Waziri Mchengerwa anena kuhusu watumishi wazuri

Waziri Mchengerwa anena kuhusu watumishi wazuri

zandrano

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2017
Posts
7,893
Reaction score
8,816
Waziri wa Utumishi wa Umma, Mhe. Mchengerwa amesema watumishi wengi wenye uwezo mzuri wa kiutendaji wana fanyiwa mizengwe na majungu ya kuharibiwa kazi, na mbaya zaidi mabosi wao wanakuwa ni sehemu ya kuwaharibia.

Waziri Mchengerwa amedhamiria kuondoa hali hiyo katika idara zote za Serikali ameeleza kuwa tatizo hilo limekuwa ni kama kansa ktk utumishi wa umma.

Kwa maneno hayo ya Mhe. Waziri inaonekana kuna tatizo kubwa sana tena sana. Viongozi wa juu yaani mabosi wana waonea sana watumishi wa chini, ukionekana mwerevu tu unapigwa nyundo ya kichwa. Kuna baadhi ya watendaji wenye dhamana wanajiona wao ni miungu watu

Ushauri:
kama kweli Waziri Mchengerwa amedhamiria kuwafuta machozi wanao nyanyaswa basi aunde tume maalumu itakayo fuatilia kero za watumishi ktk kila idara za Serikali nchi nzima.

Uchunguzi ufanyike kila idara, kuna uonevu mkubwa sana, watu wanaonewa na viongozi wao bila sababu za msingi, watu wanalia hakuna wa kuwasikia.

wapo watumishi wa umma wanatamani hata kuacha kazi kutokana na uonevu wanao fanyiwa na viongozi wao wa juu, wanachafuliwa kwa maksudi ili wasisonge mbele.
Hali hii ni hatari sana endapo itaachiliwa iendelee, lazima jambo lifanyike;
kwanza kubaini matatizo hayo ktk Idara zote za Serikali, lkn pia kuwaondoa viongozi watendaji ambao wamekuwa na tabia za uonevu kwa walio chini.

 
Legacy ya Lisu kwa watanzania ni ipi?

Ni kuolewa na Amsterdam watanzania wamepata shemeji wa kibelgiji
 
Wasiojulikana wenyewe Wana mauza uza kwao wanalia na kusaga meno acha viumane ila Hawa watu wenye dhamana Wana mambo ya king...ese Sana wanajihisi wamezaliwa kuwa viongozi.

Maish yenyewe mafupi watu roho mbaya mamaeee
 
Kwa sisi wa taasisi na kampuni binafsi tunaofanya kazi na serikali karibu kwenye kila nyanja huwa tunabaki na mshangao namna utendaji kazi unavyofanywa isee ukweli mchungu sisi Watz bado Sana.

Hasa tamisemi ni ovyo isee yaani kazi ya kupata mrejesho wa Jambo Fulani swala la dakika 5 unaweza poteza siku zima yaani wanaingia huku wanatokea kule.

Kiukweli kama tunataka kufika mbali kama nchi ni lazima kila mfanyakazi kwa nafasi yake awajibike na afanye kazi kwa weredi ni aibu Sana umekabidhiwa kitengo then unawafelisha raia kupata huduma Yani wewe ndio unakuwa chanzo.
 
Hataweza kulimaliza Hilo tatizo hao watu wanalindana mno Hilo asahau kulimaliza labda aweke wapelelezi wasiojulikana ndo atalipunguza
Akiamua na akajipanga vyema hili tatizo la viongozi kuwaonea walio chini litakwisha.

Hili ni tatizo kubwa sana, watu wana umizwa sana tena wanao waumiza ni viongozi wao wakubwa! sasa wakasemee wapi?! waendelee kunyanyaswa na kuumizwa?

Waziri peke yake hawezi kulimaliza hili tatizo, lazima asaidiwe na watu wenye nia njema na ya ukweli kama yake, vinginevyo kuna dhambi kubwa sana inatendwa ndani ya watumishi na viongozi wenye dhamana.
 
Kwa sisi wa taasisi na kampuni binafsi tunaofanya kazi na serikali karibu kwenye kila nyanja huwa tunabaki na mshangao namna utendaji kazi unavyofanywa isee ukweli mchungu sisi Watz bado Sana...
Hayo yote yanasababishwa na ROHO mbaya. Nadhani ofisi za watumishi wa umma ndio zinaongoza kwa kupigana majungu na kuharibiana kazi, yaani mkubwa anamharibia wa chini ili asipande.
 
Asee hii nchi ukiwa smart huwezi kufanya kazi serikalini.

Ujajikuta wewe ni tatizo ambapo watu wenye kazi yao watafanya juu chini ili uondoke
Yaani kila idara ni vurugu mechi, halafu cha kushangaza wakubwa wapo lkn sifahamu huwa hawajui au wanawaogopa watendaji?
kuna uonevu mkubwa sana unafanywa na viongozi watendaji ktk Idara za Serikali.

Lazima ifahamike kuwa Ofisi za umma ni za wananchi sio Mali ya watendaji walio pewa dhamana, sasa kwa nini Ujifanye ni mali yako kuwanyanyasa wengine?

tena cha kushangaza unakuta taasisi zingine ni za kutoa haki lkn ndio zinaongoza kuonea watumishi wake.
 
Hataweza kulimaliza Hilo tatizo hao watu wanalindana mno Hilo asahau kulimaliza labda aweke wapelelezi wasiojulikana ndo atalipunguza
sisi waandishi wa Habari tunaweza kumsaidia Mhe. Waziri kufichua uonevu unao fanywa na viongozi watendaji dhidi ya watumishi wa chini.
uonevu ni mkubwa sana.

Mfano;
kuna mtumishi wa umma alikuwa ni mgonjwa amepewa Rufaa kuwa kuwa karibu na hospitali kubwa aliomba ajihamishe kufuata matibabu na alikuwa na nyaraka zote muhimu lakini alizunguswa weee...hatimaye akafa na wakamsafirisha.

nilisikitika sana nilijiuliza hivi kweli kama viongozi wanashindwa kuthamini UHAI wa mtumishi wao, je kweli wanaweza kuwatendea watu wengine haki?

Uonevu wa aina hiyo upo sana ktk ofisi za umma.
 
Huyu waziri anania njema sana, lakin kuna mambo yatambana, mojawapo bajeti.

Lakin bado anao uwezo wa kufanya yale yaliyokuwa ndani ya uwezo wake.

1. Kupamdisha watumishi vyei
2. Kulipa watumishi walio kaimu kwa muda mrefu bila kuthibitishwa.
3. Kurudisha kazini watumishi walio achishwa kazi bila taratibu za kiutumishi. etc etc
 
Ni ukweli usio fichika kuwa kuna tatizo kubwa la watumishi wazuri kiutendaji kuonewa na viongozi wao wa juu, uonevu ni mkubwa sana, watu wana umizwa sana, kuna viongozi miungu watu KAZI yao ni kuwa vunja moyo watendjibwazuri.

Kuna uonevu na fitina kubwa kati ya viongozi wenye dhmana na watumishi wa kawaida, kuna Majungu na fitina hatari!

Aanze na Mhimili wa Mahakama.
 
sisi waandishi wa Habari tunaweza kumsaidia Mhe. Waziri kufichua uonevu unao fanywa na viongozi watendaji dhidi ya watumishi wa chini.
uonevu ni mkubwa sana...
Duh!

Yaani mtumishi ana nyimwa haki yake ya kujihamisha Kwa ajili ya ugonjwa na akiwa na nyaraka zote ZA kitabibu! Hadi ana kufa! Aisee hao sio binaadamu ni zaidi ya wanyama, na wanapaswa walaaniwe na ikiwezekena washitakiwe.

Mambo kama haya yasifumbiwe macho, huu ni unyanyasaji wa kiwango CHA juu.
 
Mchengerwa umesema ukweli mpaka umepitiliza. Viongozi serikalini àmbao wengi ni wanaCCM wamekalia majungu na roho mbaya Kwa watumishi Wenye uwezo na tija. Wakiona wamewashindwa wanawachomekea kuwa ni wànachama wa CHADEMA.
 
Ni ukweli usio fichika kuwa kuna tatizo kubwa la watumishi wazuri kiutendaji kuonewa na viongozi wao wa juu, uonevu ni mkubwa sana, watu wana umizwa sana, kuna viongozi miungu watu KAZI yao ni kuwa vunja moyo watendjibwazur...
kinachotakiwa ni kuvunja ukimya na kusem ukweli kama kuna uonevu au ukandamizwaji uripotiwe ili hatua stahiki zichukuliwe.
 
Ni jambo la kushukuru angalau Kwa mara ya kwanza WAZIRI Mwenye dhamana amebaini hilo tatizo la kupigwa nyundo watumishi wasio na godfather.

Angalau matumaini Kwa wanyonge yanaonekana.

Pongezi nyingi Kwa MHE WAZIRI Mungu azidi kumpa maarifa Na akili nyingi ZA kupambana Na waovu bila woga
 
Back
Top Bottom