Waziri Mkenda hawa walimu walikosea nini hadi wapewe hii adhabu ya kuporwa madawati ya kukalia?

Waziri Mkenda hawa walimu walikosea nini hadi wapewe hii adhabu ya kuporwa madawati ya kukalia?

Hao,wametaka waonekane.
Wanapenda kulialia&kutaka public sympathy.
Sijui ni kwa nini hawajipendi,hivi kweli hata furnitures tu wanashindwa kutengeneza kupitia fedha za elimu bure?
Maafisa wazima na elimu zao,wanafurahia kukalia madawati ya wanafunzi?
Aah...ni ajabu.
Kwani ni jukumu lao kujitengenezea furniture za kukalia…?
 
Ila hii Nchi hatujaliani sana ...

Yaani wote ni Watumishi wa Serikali, Tena unaweza Kuta mmesoma wote Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ila mmoja Mwalimu mwingine ni Mwanasheria.

Mmoja anaajiriwa Wizara ya Fedha kama Mwanasheria ila mwingine anaajiriwa kuwa Mwalimu.

Huyu mwingine anakuta ofisini kwake Kuna Meza na Kiti kizuri cha Kuzunguka pamoja na Chai ya Ofisini

Huyu Mwingine anaingia Darasani ambapo hakuna Kiti Wala Meza

It's unfair Wakuu

Hebu Viongozi waangalie hili suala
Ndo maana wengi wanakimbia ualimu.
 
Ndo maana wengi wanakimbia ualimu.
Kabisa, huwezi kufanya kazi kwenye mazingira hayo na ukafurahia kazi Yako

Hii Nchi imetoa MaRais 3 wakiwa na Taaluma ya Ualimu

Mwl. Nyerere
Mwl. Mwinyi
Mwl. Magufuli

Lakini hakuna aliyeweza kuwakumbuka Walimu wenzao hata kidogo zaidi ya kupeana ahadi fake...

Bora sisi Wahandisi tukikutana ERB day ni mwendo wa kupeana madeal na connection pamoja na kunywa Cocktails pamoja

Waiter tuletee kama tulivyo bill juu yangu 🤗
 
Kwanza kukubali kua mwl kwa nchi Kama tz ni ujinga mkubwa sana. Acha wanyanyaswe tu walimu wengi ni wajinga na hawana umoja kabsa. Wanajikutaga wamesona sna wakisimama mbele ya watoto na chaki zao kumbe ni hopeless kabsa. Bora niuze duka la mangi kuliko ualimu. Kwanza ukiwa mwl maisha yanakua magumu familia kuilisha nyama tu kilo moja mpaka mwisho wa mwezi siku zinazofata ni dagaa na maharagwe kazi gani hii. Mwl anavaa nguo za buku jero jero karume na mkanda wa kitambaa Kama utambi wa taa. Wakipata hela wanaenda kutamba kwenye mabanda ya gongo na libeneke baa wanapaogopa hatari
 
Naomba niwape uhalisia wa hili jambo japo kwa uchache tu, mwaka jana kikao kilikaa na mwalimu mkuu wa hiyo shule alihudhuria hicho kikao. Na baaada ya kikao mwalimu mkuu alikabiziwa pesa taslimu milioni moja na chenchi, na alitoa ahadi hadi kufikia mwezi wa 12 mwaka jana viti na meza kwajili ya walimu wa shule yake vitakuwa vipo tayari.

Ila kwa maelezo ya mtendaji, yeye alisema alimpigia simu mwalimu mkuu wa hiyo shule kuulizia zoezi hilo limefikia wapi na ilikuwa mwezi wa 12 kwenye tarehe 24. Mwalimu akajibu vipo katki hatuwa ya mwisho hadi kufikia januari shule kufunguliwa kilakitu kitakuwa sawa.

Mtendaji alienda asubuhi wiki hii akiwa na mgambo kama moja ya majukumu yake kukaguwa hali ya hapo shuleni ili ajionee mwenyewe, ila kilicho msikitisha alikuta madawati ya wanafunzi ndio walimu wamekalia ofisini, na mwalimu mkuu hakumkuta hapo shuleni😡....

Anyway mimi namuunga mkono mtendaji kwa hatua aliyochukuwa.

°Kama pesa ilitoka na akapewa mwalimu mkuu, na hakuna kilicho fanyika, hiyo pesa aliipeleka wapi?

°Je kati ya mwalimu na mwanafunzi, ni nani anatakiwa kutumia madawati?


(Hiyo ni shule ya msingi na kuna wanafunzi wanakaa chini ila madawati yamerundikana staff room et walimu ndio watumie)
 
Ila sometime walimu wapo na ujinga mwingi jukumu la kusimamia shule sio la mtendaji wao wanakubali vipi kupokonywa viti hivi huyo mtendaji anaweza kwenda zahanati akapokonya vitanda kuna mazingira ya kudhalauliwa wameyatengeneza hapo, ndio maana Majaliwa aliwachapa viboko nadhani angenikuta Mimi Sasa hivi angekuwa waziri mkuu mwenye jicho moja.
 
Ila sometime walimu wapo na ujinga mwingi jukumu la kusimamia shule sio la mtendaji wao wanakubali vipi kupokonywa viti hivi huyo mtendaji anaweza kwenda zahanati akapokonya vitanda kuna mazingira ya kudhalauliwa wameyatengeneza hapo, ndio maana Majaliwa aliwachapa viboko nadhani angenikuta Mimi Sasa hivi angekuwa waziri mkuu mwenye jicho moja.
Majaliwa yupi? PM?

Kassim hajawahi kufanya huo upuuzi.

Yeye mwenyewe, nafikiri, kitaaluma ni Mwalimu.
 
Back
Top Bottom