Waziri Makamba: Sasa Serikali itanunua shehena ya mafuta moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji

Waziri Makamba: Sasa Serikali itanunua shehena ya mafuta moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji

Habari nzuri sana hii.Huu ndio ubunifu.Huyu Waziri wetu,ni mchapakazi na mbunifu.
Tayari, kilaza m'moja kashalewa anaanza kumwaga sifa. [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Aiseeeeeee ndio maana CCM imetoboa miaka 60.
 
Mheshimiwa waziri kwa hili la kuondoa mtu kati kwenye uagizaji wa mafuta ukifanikiwa utakuwa umewasaidia sana watanzania. Mungu akusaidie maana najua mpambano wake si wa kitoto.
Hivi katika akili ya kawaida tu na nyepesi, hao waliotangulia wote hawakuona hiyo solution?!

Hapa kuna mchezo tunachezewa mchana kweupe. Ni swala la muda tu tutajua shida imejificha wapi.
 
Usisahau kuwa nyie ndio wamiliki wa makampuni makubwa ya mafuta na mnalinda maslahi yenu
Hii ni changa la macho. Hivi kimsingi eti ni kwamba eti jamaa hawa wachuuzi wa mafuta wafutwe kishkaji tu wawe wapole ili serikali iagize yenyewe.

Magufuli alishindwa kufanya hilo swala na vile alivyokuwa anapenda kuwakomoa hawa madalali wa soko huria.

Kuna kitu kitakwenda kufanyika, ukweli utakuja kujulikana na watu hawataamini namna tutakavyokuwa tumepigwa.

Ogopa sana mtu anaefosi kuonekana ni smart na brain kali above all. Na mbaya zaidi awe na tamaa ya uraisi huku anapretend hana shida nao.

Its just a matter of time. True colors will show.
 
Hizi ngonjera zake za kila siku zinatofauti gani na zile za uchumi wa kati wakati nusu ya watanzania ni masikini?

Hiyo shehena inaweza kuagizwa na bado isisaidie chochote kupunguza gharama, hasa wakati huu waziri husika anahangaika kutafuta pesa za kampeni ya kufanikisha "ndoto" yake, haka kajamaa hata sikaamini.

Kwanza kwenye huo mfuko/bahasha kamebeba nini?
Me too. This guy is very fishy and creepy in a political way.
 
TAARIFA KWA UMMA KUTOKA WIZARA YA NISHATI KUHUSU ZIARA YA WAZIRI JANUARY MAKAMBA

Kama inavyofahamika, bei ya mafuta ghafi duniani imeendelea kupanda kwa kasi na kwa kiwango kikubwa, kutoka dola 50 kwa pipa mwezi wa Januari mwaka huu hadi dola 86 kwa pipa leo tarehe 31 Oktoba 2021.

Hali hii inapelekea bei kupanda kwenye vituo vya kuuzia mafuta na mitaani hapa nchini.

Kama itakavyokumbukwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, alielekeza hatua mbalimbali za kikodi, kisheria/kanuni na kiutawala ili kupunguza makali na athari za ongezeko hili la bei. Wizara ya Nishati imeanza kutekeleza maelekezo hayo na pia kuratibu hatua mbalimbali za Wizara na taasisi nyingine za umma na kufanikiwa kupunguza ongezeko kubwa la bei ya mafuta kwa mwezi wa Oktoba.

Katika kutimiza azma ya Mheshimiwa Rais ya kuhakikisha kwamba bei za mafuta haziumizi wananchi, na shughuli za uchumi haziathiriki, Wizara ya Nishati ilichunguza na kubaini uwezekano wa unafuu wa bei iwapo Serikali yenyewe itanunua mafuta moja kwa moja kutoka kwenye mitambo ya kusafisha mafuta (refineries) ya nchi rafiki badala ya kuachia watu wa katikati (intermediaries) kununua kwa nchi hizo hizo rafiki zetu na kutuuzia kwa bei kubwa.

Kutokana na hilo, katika duru la kwanza, kuanzia tarehe 22 hadi 29 Oktoba 2021 nilifanya ziara katika nchi tatu – Saudi Arabia, Umoja wa Falme za Kiarabu na Algeria – ambazo zinazalisha mafuta kwa wingi na kuuza kote duniani. Katika nchi hizo, nilikutana na Mawaziri wenzangu wa Nishati, na viongozi wengine waandamizi wa Serikali na makampuni 2 ya mafuta ya Serikali za nchi hizo. Vilevile, nilibeba ujumbe maalum wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa viongozi wa nchi hizo.

Katika ziara hiyo, niliongozana na Ndugu Michael Mjinja, Kamishna wa Petroli na Gesi katika Wizara ya Nishati na Ndugu James Mataragio, Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC. Pia, mabalozi wetu katika nchi hizo walishiriki katika vikao na mazungumzo niliyoyafanya.

Madhumuni ya ziara hiyo yalikuwa ni kama ifuatavyo:-

1. Kuzungumza na nchi rafiki zinazozalisha mafuta ili kuangalia uwezekano wa Serikali, kupitia Shirika la Mafuta Tanzania (TPDC), kununua mafuta moja kwa moja kwenye mitambo yao ya kuzalisha mafuta (refineries) na hivyo kupunguza gharama zinazowekwa na wanunuzi wa kati.

2. Kubadilishana uzoefu na nchi hizi rafiki kuhusu uendeshaji wa sekta ya mafuta na gesi.

3. Kuimarisha mahusiano yaliyopo na kujenga ushirikiano mpya katika eneo la mafuta ili nchi yetu ipate jawabu la kudumu la kujihakikishia upatikanaji wa uhakika wa mafuta na kwa bei isiyopanda ghafla na kwa kiwango kikubwa.

Katika nchi zote hizo tatu, nilifanikiwa kukutana na kufanya mazungumzo na Mawaziri wenzangu wa Nishati, viongozi wengine waandamizi na wakuu wa mashirika ya mafuta ya taifa ya nchi hizo.

Kutokana na heshima ya nchi yetu na Rais wetu, na urafiki wa nchi yetu na nchi hizi, nilipokelewa vizuri na viongozi wote katika nchi zote hizi na walipokea na kukubali hoja na haja ya mashirikiano katika sekta hii ya mafuta. Kwa kifupi, yale yote ambayo nchi yetu iliyapendekeza kwenye nchi hizi yamekubalika.

Baadhi ya mafanikio ya ziara hiyo ni kama ifuatavyo:

1. Serikali yetu imekubaliana na Serikali za nchi hizo na makampuni yao ya Taifa ya mafuta kushirikiana katika masuala ya mafuta na gesi. Katika miezi ijayo, baada ya taratibu za kiserikali na kisheria kukamilika, makubaliano hayo yenye maslahi kwa nchi yetu yatatangazwa.

2. Kwa mara ya kwanza, ile azma ya miaka mingi ya Serikali, kununua shehena ya mafuta moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji sasa imetimia. Hata kabla ya mwisho wa safari yetu, mnamo tarehe 28 Oktoba 2021, tuliiwezesha TPDC kushiriki zabuni ya kiushindani na makampuni mengine ya kimataifa ambayo kila mwezi hushiriki zabuni ya kuleta mafuta nchini. TPDC imefanikiwa kushinda sehemu kubwa ya zabuni hiyo kwa kutoa bei ndogo zaidi ya kuagiza mafuta ya dizeli nchini kwa mwezi wa Disemba mwaka huu. Hali hii itapunguza makali ya bei ya mafuta ya dizeli kwa mwezi Disemba. Kudhihirisha kwamba hatua hii ina manufaa, kwa mfano, mwezi Agosti 2021, wakati bei ya mafuta ghafi duniani ilikuwa dola 73 kwa pipa, kampuni iliyoshinda zabuni ya kuleta mafuta ya dizeli nchini ilituuzia kwa dola 30 kwa tani za ujazo (premium). Safari hii, pamoja na bei ya mafuta ghafi duniani kupanda na kufikia dola 86 kwa pipa, TPDC italeta dizeli nchini mwezi Disemba kwa wastani wa dola 20 kwa tani za ujazo.

3. Tumefanikiwa kushawishi nchi rafiki tulizotembelea kushirikiana na nchi yetu kujenga kituo kikubwa cha upokeaji na uhifadhi mkubwa wa mafuta (fuel terminal) kwa ajili ya soko la ndani ya nchi yetu lakini kwa mahitaji ya nchi za Afrika Mashariki na Kati na nyingine za mbali pale itakapohitajika. Kituo hiki kitatuhakikishia kuwa na kiasi cha kutosha cha mafuta ndani ya nchi wakati wote. Kwa sasa, iwapo kutatokea dharura huko duniani na tukashindwa kuagiza mafuta, kiasi cha mafuta yaliyopo nchini yanatutosheleza kwa wastani wa siku 15 tu. Mazungumzo kuhusu taratibu za kuanzisha kituo hiki yataanza mwezi wa Novemba.

4. Baada ya wiki mbili kuanzia sasa, kutakuwa na ziara za viongozi na watalaam kutoka katika nchi tulizotembelea kuja Tanzania kwa ajili ya kukamilisha taratibu za utekelezaji wa makubaliano yetu kwenye maeneo tuliyokubaliana kushirikiana. Wizara ya Nishati itaendelea kuratibu na kufuatilia ili kuhakikisha

kwamba mafanikio yaliyopatikana kwenye ziara hii yanadumu na makubaliano na nchi hizi rafiki yanatekelezwa kwa maslahi mapana ya nchi yetu na watu wake.

Wakati huo huo, katika kuendelea kurekebisha sekta ndogo ya mafuta, Serikali itatekeleza yafuatayo:-

1. Kama hatua ya muda mfupi, kuiimarisha TPDC kwa kuiruhusu haraka kuajiri watumishi weledi na wajuzi wa biashara ya mafuta ili iendelee kununua mafuta kwa niaba ya Serikali kwa ufanisi zaidi.

2. Kama hatua ya muda wa kati, lakini yenye jawabu la muda mrefu, Serikali itaanzisha Hifadhi ya Kimkakati ya Mafuta (Strategic Petroleum Reserve) ili kuwa na akiba kubwa ya mafuta wakati wote kwa ajili ya dharura na pale bei duniani itakapopanda kwa kiwango kikubwa.

3. Kupitia mfumo wa uagizaji wa mafuta wa pamoja (Bulk Procurement System) ili kubaini mapungufu na kuboresha kwa maslahi mapana ya Taifa.

4. Kufanya tathmini ya utendaji na watumishi wa taasisi zote za Serikali zinazohusika na biashara ya mafuta ikiwemo TPDC, EWURA na Wakala wa Uagizaji wa Mafuta wa Pamoja (PBPA) ili kuhakikisha kwamba taasisi hizi na watumishi wake wote wanatimiza wajibu wao kwa weledi na uadilifu na kwa maslahi ya nchi.

5. Kuendelea na utekelezaji wa maelekezo ya Mheshimiwa Rais ikiwemo kuendelea kupitia tozo na kodi mbalimbali zinazochangia kuongezeka kwa bei ya mafuta nchini.

6. Kuendelea kushirikiana kwa karibu na wadau wa biashara ya mafuta nchini, ikiwemo TAOMAC na TAPSOA, na kuweka mazingira mazuri ya biashara ya mafuta nchini kwa sekta binafsi kuendelea kushiriki ili kuwe na ushindani wa haki na wa uwazi kwa manufaa ya watumiaji mafuta na nchi kwa jumla. Serikali itaongeza ufuatiliaji wa karibu zaidi kwenye sekta ya mafuta kwa kutumia vyombo na mamlaka mbalimbali ili kubaini na kudhibiti hujuma na udanganyifu katika biashara ya mafuta na kuweka adhabu kali zaidi, ikiwemo kunyang’anywa leseni, pale itakapobainika hivyo.

7. Kurekebisha miundombinu ya upokeaji na uhifadhi wa mafuta nchini, hasa kwenye bandari zetu ili kuhakikisha kwamba kuna ufanisi zaidi.

8. Kuendelea kuyafanyia kazi na kutekeleza mapendekezo ya tume iliyoundwa na Mheshimiwa Waziri Mkuu kuhusu biashara ya mafuta nchini.

HITIMISHO

Bei ya mafuta nchini kwa kiasi kikubwa inachangiwa na bei za mafuta duniani, ambazo Serikali ina nafasi ndogo kwenye kuzidhibiti. Hata hivyo, Serikali itaendelea kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha kwamba yale yaliyo ndani ya uwezo wa Serikali katika kudhibiti bei ya mafuta tunayafanyia kazi.

January Makamba (Mb.)

Waziri wa Nishati

31 Oktoba 2021

View attachment 1993488

Tatizo kubwa la bei ya mafuta nchini ni kodi na tozo mbalimbali.

Kwani hata tozo za stika za usalama barabarani nazo kama yalivyo mafaini yasiyokuwa na kichwa wala miguu barabarani si nayo ni gharama na kero zaidi kwa wenye magari?
 
Mtu anachungulia 2030 Kwa uchu jalafu unampa dili la kunegotiate si ndo Yale ya pesa za gadaffi
 
MI NAFIKIRI TURUHUSIWE KUAGIZA MAFUTA KILA MTU KAMA AMBAVYO TUNAAGIZA BIDHAA NYINGINE.MFANO UNAAGIZA ZAKO TANI 100,UNATUMIA ZIKIISHA UNAAGIZA TENA ARABUNI
 
Hivi katika akili ya kawaida tu na nyepesi, hao waliotangulia wote hawakuona hiyo solution?!

Hapa kuna mchezo tunachezewa mchana kweupe. Ni swala la muda tu tutajua shida imejificha wapi.
Nguvu ya pesa baba. Hata hii Januari ajipange sana
 
Siasa tu hizi....kama ingewezekana JPM asingeacha kutekeleza hili kwa sababu alikuwaga na bifu na madalali. Sasa Makamba marafiki zake na mabosi wake wa zamani ndo wenye filling stations ataanzia wapi kuwageuka?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] hili nalo ni neno tena zito sana. Nimewaambia haya maneno pia kuwa magu hii kitu angeweza ifanya overnight kama ingekuwa ni possible.
 
Kwanini Kabla hawakufanya hivyo ?

What are the Pros and Cons

Don't get me wrong binafsi nadhani this is the best solution..., ila nashangaa common sense haiku-prevail hapo kabla; cha muhimu tununue kabla ila sio exclusive deals hawa madalali kama wakija na bei ya chini basi tuchukue kwao pia
 
Bei ya mafuta inaongezwa na serikali yenyewe kwa kuongeza tozo na kodi kwa watoa huduma na pia tozo nyingi zaidi ya 21 kwa kila taasisi ya seriakli kwenye mafuta.... hizo tozo zikiondolewa hata wasinge agiza wenyewe bado mafuta yatashuka.....

Uzuri bei ya mafuta duniani iko wazi kabisa na mafuta yasingepanda kama serikali isingeliongeza mzigo wa kodi na pia kama kweli serikali inataka kushusha bei ya mafuta iondoe hizo tozo zaidi ya 21 kwenye mafuta .....

Mafuta hata wakiacha hao hao wanao agiza waagize bado mafuta yanweza kushuka kama wataondoa mlolongo wa kodi......kuwepo na dhamira ya kweli ya kushusha bei ya mafuta kwa kuanza kuondoa makodi na matozo story za kuagiza wenyewe.

Serikali isijiingize kwenye biashara halafu baadae tuje tuambiwe story nyingine... oooh mafuta yamepanda tulipokuwa tuna nunua oooh sijui nini oooh bei itaongezeka kidogo
 
Hahahahaha... .lakini ndiye aliyelazimisha TPDC kujenga filling stations kila mji ili baadaye ifanye biashara ya mafuta kwa niaba ya Serikali. Au umesahau?
Mnafiki huwa anajisahau kwasababu ili uwe muongo miaka yote inabidi uwe na kumbukumbu balaa jambo ambalo ni gumu sana.
 
Hongera sana
Ikimpendeza afikirie kufufua kiwanda cha kuchakata mafuta kilikuwaga Kigamboni enzi za Mwalimu Nyerere
Au pengine, aweke kingine Tanga ili tuchakate mafuta yakutokea Uganda.
Naamini technologia ya kuchakata mafuta sio kubwa sana hiyo bei itashuka sana ila pia tutapata Lami kama end products
Madalali uchwara ndio tatizo la hii inchi kusababisha mifumuko ya bei. Tutokomeze madalali uchwara tutasolve hii kitu.
 
Hakujawahi kuanzishwa kitu Tanzania halafu kikawa na muendelezo wenye tija.Tutakuja kusikia 'tunapigwa' tena kwenye hili.
 
Back
Top Bottom