Tetesi: Waziri Maghembe kutumbuliwa

Tetesi: Waziri Maghembe kutumbuliwa

Kwa PM kudai kaburi la uncle Faru John ni kutokana na maelezo ya wataalamu wa hifadhi kuwa alikufa kwa ugonjwa,na akifa kwa ugonjwa na ikathibitika hivyo,huzikwa ili kutoleta maambukizi kwa wanyama wengine wala mizoga kama fisi na mbwa mwitu,hivyo watuonyeshe kaburi lake,la hasha kama kama hakufa kwa ugonjwa ni kipi kilichomuua?
 
Alinifukuza chuo huyu akafanya nihamie bara lingine kabisa . Naamini zamu yake nae imefika kuishi kama shetani.

[HASHTAG]#BringBackBenAlive[/HASHTAG].
Duh!kama ni kweli na kama alikuonea acha zamu yake ifike haraka haraka,binafsi siwapendi watu wanaokatisha ndoto za wenzao kwa uonevu.
 
Kwa PM kudai kaburi la uncle Faru John ni kutokana na maelezo ya wataalamu wa hifadhi kuwa alikufa kwa ugonjwa,na akifa kwa ugonjwa na ikathibitika hivyo,huzikwa ili kutoleta maambukizi kwa wanyama wengine wala mizoga kama fisi na mbwa mwitu,hivyo watuonyeshe kaburi lake,la hasha kama kama hakufa kwa ugonjwa ni kipi kilichomuua?
Mkuu umeongea jambo la msingi sana. Hiki ulichoongea hasa ndio mzizi wa skandali hii. Sioni jinsi ambavyo hili jangili (Maghembe) litanusurika katika sakata hili hasa ukizingatia naye alikuwa mstari wa mbele kumdanganya PM. Sasa anapoombwa atuoneshe lilipo kaburi hilo anabaki anang'aang'aa na kupepesa macho kama tutusa. Ajitokeze kutoka huko mafichoni aliko atuoneshe kaburi. Hicho tu ndicho tunachokitaka...na asidhani akionyesha kaburi itaishia hapo...maana asije akaenda mbio mbio kuua tembo na kumzika akaja kutuambia ni John...vinasaba vitapimwa babu wee! Hapa ndipo patamu. Yaani hana pa kuchomokea...maji yako shingoni.

[HASHTAG]#bringbackourrhinoalive[/HASHTAG]
 
Mi namkumbuka Waziri Mkuu mmoja tu aliyediriki kuweka uongo na kudanganya...sasa hivi Yuki chadema
Kwani mahakama za mafisadi hazijaanza apelekwe huko akajibu tuhuma hizi?
 
kama huyu faru john alipigwa deal basi wapigaji wamepiga deal kwa kutumia akili nyingi sana..
siku ya kwanza PM anauliza kwa nini alitolewa serengeti?
anajibiwa majibu ya kitaaluma mpaka anaishiwa nguvu.
1.faru john aliondolewa setengeti kwa sababu tulitaka ku control in breeding
2.aliondolewa kwa sababu ya ukorofi wake kitu ambacho kilihatarisha uhai wa faru wengne kwamba alikuwa anawafukuza mpaka wanaenda nje ya conservation area kitu ambacho ni rahisi kuuliwa na majangili..
2.huko gurunet alikufa natural dealth sababu ya umri na upweke kwani aliwekwa ndani ya cadge.
jibu hilo linaua doubt kuwa faru aliuawa kwa kukusudia ila pembe zipo
4.naomba mfukue kabri ili apimwe vinasaba
anajibiwa.mzee faru john hakufa kwa ugonjwa wa maambukizi ila uzee hivo hakuzikwa ili ku suport food chain na ecology kwa wanyama walao mizoga.
hivi kwa sababu hizi nani atashikwa uchawi juu ya faru john.
halafu wahifadhi wanajibu kitaaluma na kwa confidence zote
PM.Kapigwa na butwaa je ?taarifa ya ki intelijensia imenipotosha au wapiga dili wanatumia akili nyingi..
Mkuu nchi hii inaongozwa na ukoo wa panya...usiumize kichwa. Wapiga deal wanaanzia Magogoni hadi kule kijijini Mtakuja. Inauma sana.
 
IMG-20161221-WA0002.jpg
 
kama huyu faru john alipigwa deal basi wapigaji wamepiga deal kwa kutumia akili nyingi sana..
siku ya kwanza PM anauliza kwa nini alitolewa serengeti?
anajibiwa majibu ya kitaaluma mpaka anaishiwa nguvu.
1.faru john aliondolewa setengeti kwa sababu tulitaka ku control in breeding
2.aliondolewa kwa sababu ya ukorofi wake kitu ambacho kilihatarisha uhai wa faru wengne kwamba alikuwa anawafukuza mpaka wanaenda nje ya conservation area kitu ambacho ni rahisi kuuliwa na majangili..
2.huko gurunet alikufa natural dealth sababu ya umri na upweke kwani aliwekwa ndani ya cadge.
jibu hilo linaua doubt kuwa faru aliuawa kwa kukusudia ila pembe zipo
4.naomba mfukue kabri ili apimwe vinasaba
anajibiwa.mzee faru john hakufa kwa ugonjwa wa maambukizi ila uzee hivo hakuzikwa ili ku suport food chain na ecology kwa wanyama walao mizoga.
hivi kwa sababu hizi nani atashikwa uchawi juu ya faru john.
halafu wahifadhi wanajibu kitaaluma na kwa confidence zote
PM.Kapigwa na butwaa je ?taarifa ya ki intelijensia imenipotosha au wapiga dili wanatumia akili nyingi..

Hahahaaaa! Na kaomba Pembe kaletewa Pembe za Fudu Pori ahangaike nalo lile la Faru John washatengenezea Mkuyati wa Kichina watu wametumia na sasa wapo juu ya Viuno wanapiga show
 
Hahahaaaa! Na kaomba Pembe kaletewa Pembe za Fudu Pori ahangaike nalo lile la Faru John washatengenezea Mkuyati wa Kichina watu wametumia na sasa wapo juu ya Viuno wanapiga show
Hahahahahahaaaaaaaaaa! Mkuu una maneno wewe.
 
maghembe na makaburu wa Sasakwa wanajuwa kila kitu warudish Faru wetu.Hawa CCM hawana jipya tulisha sema Faru wao Tembo wao.Halafu Mwakyembe anakuja na mbwembwe eti mahakama ya mafisadi haina kesi badala ya kusema haijui ianze na nani maana wote ni majizi watupu.Aibu yako Mwakyembe unaaibisha taaluma yako nenda kafundishe.
 
Hawezi kutumbuliwa kwa 100%

Akitumbuliwa hamna tena waziri kutoka kaskazini
 
Hawezi kutumbuliwa kwa 100%

Akitumbuliwa hamna tena waziri kutoka kaskazini
Kwani yupo pale kwa sababu ya UKASKAZINI wake? Kama ndivyo, basi ataendelea kuua vifaru wetu hadi atosheke mwenyewe!
 
Kuna kila dalili kwamba Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe amekalia kuti kavu, tena kavu kwelikweli.

Sakata la kuuzwa kwa faru John na kisha yeye kubariki uuzwaji huo ni udhaifu mkubwa sana na kigezo tosha cha kumfanya aondolewe kwenye nafasi yake ya sasa. Kwa mujibu wa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Majaliwa, inasemekana faru huyo aliuzwa kwa thamani ya Tsh milion 200, ambapo wauzaji walitanguliziwa malipo ya Tsh milioni 100. Waziri mkuu hawezi kusema uongo. Ni dhahiri anazo taarifa za uhakika za kiintelejensia kwamba faru ameuzwa kwa bei hiyo ya kutupwa. Ndio maana wahifadhi wanashindwa kuonyesha kaburi lake lilipo kama kweli mnyama huyo wa porini alikufa.

Sintofahamu hii inakolezwa zaidi na Maghembe mwenyewe aliyediriki kumdanganya Waziri Mkuu, kwa kushirikiana na wezi wenzake, kwamba faru yule 'amekufa' huku akijua kwamba anasema uongo. Kwa sababu hizi, pamoja na sababu nyingine ambazo bado hazijawekwa wazi ili kumtumzia heshima profesa huyu, kuna kila dalili kwamba huenda Rais, Dr Joseph Pombe akatengua uteuzi wake kabla hajamaliza faru wetu.

Ikiwa waziri mwenye dhamana ya kulinda rasilimali zetu, ama kwa kujua au kwa makusudi, ameamua kushirikiana na majangili kufilisi rasilimali zetu kuna haja gani ya kuendelea kukalia kiti cha uwaziri? Kwa dhati kabisa bila unafiki wowote, mimi namuunga mkono Rais Pombe katika utumbuaji huu. Ifike wakati kila mtu aheshimu rasilimali za taifa kwa manufaa ya watanzania wa sasa na vizazi vijavyo.

Mungu mbariki Rais wetu, Mungu wabariki watanzania, Mungu bariki rasilimali zetu za Taifa. Amen.

[HASHTAG]#bringbackourrhinoalive[/HASHTAG]
Atumbuliwe kwann alidanganye taifa kuwa faru john amekufa wakat kauzwaa
 
Back
Top Bottom