Waziri Mahiga: Serikali ya Uturuki imetuambia wamiliki wa shule za Feza ni magaidi

Waziri Mahiga: Serikali ya Uturuki imetuambia wamiliki wa shule za Feza ni magaidi

Kurzweil

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2011
Posts
6,621
Reaction score
8,411
Serikali ya Tanzania yasema haina ushahidi wa kutosha kuzitia hatiani shule za Feza zinazodaiwa kumilikiwa na raia wa Uturuki anayetuhumiwa kujihusisha na jaribio la kupindua Serikali ya Uturuki.

Serikali ya Uturuki inadai wamiliki wa shule hizo na baadhi ya wafanyabiashara wanafadhili ugaidi kwa kushirikiana na Imamu Fethullah Gulen anayeishi nchini Marekani ambaye ndio inadaiwa yuko nyuma ya jaribio la Mapinduzi.

= > Serikali ya Uturuki yatakiwa kuwasilisha taarifa zenye ushahidi wa kutosha juu ya hili.

= > Aidha, Ubalozi wa Uturuki Tanzania umedai kuwa baadhi ya walimu wa shule za FEZA ambao ni raia wa Uturuki wamekuwa wakitumia mbinu za kigaidi kufundisha wanafunzi.

Feza wamekanusha kuhusika

Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Augustino Mahiga amesema serikali ya Uturuki kupitia balozi wake hapa nchini imedai wamiliki wa shule za Feza Tanzania walifadhili jaribio la mapinduzi Uturuki

Serikali hiyo inadai mapinduzi hayo hayakuanzia jeshini tu bali yameanzia kwenye vyuo na shule mbalimbali Uturuki na nje ya uturuki
Ubalozi wa Uturuki umesema wamiliki wa shule hizo hapa nchini wanahusika na kufadhili mapinduzi hayo huko Uturuki na ada inayokusanywa kutoka kwenye shule hizo ilitumika kufadhili mapinduzi hayo na ni magaidi
Balozi Mahiga amesema wametaka ushahidi zaidi kutoka serikali ya Uturuki kuhusu madai hayo



Walimu wa shule ya Feza wamedai wao hawahusiki kabisa na mapinduzi hayo na shule zao hazijihusishi na mambo ya siasa na zinamilikiwa na watanzania
 
Unamaanisha wa

Unamaanisha Waturuki wazushi
Waturuki kwahili ni wazushi, wao walitaka kupinduana.

Sasa mas-ala yao ya kisiasa wameamua kumfatilia kila mpinzani anayeishi hata kama nje ya nchi katika sehemu yeyote hile duniani ikiwemo tanzania kumzima kwa njia yoyote hile.

Kwahiyo wanataka kuitumia tanzania kisiasa kutaka kuwazima wamiliki wa feza kwakuwa chama kinachotawala uturuki kinaamini kuwa ni wapinzani.

Na kwa mujibu wa uturuki katika jitihada zao za kutaka kuzima upinzani basi wamehukumu kuwa kila mpinzani basi kwa njia moja au nyengine itakuwa alihusika katika mapinduzi.
 
Waturuki kwahili ni wazushi, wao walitaka kupinduana.

Sasa mas-ala yao ya kisiasa wameamua kumfatilia kila mpinzani anayeishi hata kama nje ya nchi katika sehemu yeyote hile duniani ikiwemo tanzania kumzima kwa njia yoyote hile.

Kwahiyo wanataka kuitumia tanzania kisiasa kutaka kuwazima wamiliki wa feza kwakuwa chama kinachotawala uturuki kinaamini kuwa ni wapinzani.

Na kwa mujibu wa uturuki katika jitihada zao za kutaka kuzima upinzani basi wamehukumu kuwa kila mpinzani basi kwa njia moja au nyengine itakuwa alihusika katika mapinduzi.
Hapo sawa mkuu
 
Wagaratia wanaozungumziwa kwenye biblia ndio Waturuki haswa. Nadhani waislam wote waeleweni hii jamii ndio tabia yao wakigombana wao kwa wao na wewe una urafiki nao wote wanakuambia uchague upande mmoja. Zama hizo waliitwa watu wapumbavu.

Erdogan anatumia mwanya Wa mapinduzi kuteketeza adui zake wote. Hadi walimu wauza pipi n.k yaani mpango wake sio kuwazuia au kuwafunga Bali kuwanyonga wote. Watatoa msimamo wao soon na hizo shule watazichukua serikali ya Ankara
 
Watoto Wa wakubwa na matajiri na watu wenye uwezo wao ndio wanasoma shule hizo hawawezi kuzifungia zaidi watawambia wapinzani Wa erdogan popote duniani wake kuwwkeza Tanzania watawalinda. Hizo shule zikifungwa zitakatisha ndoto za watoto Wa vigogo. Hilo haliwezekani ndio maana Ada elekezi ilishindikana
 
Nadhani Ni Wanafunzi Waliosoma FEZA tu pekeyao Ndiyo Wenye Haki Kamili Hapa Ya Kuja Kututhibitishia Hayo Madai Yaliyotolewa Ya Kuwa Walimu Wanatumia Njia Za Kigaidi Kufundishia Je Ni Kweli? Njooni Mutupe Ushuhuda...

Mimi nafikiri Rais wa Uturuki anatafuta mbinu za kuwanaliza Waturuki wote wenye uwezo kifedha ambao anahisi wanaweza kula njama za kumuondoa madarakani, ni hilo tu.

Viongozi wengi Duniani wasio jiamini utumia mbinu hizo kuwadhibiti/kuonea raia wanao wahisi vibaya, hata baadhi ya Viongozi wa Africa Mashariki na Kati wanatumia sana mbinu hizo wangine wanafikia hatua ya kuwauua popote walipo au kuwafunga maisha.
 
Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Augustino Mahiga amesema serikali ya Uturuki kupitia balozi wake hapa nchini imedai wamiliki wa shule za Feza Tanzania walifadhili jaribio la mapinduzi Uturuki

Serikali hiyo inadai mapinduzi hayo hayakuanzia jeshini tu bali yameanzia kwenye vyuo na shule mbalimbali Uturuki na nje ya uturuki
Ubalozi wa Uturuki umesema wamiliki wa shule hizo hapa nchini wanahusika na kufadhili mapinduzi hayo huko Uturuki na ada inayokusanywa kutoka kwenye shule hizo ilitumika kufadhili mapinduzi hayo na ni magaidi.

Balozi Mahiga amesema wametaka ushahidi zaidi kutoka serikali ya Uturuki kuhusu madai hayo



Walimu wa shule ya Feza wamedai wao hawahusiki kabisa na mapinduzi hayo na shule zao hazijihusishi na mambo ya siasa na zinamilikiwa na watanzania
 
Back
Top Bottom