Waziri Mkuu: Dodoma kufumuka msongamano wa magari

Waziri Mkuu: Dodoma kufumuka msongamano wa magari

Sooth na Sikonge
Kuna hoja ya kutumia 'disapora' kwasababu ya uwezo wao huko walipo

Nakubali wapo Watanzania katika tasnia mbali mbali wanaofanya tusiyotarajia

Kagame amewatumia sana,wameleta culture mpya kukiwa tayari na culture ya kuwajibika na kuondoa rushwa

Nawafahamu Watanzania wengi, wahandisi, waandishi wa habari, madaktari, wahasibu n.k. wanofanya 'vitu' kwa wenzetu na wanaheshimika

Ujenzi wa rings unaweza kuwapa ikafanyika kama wanavyofanya huko waliko.

Tatizo, watakuwa 'frustrated' si kwa masilahi bali bureaucracy na rushwa

Kuna wataalam wa IT nje wangeweza kufunga vifaa 'polisi' kwa muda mfupi
na kwa ufanisi. Lakini je, wangewezaje ikiwa tunajua mradi ulihusisha vigogo? Mkataba 'umefichwa' inasemwa wamehusika ''wazito''

Mfano rahisi sana, nguli wa BBC aliletwa na kupewa shirika alibadilli.
Kweli katika muda mfupi sana watu wakaanza kutumia habari za shirika letu

Guess what! walimuondoa, hakukidhi mahitaji yao.

Huwezi kutumia disapora kwasababu 'inner circle' watakula wapi? Wanachotaka ni kampuni local ili wagawane mradi

Wagawane mradi kama ule wa machinjio ya Ruvu alioibua Mwigulu.
Nguzo zimesimama miaka nenda rudi, aliyepewa tenda, mhandisi, consultant, wenye kazi (halmashauri) wamegawana chao! ni wazawa hawa

Ili kukomesha upuuzi wa aina hii, local contractors wakae pembeni kwanza. Wajifunze maana ya kazi na si rushwa.

Tutumie Diaspora kwanza kwa kuwapa kazi moja kwa moja bila kupitia mauza uza ya bodi n.k. Najua kisheria itasumbua lakini sheria zinatungwa na watu!

Kuna nyakati lazima hatua zenye maumivu zichukuliwe

Mimi si mpenzi wala mashabiki wa 'wazawa' wanaoua wazawa wenzao kwa professional negligence inayotokana na corruptions and moral decay

Sipendi bodi kwani ni magenge ya ulaji tu, hayana masilahi na umma.

Futa bodi ya Wakandarasi, Injinia, Sumatra n.k.
Weka wazawa benchi wajifunze, tuache uzawa unaoua wazawa

Bodi hazina masilahi na umma ni maeneo ya kupatia allowance tu.
Ndugu yangu, kimsingi unakubaliana nami kuwa tatizo sio utaalam-tatizo ni bureaucracy na rushwa. Hili sio tatizo la wataalam tu, ni la kila mtu mwenye nafasi katika serikali. Tuwe na matumaini maana haya yote yanaweza kubadilika kwa hii 'takukuru mpya', mahakama ya mafisadi na utashi wa kisiasa uliopo. Hivyo bado nasimama palepale kuwa wazawa wapewe miradi. Tuache yaliyopita, tufungue ukurasa mpya.
 
Ndugu yangu, kimsingi unakubaliana nami kuwa tatizo sio utaalam-tatizo ni bureaucracy na rushwa. Hili sio tatizo la wataalam tu, ni la kila mtu mwenye nafasi katika serikali. Tuwe na matumaini maana haya yote yanaweza kubadilika kwa hii 'takukuru mpya', mahakama ya mafisadi na utashi wa kisiasa uliopo. Hivyo bado nasimama palepale kuwa wazawa wapewe miradi. Tuache yaliyopita, tufungue ukurasa mpya.
Mkuu Sooth nakubakubaliana nawe kabisa na hakuna mahali nimekataa hilo.
Nilichosema ni kuwa Eng wa nchi nyingine anajali professional na masilahi ya umma.

Eng. wa Tanzania ana utaalamu pengine Zaidi, lakini, utaalamu wake umefunikwa na kukosa maadili, rushwa na kutojali masilahi ya umma

Nikatoa mfano, limeangauka jumba msimbazi likaua watu.
Likaanguka Indira Gandhi, likaua watu.
Hata bila tume ilijulikana lile jingo liliongezwa ghorofa tofauti na ilivyokuwa.

Hakuna aliyewajibika ukiacha vidagaa vya manispaa.

Mkuu wa shirika lililolokuwa na jengo na aliyeshiriki kuongeza ghorofa kinyemeala bado yupo kazina anaendelea na ujenzi

Eng na consultant wapo with impunity. Kwa hali hii bodi ya Wakandarasi, bodi ya Eng hazikuwajibika.

Sababu kubwa ni chain ya 'uluwa' huku wakiweka public interest pembeni.

Kuendelea kuwapa kazi ni kukubali hoja yao ya kutokuwa na public interest.

Wote waliohusika hawana masilahi na Taifa wala huruma na maisha ya wazawa.

Jibu kubwa ni kuwa bodi hizi na wataalam wake huko mitaani wametengeneza syndicate ya masilahi tumbo na si ya umma

Kama yupo Mjapan au Mnigeria atakayeweza kujali maisha ya watanzania hata kama si mzawa, anajali masilahi na kuheshimu taaluma yake, apewe kazi.

Kuhusu matumaini ya 'takukuru mpya' lazima tujiulize ile ya kwanza ilifeli kwanini?

Unakumbuka sakata la mwendesha mashtaka na PCCB?

Hakuna kilichobadilika kwa kuweka watu wapya.

Tatizo la Takukuru ni mfumo, kwamba ipo chini ya mtu na si umma.

Hakuna kipya kama 'mzee' hataridhika. Hivi unategemea Takukuru ichunguze Lugumi?

Matumaini mabaya sana ni kuamini mtu na si taasisi.

Angalia taasisi za umma zilivyogeuzwa kuwa za vyama vya siasa.

Zinashindwa kufanya kazi kwa haki kwasababu zinapokea maagizo ya chama na serikali

Njia ya kweli ni kuwa na mfumo ulioandikwa(katiba) utakaombana kila mmoja kuanzia kijijini hadi Dodoma au Magogoni.

Taasisi zifanye kazi ya ku shape nchi si mtu mmoja.

Hii habari ya kutumaini mtu na si watu au wataalam ndiyo imepelekea marufuku kama za sukari ambazo kimantiki haikufanywa kiweledi na kuumiza watu bila sababu.

Tungetumia wataalam suala hilo lingefanyika kwa ufanisi

Nyerere alipopigania uhuru, nguvu haikuwa yeye bali watu na taasisi alizokuwa nazo.

Hakuna anayemsogelea hata kwa asilimia 40 kwa viongozi waliopo au waliopita
Nani ataweza mwenyewe

Hoja yangu inabaki, wakandarasi uchwara wa ndani hapana, vunja bodi za Injinia na wakandarasi hazina masilahi ya umma , ni vituo vya ajira tu!
 
Wahandisi wetu wajitahidi kufanya lobbying. Binafsi sio mhandisi lakini nawatetea kutokana na faida tutakazopata kama taifa ikiwa ujenzi utafanywa na wahandisi wetu. Sasa ungetarajia waje hapa waeleze kwanini wao wapewe kazi na sio wachina. Ungetarajia waje hapa waeleze kwanini kazi zao zinatiliwa shaka. Tusipuuze jukwaa hili, viongozi wanapita na kupembua pumba na mchele hivyo kutoa fursa adhimu ya wao kusikilizwa.
 
Sooth Nguruvi3 Sikonge ushauri wenu na mjadala wenu umeendelea kunipa maarifa zaidi..

Naona ushauri wenu kwa Taifa letu, na wote tunajua uadilifu ndio TATIZO kubwa kwa washika Dau wanao Pata dhamana.. Naamin kama wale mafisadi wanasoma huzi huu watakua wanajua jinsi gani tunawachukia kwa wao kutanguliza matumbo yao
 
Wahandisi wetu wajitahidi kufanya lobbying. Binafsi sio mhandisi lakini nawatetea kutokana na faida tutakazopata kama taifa ikiwa ujenzi utafanywa na wahandisi wetu. Sasa ungetarajia waje hapa waeleze kwanini wao wapewe kazi na sio wachina. Ungetarajia waje hapa waeleze kwanini kazi zao zinatiliwa shaka. Tusipuuze jukwaa hili, viongozi wanapita na kupembua pumba na mchele hivyo kutoa fursa adhimu ya wao kusikilizwa.
Mkuu kuna wanaodhani ipo chuki dhidi ya fani ya uhandisi, si kweli.

Tunachoeleza hapa ni kujitetea sisi kama wananchi.
Waliopewa dhamana ya kututetea wanatetea matumbo yao kwa rushwa, gharama za uzembe huo anazilipa mama ntilie au kibarua aliyeuawa jengo likiporomoka.

Gharama tunalipa walipa kodi tunaolazimika kujenga barabara kama ya Sinza kila baada ya miaka 2, wakati Morogoro rd ya Kajima ina miaka 20.

Gharama tunalipa kwa kupoteza maisha barabarani na kubaki na walemavu kutokana na kazi hovyo za wahandisi wazawa

Bodi za wahandisi za wazawa zinazopaswa kulinda public interest, au wakandarasi na consultants zimejiunga katika kazi hafifu kwa ubora na hatari kwa maisha yetu.

Yes, tunataka pesa ibaki katika mzunguko wetu badala ya kwenda nje, gharama za kubakiza pesa ni kubwa kwa thamani ya maisha kulikokuziacha ziende nje

Majengo yanaporomoka hakuna anayewajibishwa.
Juzi wameambiwa wasijenge ghorofa zaidi ya 2 Dodoma, nani anajali.

Lakini pia inakula kwao, mashirika ya nje yakitaka ujenzi hualika watu

Wanajua, wahindisi, contractors, consultants na bodi zinazowasimamia hazina viwango , zimejaa rushwa na hazina maadili wala uzawa unaosemwa

Mradi wa Milioni 500 akipewa mzawa, na mradi huo uki ongezwa thamani na kuwa mili 800 kwa mgeni, nitafurahi mgeni akipewa.

Mkuu hawawezi kuja kujitetea au ku lobby kwasababu wanajua rushwa imechafua tasnia yao, madhara wanayosababisha kwa umma, na syndicate wanazozifanya kwa maisha ya wazawa.

Njia ni moja, wakae pembeni!
 
Kwani ile ripoti ya CDA+Mkuu wa mkoa ishawasilishwa? Maana haya mapendekezo ndio yalipaswa yawe mle ili mji wa Dom usije kuwa kama Dar
 
Wana JF,

Nikiwa nimesomea Uhandisi ujenzi wa barabara ingawa sipo kwenye ujenzi tena, nimelipokea kwa furaha sana tangazo la serikali kuwa hatimaye wanahamishia DODOMA Makao Makuu ya taifa la Tanzania ambayo ni zaidi ya miaka 40 tangu tutangaze kuhamishia huko.

Naiomba tu Serikali yetu ya awamu wa ya tano kuchora mapema barabara za mduara kuzunguka Dodoma walau mbili. Ukiangalia miji mingi mikubwa wana hizo RINGS kuzunguka miji yao na mara nyingi zinakuwa ni Highway Roads au Express roads.

Hizi barabara zitawasaidia ambao hawataki kupita Dodoma mjini hasa Maroli kuuzunguka mji na kutokusabisha foleni za magari pamoja na zenyewe pia kuingia kwenye foleni za magari kama ulivyo mji wa Dar es salaam.

Najua sasa hizi kuna maeneo tayari watu wameshajenga na hivyo serikali itabidi ilipe fidia ila ninaamini hawajajenga wengi na hivyo kuwahamisha haitakuwa gharama kubwa. Ila mara tu Serikali na Mabalozi wakihamia basi utafumuka msululu mkubwa sana wa magari mjini Dodoma na itakuwa taratibu tunahamisha shida za Dar kuja Dodoma.
Tukichelewa kuhamisha watu na kusimamisha ujenzi kwenye maeneo zitakapopita hizi RINGS za barabara kuzunguka dodoma (napendekeza ziwe barabara 2 kwa kila upande na upana uwe 3.5m kila barabara ambayo inaleta upana wa min. 20m) huko mbele gharama zitakuwa kubwa na tutapata shida kama ilivyo leo mtaa wa Uhuru Dar es salaam.

Natamani watu wa CDA wawe wameshalifanyia kazi na kama bado basi wafanye haraka ili liingizwe kwenye Master Plan ya DODOMA na watu wa Urban Planing wakisaidiana na wizara ya ujenzi pamoja na TanRoads.

Kwenye picha nimeweka tu kwa haraka muonekano wa hiyo miduara au RINGS kuzunguka Dodoma ila wataalamu wa Urban Planing watajua ni nini nilimaanisha na kuziweka kwa usahihi zaidi wakishirikiana na watu wa Road designing.View attachment 370791
Mkuu Sikonge tunashukuru mawazo yamesomwa na yatafanyiwa kazi. Ni jambo jema na huo ndio uzalendo na ujenzi wa Taifa

Rais kasema itajengwa ''ring road' Dodoma, apongezwe kwa hili kama tulivyolijadili
Dodoma ikpendeza, Tanzania itapendeza, Watanzania tutapendeza na sote tutakuwa washindi
 
Nguruvi3 asante kwa maelezo yako. Nilihangaika kidogo kutafuta ni wapi Rais kalisema hili. Ila nimefanikiwa kuipata video yake.
Cha muhimu kwa sasa ni kuwa wazichore na ziwe kwenye ramani. Hata kama watachonga barabara ya vumbi hasa ile ya pili nje ya mji na iwe hivyo kwani kwa miaka ya mbele eneo litakuwepo na muda ukifika ni kujenga tu baada ya kusafisha.

Watu hata wakilima si mbaya ila.cha muhimu wasijenge. Muda ukifika wa kujenga kwanza tauari mji utakuwa umefika huko.
Nimependa pia hili la ujenzi wa reli. Nafikiri hapa tungelijenga tayari Trams. Ndiyo maana kuna umuhimu wa kufanya barabara pana kwani zitaweza kupitisha line sa umeme, mabomba ya Gas, mabomba ya Maji safi na maji taka pamoja na maji ya mvua. Pia si vibaya tukianza kujenga line za Waenda kwa Mguu na waenda na Baiskeli.
Dodoma hainyeshi sana na hivyo mtu anaweza kuwa anaendesha baskeli yake kwenda kazini na kurudi. Fikiri mtu anakaa Area C na anafanya kazi Dodoma Hotel, si unaendesha tu Baskeli? Pia ni zoezi zuri kabisa.
SKY IS THE LIMIT. Tujifunze kutoka kwa wenzetu.

Hapa MSHINDI ni Mtanzania kwani hizi Ring Roads zitasaidia kila anayeishi Dodoma na wote wanaopita njia kuelekea mikoa mingine na hata nje ya nchi.


Mkuu Sikonge tunashukuru mawazo yamesomwa na yatafanyiwa kazi. Ni jambo jema na huo ndio uzalendo na ujenzi wa Taifa

Rais kasema itajengwa ''ring road' Dodoma, apongezwe kwa hili kama tulivyolijadili
Dodoma ikpendeza, Tanzania itapendeza, Watanzania tutapendeza na sote tutakuwa washindi
 
Hii report sijui kama iliwakilishwa.

Nategemea hata kama walishafanya na wakasahau hili.basi waongezee. Wasisahau tu kuongezea na plan ya usafiri wa Railway kuzunguka mjini na hasa Trams ambazo zinakwenda kasi zaidi bila kuwa na foleni kama Mabasi ya mwendo kasi. Ethiopia wameweza.


Kwani ile ripoti ya CDA+Mkuu wa mkoa ishawasilishwa? Maana haya mapendekezo ndio yalipaswa yawe mle ili mji wa Dom usije kuwa kama Dar
 
Samahani wakuu Sikonge na Nguruvi3 hii makala nimeiona leo. Mawazo mazuri sana ya kuweka hizi ring-roads mapema kabla msongamano haujakuwa mkubwa. Hongereni sana.

Nilikuwa na wazo la nyongeza au mbadala kwa mji mpya wa Dodoma lakini pengine limekwishapitwa na muda. Wazo langu lilikuwa kuifanya Dodoma mjini (Central Business District au CBD) isiwe na magari (car free zone). Usafiri ungekuwa wa light-rail au mabasi (mithili ya mwendokasi), baskeli, miguu. Mjini Dodoma uwe rafiki kwa watembea miguu.

Oh well, this may be moot.




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Samahani wakuu Sikonge na Nguruvi3 hii makala nimeiona leo. Mawazo mazuri sana ya kuweka hizi ring-roads mapema kabla msongamano haujakuwa mkubwa. Hongereni sana.

Nilikuwa na wazo la nyongeza au mbadala kwa mji mpya wa Dodoma lakini pengine limekwishapitwa na muda. Wazo langu lilikuwa kuifanya Dodoma mjini (Central Business District au CBD) isiwe na magari (car free zone). Usafiri ungekuwa wa light-rail au mabasi (mithili ya mwendokasi), baskeli, miguu. Mjini Dodoma uwe rafiki kwa watembea miguu. Oh well, this may be moot.
Kama wangekuwa wanashaurika mji ulikuwa upangwe mapema sana. Wazo la light rail ni zuri sana. Mfano kuanzia Makutopora hadi Railway station

Ili kupunguza msongamano, ring roads zilitakiwa zianze kwanza, halafu kutenga maeneo kwa shughuli mahususi
Kwa mfano kuwe na blocks, kwamba kuna central business district, gov. offices karibu na Bunge
Academic arena kuzunguka UDOM, eneo la mabalozi, maeneo ya starehe na biashara

Hili litasaidia sana kusambaza 'watu' hasa nyakati za kazi na kupunguza msongamano

Lakini pia kwa vile bado maeneo ya wazi yapo kwanini wasifikirie kuwa na ''satellite cities ''
 
Kama wangekuwa wanashaurika mji ulikuwa upangwe mapema sana. Wazo la light rail ni zuri sana. Mfano kuanzia Makutopora hadi Railway station

Ili kupunguza msongamano, ring roads zilitakiwa zianze kwanza, halafu kutenga maeneo kwa shughuli mahususi
Kwa mfano kuwe na blocks, kwamba kuna central business district, gov. offices karibu na Bunge
Academic arena kuzunguka UDOM, eneo la mabalozi, maeneo ya starehe na biashara

Hili litasaidia sana kusambaza 'watu' hasa nyakati za kazi na kupunguza msongamano

Lakini pia kwa vile bado maeneo ya wazi yapo kwanini wasifikirie kuwa na ''satellite cities ''
Exactly kama ninavyofikiria. Safari (trips) huanzishwa na vyanzo (trip generators) pamoja vivutio (trip attractors). Wazo la kuwa na satellite cities ni ili kusambaza hivi vyanzo na vivutio vya safari ili kuondoa msongamano.

Ukizisambaza hizi activities zinazosababisha safari basi asubuhi sio kila mtu anaelekea sehemu moja na joini anarudi nyumbani toka sehemu moja. Hiki ndio chanzo cha msongamano wa asubuhi na jioni.

Kwa kuwa Dodoma bado ndio inaanza kukua hii ni fursa nzuri sana kupangilia miundombinu ya huu mji uwe mfano Afrika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu yangu Sikonge,

Umeleta wazo moja kubwa sana endelevu! Wala si Dodoma pekee ambayo inahitaji ring roads kuhakikisha inter regional transit inaendelea bila kuleta bottle neck kwenye mji au wilaya husika!

Ni dhahiri lazima wizara ya miundombinu na mamlaka ya Barabara TanRoads waanze kufikiria kupanua mfumo wa miundombinu ya barabara kwa kuweka ring roads na kuanza kutenga maeneo maalum hasayasiyona watu wengi ili kuweka new road reserves kisha kuwekeza ujenzo wa barabara!

Think of barabara kuu kwenda Arusha ilivyo na congestion kutoka njia panda Himo mpaka upite Ngaramtoni au Kambi ya Fisi...

Huwa nafanya gumzo na Waziri husika kule twitter(ndiko makazi yangu mapya siku hizi 😉) nitamuuliza kama hii ya ring roads pale Dodoma au hata Morogoro kama iko kwenye pipeline!

Wasalaam,
Mchungaji
 
Mkuu hatuna upungufu wa sheria, tuna upungufu wa mfumo utakaohakikisha sheria zinafuatwa. Kinachotokea sasa hivi ni ladha ya 'big G' si jambo sustainable

Kwanini mahakama zilishindwa kusimamia rushwa hapo awali?
Unakumbuka mgao uliohusisha majaji? Nini kimetokea baada ya kubainika?

Unakumbuka jengo lililoanguka kati kati mjini la ghorofa 16, kati hizo nne ziliongezwa kinyemela taasisi ya umma ikihusishwa! Mkurugenzi wa shirika husika yupo kazini, watu walikufa hakuna kilichotokea

Kama tunakubaliana pesa ibaki nchini, tunaweza kuweka miradi na kuigawa kwa wazawa pesa ikaenda 'nyumba' ndogo tukapata rings hewa.

Bandari tulikuwa na mradi, pesa ikaenda 'nyumba ndogo' leo tunarudi pale pale
Tunacheza mduara wenzetu wapo sambamba na Michael Bolton

Mimi nakiri kabisa, sisi waafrika tumefeli kujisamimia.

Nguruvi3

Kule twita Mh. Ally Saleh alinirushia changamoto mbili ambazo nitazifungulia uzi mpya nisiharibu hoja ya Mzee Sikonge. Lakini nitanukuu maswali hayo:

  1. Tuna ukanda wa bahari 1500 klms...na hatuwezi kujilisha kwa samaki sembusa kusafirisha...nchi hii imerogwa...
  2. Tuna energy source za jua, makaa ya mawe, upepo, taka marundo, bahari, mito, maziwa na ndio kwanza megwatts kiduchu tukielekea VIWANDANI....
Kwa nini tunacheza mduara tunarudi pale pale?
 
Hapo inabidi rais awe mkali kama Kagame. Ukiharibu kwa Kagame, hata ujifiche kwapani kwa Obama atakupata tu. Nchi hii iliwahi kuwa na uwezo wa kuwaadabisha wabadhirifu, enzi hizo ukisakia Usalama wa Taifa unatetemeka. Siku hizi usalama unakuhusu kama ni mwanasiasa wa upinzani au kama umemkashifu mkubwa mtandaoni. Economic Intelligence haipo kabisa. La sivyo wale wote wa Escrow wangekuwa wanalia kama Ulimboka.
Ni makosa makubwa kutegemea mtu mmoja kusimamia na kuleta unyoofu na ustawi. Kuwa na Rais mkali haisaidii. Wananchi lazima tuwajibika kwa kila njia kuhakikisha kuna uwajibikaji kila sehemu na kwa kila mtu.
 
Nguruvi3

Kule twita Mh. Ally Saleh alinirushia changamoto mbili ambazo nitazifungulia uzi mpya nisiharibu hoja ya Mzee Sikonge. Lakini nitanukuu maswali hayo:

  1. Tuna ukanda wa bahari 1500 klms...na hatuwezi kujilisha kwa samaki sembusa kusafirisha...nchi hii imerogwa...
  2. Tuna energy source za jua, makaa ya mawe, upepo, taka marundo, bahari, mito, maziwa na ndio kwanza megwatts kiduchu tukielekea VIWANDANI....
Kwa nini tunacheza mduara tunarudi pale pale?

Niliyaona haya maswali ya Mh. Saleh kule twita lakini sikutaka kuyapatiliza kwa ajili ya ufinyu wa uga wa kujibu. Yaanzishie uzi Rev. Kishoka hapa watu wayadadavue.

Jibu rahisi kwake ni kuwa "Penye miti hakuna wajenzi." Hapa ninamaanisha kuwa kama tunataka kuitumia hii "miti" tulionayo vizuri lazima tuanze kufikiria kama "wajenzi".

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni makosa makubwa kutegemea mtu mmoja kusimamia na kuleta unyoofu na ustawi. Kuwa na Rais mkali haisaidii. Wananchi lazima tuwajibika kwa kila njia kuhakikisha kuna uwajibikaji kila sehemu na kwa kila mtu.
Mkuu wananchi kuwajibika ni pamoja na kueleza nini wanataka, lini na kiwe vipi. Katika mkusanyiko wa mawazo ndipo uwajibikaji unapotokea kwa maana ya neno 'tumekubaliana'

Kwa bahati mbaya sana kwasasa utamaduni huo haupo, kuna misemo inatumika kuzima sauti za wananchi
1. Huo ni uchochezi
2. Hali ya usalama haijatangamaa na taarifa za kiintelejensia
3. Kwamba, kila mtu azungumzie maendeleo ya eneo lake na si nchi.
Mwenye jimbo la Tanzania ni mmoja

Kumejengwa hali ya woga miongoni mwa wawakilishi na watendaji. Hili limeua 'new idea'
1. Tazama bunge lilivyogeuka kuwa tawi la serikali
2. Watendaji wanavyoogopa kuwa na 'innovation'

Katika hali hiyo usitegemee kuna mtu anayekaa chini na kufikiri kwanini kusiwe na fast train kati ya Arusha na Moshi.

Arusha ni host wa Watalii na Moshi ni sehemu ya kutembelea hasa mlima Kilimanjaro
Ni umbali wa KM chini ya 150, inachukua masaa 4 au 5 kutoka point moja hadi nyingine

Wazo la train ya Mwakyembe lilizaliwa hapa JF. Hata kama haijafanikiwa kwa kiwango lazima tukubali kuna uthubutu na maboresho yakifanyika inawezekana

Mawazo kama hayo ni mengi yanataka mtu wa ''ku-harness''

Soon Dodoma kutakuwa na congestion.

Halamashauri za majiji na manisaa nyingi zime prove failure

CDA haikuwa na tatizo kama authority.
Tatizo lilikuwa kwa viongozi kufanya CDA kama eneo la wastaafu

Sioni kwanini CDA ilifutwa kwasababu ilianzishwa kwa mujibu wa sheria ya bunge ikiwa na mamlaka zaidi ya failure Municipal and City councils.

Kwa maneno mengine, Dodoma inategemea mipango sijui ya kamati ambayo haina mamlaka makubwa ya kisheria kama ilivyokuwa CDA

Kuhusu hoja kwanini tunacheza mduara tukiwa na resource zote.

Jibu ni rahisi, viongozi wetu wapo bize na mambo yasiyo na maana kuliko innovations. Hivi kukimbizana na dhamana za wanasiasa inasaidiaje nchi na watu wanaofanya hivyo wana muda gani mwingine wa kufikiri?

Waulize viongozi hao, katika miezi 8 wamefanya nini cha kubadili maeneo yao kimaendeleo, zero!

Muda mwingi ni wa kutafutana , kuwekana mahabusu kukimbizana nani asipewe dhamana na insane kama hizo

Fikiria Mbunge mmoja aliwekwa mahabusu miezi 4. Uongozi wa mkoa ulikuwa bize kuhakikisha hapati dhamana.

Uongozi huo huo hauna ring roads katika mkoa na congestion inaendelea.
Muda wa miezi 4 kukimbizana na dhamana, wazo la light rail, ring roads litatoka wapi!!

Kuna maswali relevant.Kwanini Dar samaki auzwe bei sawa na Nairobi, Bujumbura au Kigali
Kwanini tuwe na uhaba wa samaki kukiwa na maziwa na bahari! Nani amefikiri hilo

Tunacheza mduara kwasababu hatuna 'management' kama nchi. T
umejawa hofu, woga na kulamba miguu watu
 
Kama wangekuwa wanashaurika mji ulikuwa upangwe mapema sana. Wazo la light rail ni zuri sana. Mfano kuanzia Makutopora hadi Railway station

Ili kupunguza msongamano, ring roads zilitakiwa zianze kwanza, halafu kutenga maeneo kwa shughuli mahususi
Kwa mfano kuwe na blocks, kwamba kuna central business district, gov. offices karibu na Bunge
Academic arena kuzunguka UDOM, eneo la mabalozi, maeneo ya starehe na biashara

Hili litasaidia sana kusambaza 'watu' hasa nyakati za kazi na kupunguza msongamano

Lakini pia kwa vile bado maeneo ya wazi yapo kwanini wasifikirie kuwa na ''satellite cities ''

Naomba kuuliza, planners wetu hasa wa CDA walikwenda wapikujifunz mipango miji?

Je wizara ya ardhi na maendeleo ya nyumba na mipango miji, ina kitengo maalum cha town/city planners?
 
Naomba kuuliza, planners wetu hasa wa CDA walikwenda wapikujifunz mipango miji?

Je wizara ya ardhi na maendeleo ya nyumba na mipango miji, ina kitengo maalum cha town/city planners?
Mkuu ninakumbuka tu kuwa CDA ilipoanzishwa kulikuwa na wataalam waliopelekwa nje kujifunza

CDA haikuanzishwa ku plan mji, ilianzishwa kusimamia suala la uendelezaji wa miji
Tuna chuo cha ardhi ambacho kimetoa wataalam wengi katika ukanda wanaofanya vizuri

Ilikuwa jukumu la CDA kuwatumia yenyewe ikiwa ni authority hasa katika management

Kilichotokea ni kuifanya CDA kama eneo la wastaafu kupata 'kibarua' wakielekea kuchoka
Hapakuwepo na innovation kwasababu ilikuwa ni eneo la mapunziko

Ukiisoma sheria iliyaoanzisha CDA kama mamlaka hakuna tatizo kabisa.
Hivyo CDA kama chombo na sheria hakikuwa na tatizo, tatizo ni lile lile la kila siku 'management ya masuala ya kitaifa' kwamba, mambo yanafanyika bila kuwa na sera wala mipango

Kosa hilo linajirudia kwa kuundwa chombo na serikali kusimamia mipango ya Dodoma. Nasikiawalikwenda kujifunza China na kwingine. Swali, tunaongozwa na sera gani kuhamia Dodoma ghafla kiasi hicho?
 
Naomba kuuliza, planners wetu hasa wa CDA walikwenda wapikujifunz mipango miji?

Je wizara ya ardhi na maendeleo ya nyumba na mipango miji, ina kitengo maalum cha town/city planners?

Karibuni kila mji mkubwa TZ una/ulikuwa na master plan yake. Tatizo ni usimamiaji wa hizi masterplans. Development inaachiwa kuendelea kiholela halafu baadae inafuatiwa na bomoa bomoa.

DSM ina Master Plan (MP) mpya (2010-2030) iliyobuniwa na DODI MOS Architects na kudhaminiwa na World Bank. Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi (Land, Housing, & Human Settlement) ndio owners na wasimamiaji wa MP hii. Je itapuuzwa kama MP za nyuma zilizotuletea mfumuko holela wa DSM? Time will tell.

Dodoma kwa sasa wanafanya mchakato wa kupata MP mpya ya mji. Hii iliripotiwa na magazeti hivi majuzi kama Tanzania: Govt Begins Drafting Master Plan for Dodoma.

Nadhani michango yetu hapa na kwengineko inaweza kuzaa matunda. Kwa hiyo watu wasichoke kukisema kile wanachokiona kinafaa kama wakuu Sikonge Nguruvi3, n.k.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom