Waziri Makamba kaanza vibaya, nahofia atafeli kama wenzie

Akili yq mtu upimwa kwa kazi zake na maneno yake. End
 
Wazo la kuletwa CEO kutoka nje ni la ovyo kuliko la makamba kufukuza fukaza watu,nalo ni la kishamba

The bad news ni kua Tanesco ni taasis tegemezi ya cartels za upigaji.cartel kuu inategemea sana huko.

And the good news is the man is out now
 
Katoa vitisho juzi...

Leo Jiji halina umeme umekatika...
 
Hili la kusema MD atoke nje ya nchi sio sahihi.Hivi unakumbuka TANESCO iliwahi kuongozwa na watu kutoka nje wanaitwa "Net grouy solution?"walileta manufaa gani?


Net solution hawakupewa kazi ya kuliimarisha Tanesco..walipewa kazi ya kuliandaa kuliuza ..
Huwezi sema walifeli wakati hawakutakiwa kukufanya lijiendeshe kifaida ...wala kulifanya liwe bora
 
Bila kuondoa monopoly policy, hayo mengine ni makelele cheap sana.
Maya zaidi watenda kazi walibainisha sababu za wazi na halisia za kukatika umeme
 
Tunajua jukumu la kwanza ni kuvunja management ya Tanesco tupate uwanja wa kufanya yetu. Team GASOM
 
JPM alimponda waziri wake mmoja kwa kushindwa kuondosha mifuko ya plastic kulinda mazingira. Sasa huku kwenye umeme sijui atawezaje.
 
Cha kufanya amrudishe eng mramba kuwa managing director jamaa yupo vizuri alitolewa kwa fitina tu za muhongo na magu
 

Ustaz the boss,, acha awanyooshe kidogo hao tanesco.
 
Sio huyo tu, hata yule alqaeda wa habari nae kapinga Mkwara mzito! Tatizo ni recycling wanaturudishia magarasa hayajui kwamba hayajui!
 
Cha kufanya amrudishe eng mramba kuwa managing director jamaa yupo vizuri alitolewa kwa fitina tu za muhongo na magu
Utakuwa ni mnufaika wa Mramba bila shaka. Baada ya Idrisa, hakuna MD wa Tanesco aliyekidhi vigezo.

Mramba ni mwanafunzi wa Mhando, yeye akiwa ndo junior kwenye top layer, Mhando alipenda kumkaimisha nafasi kwakuwa jamaa ni bingwa wa kutoa maandiko ambayo yalikuwa yakikubalika sana wizarani, hivyo Mhando kunuona mwana kuwa ndio wing man wake.

Mhando alijenga safu yake ambayo ni Tangaline, na kila kitu cha shirika kikahamishiwa Tanga. Mramba, unadhani alifanya tofauti?

Akae MD yeyote pale, kama hana hulka za kijiwe, hawezi kufanya vizuri, kulikuwa na safu ya kanda ya ziwa pale, ndio ilikuwa creamy ya shirika, wao ndo wanaamua mwenendo wa shirika. Kamuulize aliyewahi kuwa GM wa mwisho kabla ya 2010, kabla cheo hicho hakijavunjwa, pia kina DMDs watakuambia mchezo ulivyo.

Wanasema chama cha kijani, mrija wake pia uko hapo, muulize Ngeleja alikuwa anafanya nini? Iulize tume ya Warioba, walikuwa wananyonya wese la magari yao kutoka wapi? Waulize walimwengu, zile VX V8 za kijani mawilayani kwaajili ya kampeni kipindi cha Vasco, nani alinunua? Ndivyo wananchi wanavyonong'ona.
 
JPM alimponda waziri wake mmoja kwa kushindwa kuondosha mifuko ya plastic kulinda mazingira. Sasa huku kwenye umeme sijui atawezaje.
Makamaba ni failure tokea mwanzo na kaletwa na failure mwenzake!
 
Humjui makamba wewe
 
Aisee ikawa asuhuhi, ikawa jioni siku ya pili! Muyaonapo haya yanatokea basi mjue mwana wa adamu anakuja kuchukue kiumbe!

Tuombeeee!!!
 
Makamba atachoka akifuata kila ushauri unaotolewa humu...kila mtu anaonekana anataka kumfundisha kazi.
Watanzania hawana raisi mwema wala waziri mwema, kazi ni malalamiko tu. Mtu ameteuliwa hata wiki haijafika tayari malalamiko. Labda tusubiri malaika kutoka mbinguni ndiyo waje kutuongoza.
 
Hii wizara ni lawama tu,
Mbaya zaidi January amewekwa kwa lengo la upigaji tu
 
Hili la kusema MD atoke nje ya nchi sio sahihi.Hivi unakumbuka TANESCO iliwahi kuongozwa na watu kutoka nje wanaitwa "Net grouy solution?"walileta manufaa gani?
Aliyeweza kuendesha tanesco mpaka ikawa kwenye mrengo wa kupata faida ni Idris Rashid peke yake, maana yule alikuwa na muelekeo wa kibiashara. Mimi niliambiwa hayo na wafanyakazi wenyewe wa tanesco kipindi kile.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…