Waziri Makamba ujue siyo kila kitu ni cha kubinafisisha

Waziri Makamba ujue siyo kila kitu ni cha kubinafisisha

mkuu Sijamsikia makamba akisema shirika libinafisishwe,wewe umetoa wapi hii taarifa
 
Unabinafisaji uendeshaji maana mswahili hawezi akaendesha kitu kwa ufanisi na ishu ya security inabakia kwenye serikali kwa national security.
Check tu mfano Tazara wameshindwa japo market ni kubwa na ya uhakika.
Anayebinafsishwa sharti asiwe mswahili ?
 
Turuhusu tuu watu/makampuni binafsi yazalishe na kusambaza umeme, soko huru kama makampuni ya simu, TANESCO shirika linaloishi kwa ruzuku na kuendeshwa kijima haliwezi kuhudumia watu milioni 70, sheria zetu za kuipa TANESCO monopoly ndio zinatuumiza, tubadilishe sheria matatizo ya umeme yataisha
 
Mfano wa Tazara sio kweli. Uliza kabla ya kupotosha wengine, kwa mfano, maamuzi ya uendeshaji wake yanafanyikaje ukizingatia ni mradi wa serikali mbili. Tukirejea kwa tanesco au mashirika mengine ya umma, yana mamlaka kiasi gani kufanya maamuzi kitaaluma bila kuingiliwa na wanasiasa. Yawezekana baadhi ya mashirika hayana uhuru huo kwa maana ya kila mara kukimbilia Wizarani kupata baraka wakati mwingine kutoka kwa maofisa wasiokiwa na taaluma/uzoefu stahiki.
Wanasiasa hawawezi chezea shirika binafsi
 
Waziri wa Nishati January Makamba ajulishwe kuwa kwenye taifa siyo kila kitu ni cha kubinafisishwa kwa masilahi mapana ya taifa.
  • Umeme
  • Bandari
  • Reli
  • Viwanja vya ndege
  • Mbuga etc
Baba wa taifa Mwl Nyerere kwenye hotuba yake moja mwaka 1995 alikemea vikali akili ya kuchukua mali ya uma na kuwakabidhi watu wachache, mfano umeme ndiyo injini ya uchumi wa nchi kwa kuvutia kujengwa kwa viwanda vingi na kuzalisha bidhaa za bei ndogo zitakazoshindana kwenye soko, kamwe hatuwezi kuwapa watu wachache watufanyie biashara kwa kutuuzia umeme alafu tukategemea bidhaa zetu zishindane kwenye soko la Dunia.

Enzi za Kikwete Tanesco nusura ibinafisishwe baada ya kuwa na madeni makubwa ya kulipia capacity charges kutoka kwenye generator za kampuni la symbion.

Alipoingia Magufuli akafuta baadhi ya mikataba ya hovyo na kuliwezesha shirika kukusanya zaidi ya trillion 2 kwa mwaka hivyo likaacha kujiendesha kwa kutegemea ruzuku ya serikali na kufuta mpango wa kulibinafisisha shirika hili la uma.

Ameingia rais Samia na alipomteua waziri January Makamba tayari ameingia na mentality ileile ya enzi za Kikwete.

1. Pamoja na kwamba Tanesco ya leo hawaagizi nguzo nje ya nchi kama walivyokuwaga wanafanya huko nyuma lakini bado Makamba anataka shirika libinafisishwe.

2. Pamoja na kwamba Tanesco ya leo wanakusanya zaidi ya trillion mbili kwa mwaka lakini bado waziri Makamba anataka shirika libinafisishwe!

3. Pamoja na kwamba kupitia REA Tanesco imetapakaa nchi nzima lakini bado waziri anataka shirika libinafisishwe.

4. Pamoja na kwamba sasa hivi Tanzania inajenga bwawa kubwa kabisa la kufua umeme lakini bado waziri anataka Tanesco ibinafisishwe.

Hii speed ya 4G ya Makamba kutaka Tanesco ibinafisishwe inasukumwa na nini? Hivi kwa akili hii vipi huyu Makamba angeshinda urais mwaka 2015?
Ubinafsishaji huongeza tija na ufanisi, wala hatuna haja ya kutia shaka kuhusu suala hilo.
 
Wapi alipotangaza anataka TANESCO ibinafsishwe? Au chuki zako tu.
Tangu lini wakitaka kubinafsisha hutangaza. Majanuary anataka kukaa mkao wa kula. Miaka yote ubinafsishaji umekuwa ndiyo njia pekee ya kuwapelekea wakubwa kuwa mamilionea/mabilionea/matirilionea. Majanuary anataka wahi, mkishtushtuka atakuwa tayari kafunga bao na kukimbilia USA.
 
Tangu lini wakitaka kubinafsisha hutangaza. Majanuary anataka kukaa mkao wa kula. Miaka yote ubinafsishaji umekuwa ndiyo njia pekee ya kuwapelekea wakubwa kuwa mamilionea/mabilionea/matirilionea. Majanuary anataka wahi, mkishtushtuka atakuwa tayari kafunga bao na kukimbilia USA.
Chuki zitakuua.
fanya kazi uwajengee maisha bora wanao ili nao wawe kama familia ya Makamba wasigeuke wapiga stori za vijiweni.
 
Chuki zitakuua.
fanya kazi uwajengee maisha bora wanao ili nao wawe kama familia ya Makamba wasigeuke wapiga stori za vijiweni.
Labda wewe, mimi kila kitu kwenye maisha yangu kiko sawa. Nina chakula cha kutosha, ninavaa vizuri, nina kibanda cha kulala na sina matamanio mengine, na pia sikufika nilipo kwa njia haramu. Kazi ya chaki ndiyo imenifikisha nilipo.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Chuki zitakuua.
fanya kazi uwajengee maisha bora wanao ili nao wawe kama familia ya Makamba wasigeuke wapiga stori za vijiweni.
Mkuu unafikili basi nao familia zao ziko njema kihivyo asilimia 100,nenda kakague miji yao wanayotokea barabara na nyumba zinazowazunguka ni mbovu kuliko mfano,watumishi wa uma huko wanakotoka wanatamani kuhama kila siku maana hakuna hata motisha.kifupi hawa viongozi wanasiasa vijana ni walafi wa mali ya uma na wakati huo huo wana choyo hata kwa maendeleo ya kaya zao.
Wanafisadi fedha za miradi alafu wanazikimbiza nje huko kwa wazungu wakifa ndio zimeishia huko huko.

Magu kawapa somo ndani ya miaka 6 kaacha alama kubwa kule Chato hakuna taasisi ya kiserikali imekaa kiholelaholela.
 
Waziri wa Nishati January Makamba ajulishwe kuwa kwenye taifa siyo kila kitu ni cha kubinafisishwa kwa masilahi mapana ya taifa.
  • Umeme
  • Bandari
  • Reli
  • Viwanja vya ndege
  • Mbuga etc
Baba wa taifa Mwl Nyerere kwenye hotuba yake moja mwaka 1995 alikemea vikali akili ya kuchukua mali ya uma na kuwakabidhi watu wachache, mfano umeme ndiyo injini ya uchumi wa nchi kwa kuvutia kujengwa kwa viwanda vingi na kuzalisha bidhaa za bei ndogo zitakazoshindana kwenye soko, kamwe hatuwezi kuwapa watu wachache watufanyie biashara kwa kutuuzia umeme alafu tukategemea bidhaa zetu zishindane kwenye soko la Dunia.

Enzi za Kikwete Tanesco nusura ibinafisishwe baada ya kuwa na madeni makubwa ya kulipia capacity charges kutoka kwenye generator za kampuni la symbion.

Alipoingia Magufuli akafuta baadhi ya mikataba ya hovyo na kuliwezesha shirika kukusanya zaidi ya trillion 2 kwa mwaka hivyo likaacha kujiendesha kwa kutegemea ruzuku ya serikali na kufuta mpango wa kulibinafisisha shirika hili la uma.

Ameingia rais Samia na alipomteua waziri January Makamba tayari ameingia na mentality ileile ya enzi za Kikwete.

1. Pamoja na kwamba Tanesco ya leo hawaagizi nguzo nje ya nchi kama walivyokuwaga wanafanya huko nyuma lakini bado Makamba anataka shirika libinafisishwe.

2. Pamoja na kwamba Tanesco ya leo wanakusanya zaidi ya trillion mbili kwa mwaka lakini bado waziri Makamba anataka shirika libinafisishwe!

3. Pamoja na kwamba kupitia REA Tanesco imetapakaa nchi nzima lakini bado waziri anataka shirika libinafisishwe.

4. Pamoja na kwamba sasa hivi Tanzania inajenga bwawa kubwa kabisa la kufua umeme lakini bado waziri anataka Tanesco ibinafisishwe.

Hii speed ya 4G ya Makamba kutaka Tanesco ibinafisishwe inasukumwa na nini? Hivi kwa akili hii vipi huyu Makamba angeshinda urais mwaka 2015?
Ivi waziri yupo siliazi au?
 
Ni lini ametamka kubinafsisha?

Na kama kweli anataka kubinafsisha ujue ndio anaanza kuiba pesa kwa kula rushwa za wawekezaji na kuingia mikataba ya kula pesa

Huyu na Nape Nnauye pamoja na Ridhiwani ni wa kuwa nao makini sana
 
Watu wamerukia kumshutumu JM bila hata kujiridhisha kuwa kayasema hayo mambo ya ubinafsishaji.

Mtoa mada athibitishe kwanza kuwa JM anataka kubinafsisha Tanesco la sivyo ni chuki binafsi.

Kwanza Tanesco haiwezi kubinafsishwa bila ridhaa ya rais, baraza la mawaziri na bunge. Tanesco ikibinafsishwa hao wote hawawezi kukimbia hilo jukumu.
 
Back
Top Bottom