Tetesi: Waziri Maghembe kutumbuliwa

Wazir mkuu alisema kuwa serikali imetoa trilion 1 kununua madawa. Magufuli akasema serikali imetoa billion 200 kunuNua dawa. Nani apo ni muongo?
Ww ndiyo muongo, jamaa hao ndiyo serikali utapiga kelele bure subiri cdm yenu mwaka 2200
 
Kumtumbua Maghembe ni uonevu mkubwa. Kama jambo hili la faru john limefanyika ndani ya awamu hii basi waziri mkuu Majaliwa Kasimu Majaliwa ajiuzuru.

Yeye ndiye mtendaji mkuu wa serikali, iweje waziri aliye chini yake auze nyara za umma halafu waziri mkuu ajipe kazi ya kukata mkono wake (waziri)
 
Mimi sijui wanapinga maelezo ya uzi huo wanahitaji nini hasa, wanataka waziri mkuu aseme uongo au wale waliohusika na kupotea kwa faru wachukuliwe hatua
 
Nauliza hiviiiiiiiiii eti ile mahakama ya mafisadi ipo au haipo ? Kama ipo kwanini hawa wasipelekwe huko ?

Bado mafundi wanapaka rangi, kisha viwekwe na vigaye chini, hapo mambo uatakuwa tayari.
 
watumbuane tu.maana me nishachoka ikiwezekana rais avunje baraza lote
 

Angalieni asije akataka na jina la padri alieendesha misa ya kumzika marehemu John......
 
ni malaika nadhani! hehe
Unajua, wakati wa JK, Waziri angeliweza kusema ukweli na akadumu kazini. Leo siyo hivyo. Utatumbuliwa. Lazima useme uongo umpendezeshe. Nasikia????? not confirmed please- nilisoma humu JF kuwa kuna wilaya fulani wanalaza wagonjwa wa kipindupindu katika wodi za kawaida kuogopa kuambiwa kuwa wameshindwa kusimamia usafi DC and therefore risk being fired (kutumbuliwa)- sijui kama ni kweli????
 
Sipo kwenye hoja ya faru kwa kuwa siujui undani wake.lakini napinga maelezo yanayosema waziri mkuu hawezi kusema uongo hali na yeye ni binadamu na mpaka alipofikia kwenye suala la faru ameshawahi kudanganya akiwa jimboni mwake kuwa ajira mpya za walimu hususani wa sayansi zitatoka julai kitu ambacho hakikutokea mpaka leo
 
Hivi Ben na faru yohana nani was maana
Kila kitu kinaangaliwa katika context yake Beni ni wa muhimu serekali lazima iwajibike kumtafuta kupitia vyombo vyake vya kipelelezi polisi ....kwa upande mwingine vita ya kupambana na ujangili ni muhimu lazima iendelee ...kwa hiyo udadisi wa faru john ni muhimu sana
 
information ya kwamba faru alizikwa ameipata kwenye report waliompelekea. wao ndo waliosema wamemzika. sasa waseme walipomzika watu wafanye vipimo tujue mbichi na mbivu.
 
Maendeleo ya kweli yanapatikana kwa kufanya kazi kwa bidii , nidhamu ya mtumizi na heshima kwa maslimali zako na zataifa zaidi ya hapo ni kupiga mbizi kwenye mchanga tu na bahati mbaya wezi wa nchi hii ni wasomi sasa unajiuliza watu wenye kutakiwa kutupeleka kwenye nchi ya ahadi ndio wafalme wa Egypt
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…