Waziri Mkuu awataka Wananchi kujilinda na Magonjwa kwa kunawa mikono na kuvaa Barakoa

Waziri Mkuu awataka Wananchi kujilinda na Magonjwa kwa kunawa mikono na kuvaa Barakoa

Lets call a Spade a Spade not a big Spoon.... Magonjwa mbali mbali yapi ? kuumwa kichwa, kuteguka mguu ?.., Sijui kwanini hawa watu wanaona uvivu ukakati kutamka hili neo ambalo linaendana na changamoto ya upumuaji
 
Yaani itafika mahali watakiri tu ukweli! Kweli mficha maradhi kifo humuumbua
 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Watanzania wana jukumu kubwa la kumuenzi Balozi John Kijazi kwa kutenda yale yote mema aliyokuwa akitenda.

Aidha, amesema jukumu jingine ni kuendelea kuiombea familia yake, hasa katika kipindi hiki kigumu.

Akitoa salamu za serikali kwenye mazishi ya Balozi John Kijazi amewashukuru viongozi wa dini kwa kuendelea kuliombea Taifa kama ambavyo Rais Dkt. Magufuli alihimiza jana, na kwamba jana Waislamu walitimiza, leo Wasabato na kesho anaamini wengine wataendelea.

Amesema serikali inawapenda wananchi wake na inaendelea kufuatilia magonjwa yote, lakini wananchi waendelee kuchukua tahadhari ikiwemo kunawa mikono, kutumia vitakasa mikono na kuvaa barakoa.

Kuhusu ugonjwa wa Corona amesema inafahamika kwamba hii ni vita na imeanzia kwa wakubwa na bado inaendelea, hivyo ni vyema wananchi wakajiridhisha na vitu wanavyotumia ikiwemo barakoa, kama ambavyo Rais Magufuli amewahi kutahadharisha

View attachment 1707668
Nilikua sijui PM naye ni msanii
 
Back
Top Bottom