namna hiyo na familia wakaripoti polisi, si kazi ya polisi kusaidia kumtafuta? kazi ya polisi ni nini sasa!! hadi wapate ushahidi kuwa ametekwa ndio wamtafute?
Wengi wanatoweka majumbani kwao kwasababu moja au nyingine si jukumu la polisi kufuatilia mtu aliyetoweka nyumbani kwake hapo elewa vizuri sheria za nchi.Wengi tu wanaasi familia zao na kukimbilia sehemu zingine kutafuta maisha.Wengi wapo migodini na familia zao hazijui na wengine hata kumaliza matanga kumbe watu wako hai sehemu zingine.Polisi inashughulika na uhalifu.
 
Waziri Lugola alisema kama Gwanda alitoweka wakati akiwa nyumbani, wao hawahusiki bali wanahusika na mtu aliyetendewa uhalifu ikiwamo kutekwa, akisema katika tukio kama hilo vyombo vya dola humtafuta mtekaji.

“Hawa ambao wanatoweka kwao tu, wanakuwa na sababu nyingi. Kuna wengine maisha yakiwashinda anaamua kwenda kwingine,” alisema.


...
 
Back
Top Bottom