Tetesi: Waziri Maghembe kutumbuliwa

Tetesi: Waziri Maghembe kutumbuliwa

tpaul kwa hakika wewe unaongea kinafiki kwa kuvunga eti unamsifia JPM ili tu ionekane anatumbua mawaziri wengi nakwamba Serikali yake inayumba au kukosa uimara. Wewe ni Li-Chadema, acha unafiki wako. Tumeshakugundua, huwezi kutujaza ujinga ng'o.
 
Kwani mahakama za mafisadi hazijaanza apelekwe huko akajibu tuhuma hizi?
Sijaongelea ufisadi Bali kusema uongo na kudanganya kwa Waziri Mkuu wa kipindi Fulani...akadanganya tena kuwa hawezi Kutoka ndani ya chama kilichomlea...historia inamhukumu
 
Wait....huyu bwana John kafa au kapotea na yeye? Mbona kama mtoa mada kama sijakuelewa vile....Kama umekuja na taarifa yako nyingine vile
 
Wait....huyu bwana John kafa au kapotea na yeye? Mbona kama mtoa mada kama sijakuelewa vile....Kama umekuja na taarifa yako nyingine vile
Rudia tena kusoma uzi mkuu. Faru Johm kauzwa na Maghembe akishirikiana na genge lake la majangili kwa thamani ya Tsh milioni 200. Baada ya kumuuza wamesingizia kwamba faru alikufa wakamzika. PM kawaambia wakamletee mifupa yake ipimwe DNA, wahusika wameingia mitini.
 
Rudia tena kusoma uzi mkuu. Faru Johm kauzwa na Maghembe akishirikiana na genge lake la majangili kwa thamani ya Tsh milioni 200. Baada ya kumuuza wamesingizia kwamba faru alikufa wakamzika. PM kawaambia wakamletee mifupa yake ipimwe DNA, wahusika wameingia mitini.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] kwa hiyo mkuu sasa huyu jamaa john yupo somewhere katulia? Au kauzwa then akafa? Hapa ndo panaponichanganya sasa....
 
Kuna kila dalili kwamba Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe amekalia kuti kavu, tena kavu kwelikweli.

Sakata la kuuzwa kwa faru John na kisha yeye kubariki uuzwaji huo ni udhaifu mkubwa sana na kigezo tosha cha kumfanya aondolewe kwenye nafasi yake ya sasa. Kwa mujibu wa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Majaliwa, inasemekana faru huyo aliuzwa kwa thamani ya Tsh milion 200, ambapo wauzaji walitanguliziwa malipo ya Tsh milioni 100. Waziri mkuu hawezi kusema uongo. Ni dhahiri anazo taarifa za uhakika za kiintelejensia kwamba faru ameuzwa kwa bei hiyo ya kutupwa. Ndio maana wahifadhi wanashindwa kuonyesha kaburi lake lilipo kama kweli mnyama huyo wa porini alikufa.

Sintofahamu hii inakolezwa zaidi na Maghembe mwenyewe aliyediriki kumdanganya Waziri Mkuu, kwa kushirikiana na wezi wenzake, kwamba faru yule 'amekufa' huku akijua kwamba anasema uongo. Kwa sababu hizi, pamoja na sababu nyingine ambazo bado hazijawekwa wazi ili kumtumzia heshima profesa huyu, kuna kila dalili kwamba huenda Rais, Dr Joseph Pombe akatengua uteuzi wake kabla hajamaliza faru wetu.

Ikiwa waziri mwenye dhamana ya kulinda rasilimali zetu, ama kwa kujua au kwa makusudi, ameamua kushirikiana na majangili kufilisi rasilimali zetu kuna haja gani ya kuendelea kukalia kiti cha uwaziri? Kwa dhati kabisa bila unafiki wowote, mimi namuunga mkono Rais Pombe katika utumbuaji huu. Ifike wakati kila mtu aheshimu rasilimali za taifa kwa manufaa ya watanzania wa sasa na vizazi vijavyo.

Mungu mbariki Rais wetu, Mungu wabariki watanzania, Mungu bariki rasilimali zetu za Taifa. Amen.

[HASHTAG]#bringbackourrhinoalive[/HASHTAG]
Faru aliuzwa kabla hajawa Waziri acha uongo wewe mwongo
 
Faru aliuzwa kabla hajawa Waziri acha uongo wewe mwongo
Nani muongo? Maghembe? Ni kweli Maghembe ni muongo....hata kama hakuwepo wakati anauzwa kwanini amdanganye waziri mkuu kwamba yule faru amekufa ilhali wamemuuza kwa makaburu?
 
Magufuli ni mtu wa visasi...kamwe hawezi kuwateua wapinzani zaidi ya alivyompoza Mrema kwa jitihada zake za kubomoa upinzani.
Hii nchi bhanaa ni shidah! Watu saba kwenye viroba wamekutwa wamekufwa na mawe juu wasionekane, mtaani ibaki stori, polisi kampiga mtoto risasi, ikasemwa polisi alilenga kupiga kwenye lami ikapita, polisi wamevamiwa wakauwawa, wakati mwingine wakaporwa silaha ikapita. sasa faru kupotea imekuwa ishu? Hivi thamani ya watanzania uhai wao si kitu ukilinganisha na wa wanyama pori? Uwiiiiiiiiii
 
Sina uhakika na jambo hili lakini jana nilisikiliza maelezo ya ni namna gani mnyama ambae hakufa kwa magonjwa yasiyoambukiza, dispoasal yake haiwezi kuwa kwa kuzikwa!

Haijalishi kama Faru John amekufa kweli or not; lakini ikiwa PM hakuambiwa Faru John alikufa kwa maradhi ya kuambukiza basi ile kuagiza kaburi lifukuliwe peke yake inatosha kuonesha huwa anaropoka bila kutafiti kidogo! Endapo angetumia dakika 5 tu kutafiti basi angejuwa aina ya "kifo" cha John haikutakiwa kuzikwa na hivyo badala ya kuagiza kaburi kufukuliwa angeagiza kuoneshwa ni wapi mzoga wa John ulitelekezwa! Na kwa mtindo huu si ajabu hatimae akaagiza "nendeni Gurunet mkaangalie masalio ya Faru John hapo alipotelekezwa" Hatimae ataletewa jibu Fisi wamekula hadi mifupa kwahiyo hamna hamna masalio!"
wewe nae jiongeze, walipataje zile pembe, kama hawajui mahali alipofia, kwa kuwa alikuwa chini ya uangalizi maalumu, lazima alipo kufa picha za kumbukumbu zilichukuliwa, na mwenendo wa afya yake lazima zilikuwa zinarekodiwa, nahivi ndo PM anavitaka, reasoning beyond dought
 
wewe nae jiongeze, walipataje zile pembe, kama hawajui mahali alipofia, kwa kuwa alikuwa chini ya uangalizi maalumu, lazima alipo kufa picha za kumbukumbu zilichukuliwa, na mwenendo wa afya yake lazima zilikuwa zinarekodiwa, nahivi ndo PM anavitaka, reasoning beyond dought
Sasa nijiongezee nini hapo?!
 
Sasa nijiongezee nini hapo?!
ujiongeze kutoka kwenye maelezo uliosikia, rhino are endemic species, wapo chini ya uangalizi maalumu ndo maana wameitwa hadi majina, si rahisi akafa bila kuwepo na rekodi za msingi
 
ujiongeze kutoka kwenye maelezo uliosikia, rhino are endemic species, wapo chini ya uangalizi maalumu ndo maana wameitwa hadi majina, si rahisi akafa bila kuwepo na rekodi za msingi
Umenisoma kwa vituo ukanielewa?!
 
wewe nae jiongeze, walipataje zile pembe, kama hawajui mahali alipofia, kwa kuwa alikuwa chini ya uangalizi maalumu, lazima alipo kufa picha za kumbukumbu zilichukuliwa, na mwenendo wa afya yake lazima zilikuwa zinarekodiwa, nahivi ndo PM anavitaka, reasoning beyond dought
Mkuu kuna baadhi ya watu humu wanapenda kujitoa akili utadhani wamekatwa vichwa.
 
Sasa sio TETESI tena bali ni DHAHIRI. Waziri Mkuu amekasirika sana baada ya kugundulika kwamba Prof Maghembe alimuonyesha pembe feki za faru na wala hazikuwa za faru John kama ilivyotarajiwa. Baada ya habari hizi kumfikia Rais Makufuri anatarajiwa kumtangaza mrithi wa Maghembe muda wowote juanzia sasa.

Mods tafadhali naomba mbadilishe status ya uzi huu kutoka TETESI kuwa BREAKING NEWS!
 
Sasa sio TETESI tena bali ni DHAHIRI. Waziri Mkuu amekasirika sana baada ya kugundulika kwamba Prof Maghembe alimuonyesha pembe feki za faru na wala hazikuwa za faru John kama ilivyotarajiwa. Baada ya habari hizi kumfikia Rais Makufuri anatarajiwa kumtangaza mrithi wa Maghembe muda wowote juanzia sasa.

Mods tafadhali naomba mbadilishe status ya uzi huu kutoka TETESI kuwa BREAKING NEWS!
Umetisha..kama vile ulikua ukimchungulia Faru John all the time
 
Back
Top Bottom