Waziri Mchengerwa kwa hili la Mpira miguu unazidi kumpoteza "Rais" katika ramani zake

Waziri Mchengerwa kwa hili la Mpira miguu unazidi kumpoteza "Rais" katika ramani zake

kasenene

JF-Expert Member
Joined
Jun 6, 2008
Posts
1,632
Reaction score
2,413
Tumekusikia jana ukitoa maelekezo ya kutosha Baraza la michezo jinsi Wizara yako mnavyotaka isimamie mpira wa miguu “as if” Baraza la Michezo kazi yake ni kusimamia mpira wa miguu tu na huku ukijisahau kuwa wewe sio Waziri wa mpira wa miguu peke yake. Okay tuliacahe hilo.

Tumesikia maoni ya wizara yako (sijui ni yako binafsi) kuhusu suala zima la Waamuzi wa mpira wa miguu na mapendekezo uliyoyatoa ikiwemo kuwashirikisha TAKUKURU katika semina za uwezeshaji waamuzi !!? Kweli Takukuru Mchengerwa!!

Haya hili tuliache, huku ukielewa kuwa bajeti ya wizara yako ni ndogo karibia kuliko wizara zoote unakuja na wazo la VAR na kwamba kama wizara mna mpango wa kuagiza VAR kwa ajili ya viwanja vitano (5) tu kwa kuanzia. Kweli Waziri umefikiria saana hili au umedanganywa na akili za yule Waziri mwenzako “mpigaji” ambaye lazima VAR moja aagize ifungwe Singida!

Ahaa... Kweli Mchengerwa najua umecheza mpira wa miguu na unamiliki timu kama alivyo huyo waziri mwenzako anayekupotosha. Kweli tatizo la soka letu Bongo ni waaamuzi? Umeangalia viwanja vyetu, vipi posho na maslahi ya wasimamizi wa mpira wa miguu!!

Camera zenyewe za kurekodi mechi zinatosha, vipi kuhusu taa? au Unajua gharama ya VAR moja. Hapa Africa ni Morocco peke yake wameweza kutumia VAR wewe fikiria hata Champions League Africa imetumika kwenye mechi moja tu ya Fainali mwaka jana.

Vile vile elewa unapoamua kuzungumzia michezo hapa nchini hiyo ni agenda kubwa saana lakini kikubwa sote tunaelewa katika nchi maskini kama zetu tuna vipaumbele vingi saana kuliko michezo na ndio maana wizara yako inakuwa haipewi kipaumbele saana kama wizara nyingine.

Kama unataka kusaidia michezo na kuna pesa kidogo wekeza kwenye michezo iliyosahaulika na sio mpira wa miguu. Mpira wa miguu ni wa mwisho kwani umeshasimama saana kulinganisha na michezo kama kuogelea, kuruka juu na chini n.k….vipi UMITASHUMITA ipo kweli!!

Ushauri wangu Bwana mdogo Waziri:

Ukitaka mama asizidi kukupoteza pamoja na ukaribu mlio nao angalia na tafakari juu ya huu msemo. Akili kuambiwa changanya na yako...JMK
 
Waziri hata hajui mambo ya mpira msimamizi wake mkuu ni FIFA, anataka kujichanganya kwa kujazwa upepo wa kishabiki na Mwigulu halafu Tqnzania ije kufungiwa na FIFA ndio hawa vilaza watapata akili.
 
Unadhani angekuwa na Akili and that Competent angehamishwa kutoka ile Docket Muhimu na Kutupwa huku katika Michezo?

Hiyo ni Demotion ya hali ya Juu sema wengi wenu hamjajua na amesalimika kwakuwa tu ndiyo Sabuni ya Furaha na Upendo ( hasa Kibaiolojia ) kwa Mtoto wa Mama wa Kikatiba Tanzania.
 
Wajingansana nyinyi. Naona mmetoka shimoni huko mnapiga kelele hamtaki tatizo la waamuzi kutatuliwa. Mnataka liendelee kuwepo ili litimu lenu bovu liendelee kunufaika mkijificha kwenye kichaka cha matatizo makubwa ya mpira.

Aliewaambia kua suala la waamuzi ni tatizo dogo nani? Tatizo ili liwe kubwa linapaswa kuaje?

Imeuma eeh. Basi na bado, mtanyooka mwaka huu. Hakuna mchongo wala chupli chupli.
 
Wajingansana nyinyi. Naona mmetoka shimoni huko mnapiga kelele hamtaki tatizo la waamuzi kutatuliwa. Mnataka liendelee kuwepo ili litimu lenu bovu liendelee kunufaika mkijificha kwenye kichaka cha matatizo makubwa ya mpira.

Aliewaambia kua suala la waamuzi ni tatizo dogo nani? Tatizo ili liwe kubwa linapaswa kuaje?

Imeuma eeh. Basi na bado, mtanyooka mwaka huu. Hakuna mchongo wala chupli chupli.
Duuh kaka umesoma mara mbili mbili kabla ya kijibu? aisee..ebu rudia tena kusoma bila kuleta Uyanga na Usimba tafadhali....
 
Sio utaratibu wa FIFA
Kwenye swala la VAR ni mbali sana, kungekuwa tu na ka TV kamoja kalichounganishwa na Azam TV ili muamuzi awe anaangalia marudio akiwa uwanjani Kama tunavyoangalia sisi tukiwa bandani .
 
Hahahaaaaa wateule wakweeeeeeeeeeeeeeeee, hata kama kilaza nchi hii unaweza kuwa kiongozi yoyote tu ilimradi unamfahamu mtu huko juu
 
Ukiona jambo linashikiwa bango basi juwa kuna 10 %

Ova
 
Ukiona jambo linashikiwa bango basi juwa kuna 10 %

Ova
VAR ni gharama, ligi nyingi hata Europe wameshindwa kuweka.
Ni bora hiyo pesa wangejenga na kuboresha viwanja kuwa vya kisasa.
Viwanja vingi pitch ni mbaya sana, waboreshe hapo kwanza
Pia VAR haiondoi sana makosa ya refa, maana tumeshuhudia pia sehemu nyingi pamoja na kuwa na VAR Ila bado marefa walikosea
 
kuweka VAR sio wazo baya lakni pia sio tatiz l kimsingi kwnye soka l Nchi ,tusiwaze kunnua kitanda wkt godor l kulalia ha2na bdo..
 
Kwenye swala la VAR ni mbali sana, kungekuwa tu na ka TV kamoja kalichounganishwa na Azam TV ili muamuzi awe anaangalia marudio akiwa uwanjani Kama tunavyoangalia sisi tukiwa bandani .
Hata hii itawezekana...inakuwa ni TV ambayo kuna watu hata wanne nao wanaangalia pamoja na muamuzi; wanaweza kurudiarudia kadri wanavyotaka....kisha wanamwachia muamuzi atoe maamuzi. Kwa hiyo muamuzi anatoa maamuzi huku akijua kuwa kuna watu wameona lile tukio pia.
 
Nikiona kiongozi wa kibongo anakomalia jambo ambalo uchumi na mazingira haviruhusu namkumbuka Mramba.
Aliwahi sema marehemu B. Mramba "...hata watanzania wale nyasi, ndege ya raisi itanunuliwa"
 
Kurekebisha pitch tu tumeshindwa hiyo VAR tutaweza kweli!
 
Back
Top Bottom