The Good
Senior Member
- May 26, 2010
- 185
- 119
Utaratibu ni kwamba Wakati wa kuunda Bodi Waziri anapeleka majina yasiyopungua matatu kwa nafasi ya Mwenyekiti na Majina ya Wanaopendekezwa kuwa Wajumbe wa BodiHuyu mama Maajar ni miongoni mwa Waanzilishi/Wamiliki wa kampuni ya REX ATTORNEYS na hiyo kampuni ya uwakili ndiyo inayoiwakilisha Symbion na Dowans katika kesi zao dhidi ya TANESCO.
Halafu unatoka hapo unamteua huyo mtu kuwa mjumbe wa bodi ya TANESCO, huoni kuna mgongano wa Maslahi hapo?
Huoni huyo mama atakuwa anapata sensitive information ndani ya TANESCO ili kuwapa advantage wateja wake wanaomlipa mamilioni katika kesi dhidi ya hilo shirika?
Waziri Makamba, tengua haraka sana bodi uliyoiunda yenye mgongano wa masilahi.
1. Hatutaki kuona tena huduma za umeme zikizorota ili watu wauze majenereta yao
2. Hatutaki kuona hujuma kwenye mabwawa yetu ya umeme ili umeme uwe shida halafu nchi iingie kwenye mikafaba ya kifisadi kama IPTL
3. Hatutaki kuona time table ya kukamilika kwa Stieglers inachelewa ili wapiga dili wapate kisingizio cha kuingia mikataba ya kifisadi ya umeme
Waziri Makamba tunataka uchukue hatua, hili chaguo la Balozi Maajar hatulielewi!
Wote hao wanafanyiwa Vetting
Baada ya hapo Rais anateua mwenyekiti kutoka hao watatu au anakataa wote na kuteua anayeona anafaa
Majina ya Wajumbe yakipitishwa baada ya Vetting yanarudishwa kwa Waziri kuyatangaza pamoja na jina la Mwenyekiti aliyeteuliwa
So kama kuna tatizo lingeonekana wakati wa vetting
naomba kuwakilisha