Tatizo watumishi wengi wa serikali/umma hawafanyi kazi kwa kufuata taratibu/miongozo ya kazi zao, bali hufuata matakwa ya wanasiasa (wenye maslahi binafsi). Ndio maana hata kwenye kesi ya Mbowe ulikuwa unasikia afisa wa polisi anaulizwa kuhusu vifungu vya PGO ambayo ni muongozo wa utendaji wao wa kazi lakini anasema hajuiPPRA kazi yake kuu hasa ni nini naona haifanyi majukumu yake ipasavyo
Huyu haaminikiki, ndiye aliyetuficha wakati Magufuli amekwisha kufa akatudanganya eti alikuwa ofisini!! Ni mbwekaji mzuri lakini hana meno.Hivi alishwahi kumchukulia hatua yeyote hapa nchini? Kama maneno yake yangekuwa kweli. Leo ingekuwa inakaribia mwaka tangu trein ya mwendo kasi kuzinduliwa
Asante Waziri mkuuWaziri Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Godfred Mbanyi amkute katika ofisi za Bohari ya Dawa (MSD) Jumatatu saa nne asubuhi, baada ya kubaini madudu katika ununuzi wa vifaa vya matibabu.
Waziri Mkuu ametoa agizo hilo katika ufunguzi wa Wiki ya Ununuzi wa Umma jijini Arusha ambapo ametaja gharama kubwa iliyotumika kununua vifaa hivyo tofauti na bei halisi za soko, na hivyo kupoteza fedha nyingi za umma na kuwakosesha wananchi huduma kwani vifaa vilivyonunuliwa ni vichache.
Akizungumza na wataalamu wa ununuzi na ugavi, ametaja baadhi ya manunuzi hayo kama vile ununuzi wa seti moja ya vitenganishi kwa ajili ya awamu moja ya kusafisha damu kwa shilingi 65,000, lakini wakanunua kwa shilingi 189,000.
Aidha, MSD walitakiwa kununua mashine ndogo ya kipimo cha haemolojia ya mwili kwa shilingu milioni 5, lakini wakanunua kwa shilingi milioni 14,045,000.
Ametoa mfano mwingine ambao ni kipimo kikubwa cha haiemolojia ya mwili ambacho ni shilingi milioni 37, lakini MSD wamenunua kwa shilingi milioni 147.9, pia walitakiwa kununua mashine ya kuchakata maji kwa ajili ya kusafisha damu ambacho kinauzwa milioni 32 lakini wamekinunua kwa shilingi milioni 129.
"Kwanini hili linatokea? kwa maslahi ya nani?" amehoji Waziri Mkuu
Kutokana na PSPTB kuwa na jukumu la kuwachukulia hatua wataalamu wa ununuzi na ugavi wanaokiuka sheria, Waziri Mkuu Majaliwa ameiagiza kufika ofisi za MSD akisisiitiza kuwa serikali haiwezi kukubali hali hiyo kuendelea.
"Na mimi sitasita kwenda na Kamanda Sirro, na Kamanda Hamduni, ili washughulike na watu. Lazima tuanze na watu hawa wanaofanya kazi hii, wakae nje, hatua nyingine zifuate," amesisitiza Waziri Mkuu Majaliwa
Ameongeza kuwa pengine wasimamizi wa vitengo vya ununuzi na ugavi wanahitaji kuapishwa, kutokana na unyeti wa nafasi zao katika kutoa huduma kwa Watanzania.
Uzuri mmepewa bunge na Kila kitu kwanini msipeleke hoja ya dharura na maazimio yachukuliwe kushughulikia wizi as per report ya CAG??Enzi zimeshapita, mkwara kama huu wakati wa JPM tayari watu wangeshakimbia nchi. Lakini huyu wa kukunwa vizuri na kupapasa ndo wamekula kwa urefu wa kamba zao.
Eti wahalifu wamsubiri aende na siro na hamduni utafikiri huko hakuna polisi wa kuwaweka ndani.
Acha aupige mwingi.
January oyeee
Nape oyeee
Riz1 oyeee
Mama wa mafao ya wake za viongozi oyeee
Haya majizi msubirini katelefone anakuja na siro na hamduni.
Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
majaliwa simkubali ni mwongo sana hata magu kipndi anaumwa aliwadanganya uma wa watanzaniaUpo sahihi hapa hakuna mtu kabisa
Kwa kweli !!!Uwiz ndiyo jadi yetu
Ova
Hafai kuwa kiongozi hata kidogomajaliwa simkubali ni mwongo sana hata magu kipndi anaumwa aliwadanganya uma wa watanzania
Ni kweli na ukifanikiwa kuiba mimali mingi unasifiwa kwa kuitwa mjanja wa mjini !!! Tuko vizuri sana !! Au siyo ??Uwiz ndiyo jadi yetu
Ova
Mjeshi ametolewaKwani hapo MSD si palikuwa panaongozwa na mjeshi?wabongo noma sana hawakuogopa hata zile gwanda
Ccm ni mafiii tunataka rais FULL DICTATOR MZALENDOWaziri Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Godfred Mbanyi amkute katika ofisi za Bohari ya Dawa (MSD) Jumatatu saa nne asubuhi, baada ya kubaini madudu katika ununuzi wa vifaa vya matibabu.
Waziri Mkuu ametoa agizo hilo katika ufunguzi wa Wiki ya Ununuzi wa Umma jijini Arusha ambapo ametaja gharama kubwa iliyotumika kununua vifaa hivyo tofauti na bei halisi za soko, na hivyo kupoteza fedha nyingi za umma na kuwakosesha wananchi huduma kwani vifaa vilivyonunuliwa ni vichache.
Akizungumza na wataalamu wa ununuzi na ugavi, ametaja baadhi ya manunuzi hayo kama vile ununuzi wa seti moja ya vitenganishi kwa ajili ya awamu moja ya kusafisha damu kwa shilingi 65,000, lakini wakanunua kwa shilingi 189,000.
Aidha, MSD walitakiwa kununua mashine ndogo ya kipimo cha haemolojia ya mwili kwa shilingu milioni 5, lakini wakanunua kwa shilingi milioni 14,045,000.
Ametoa mfano mwingine ambao ni kipimo kikubwa cha haiemolojia ya mwili ambacho ni shilingi milioni 37, lakini MSD wamenunua kwa shilingi milioni 147.9, pia walitakiwa kununua mashine ya kuchakata maji kwa ajili ya kusafisha damu ambacho kinauzwa milioni 32 lakini wamekinunua kwa shilingi milioni 129.
"Kwanini hili linatokea? kwa maslahi ya nani?" amehoji Waziri Mkuu
Kutokana na PSPTB kuwa na jukumu la kuwachukulia hatua wataalamu wa ununuzi na ugavi wanaokiuka sheria, Waziri Mkuu Majaliwa ameiagiza kufika ofisi za MSD akisisiitiza kuwa serikali haiwezi kukubali hali hiyo kuendelea.
"Na mimi sitasita kwenda na Kamanda Sirro, na Kamanda Hamduni, ili washughulike na watu. Lazima tuanze na watu hawa wanaofanya kazi hii, wakae nje, hatua nyingine zifuate," amesisitiza Waziri Mkuu Majaliwa
Ameongeza kuwa pengine wasimamizi wa vitengo vya ununuzi na ugavi wanahitaji kuapishwa, kutokana na unyeti wa nafasi zao katika kutoa huduma kwa Watanzania.
Anabweka tu kama mbwa koko, hivi anayajua mamlaka yake kweli?Upo sahihi hapa hakuna mtu kabisa
Pascal MayallaPPRA kazi yake kuu hasa ni nini naona haifanyi majukumu yake ipasavyo
NikuongezeeHivi alishwahi kumchukulia hatua yeyote hapa nchini? Kama maneno yake yangekuwa kweli. Leo ingekuwa inakaribia mwaka tangu trein ya mwendo kasi kuzinduliwa