Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 15,101
- 56,054
Au anataka kujijenga kisiasa mbele ya "wanyonge" ili aonekane kuwa yeye ni Magufuli aliyebaki?Ni chatu gang anataka kurudi kwenye kiki.
Yapo jangwani kule nyuma ya nyumba mafundi wameyafanya toolbox yao kila fundi ana basi lakeHayo mabasi 100 yanafanya kazi barabara zipi aisee?? Abiria wanajazana kituoni mabasi hayaji halafu mnasema mabasi yaliyo barabarani ni 100,aah wapi?
Mwendokasi ubabaishaji ni mkubwa sana, mfumo wa kuonesha tiketi kwenye mashine umekufa zaidi ya miaka 2 sasa na hakuna hatua zinazochukuliwa.
Mabasi yanayofanya kazi ni machache na hayo machache madereva wanapaki wanavyotaka..utasikia derava anakunywa chai, mara anapumzika nk
Anapiga gamba; kobe yupo ndani salama salimini.Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo amefanya ziara ya kushtukiza kituo cha mwendokasi eneo la gerezani na kukuta mfumo wa kusoma tiketi haufanyi kazi, mtendaji mkuu alisema mfumo haufanyi kazi baada ya kutokea mgogoro kati ya supplier na alieununua. Meneja huyo amesema mfumo mpya unajengwa na waziri mkuu kumuhoji inatumia miaka mingapi kukamilika?
Majaliwa amesema wanaibiwa mapato kwani wao wanatumia mtambo na wengine wanatumia mtambo mwingine na hawana namna ya ku-check.
Pia Meneja amehojiwa tangu aingie amenunua mabasi mangapi baada ya serikali kununua mabasi 140 huku mabasi yanayokadiriwa kuwa barabarani ni wastani wa 100.
Mtoa huduma ya mwendokasi aliagiza mabasi 70 ambayo yamekwama kuingia barabarani kutokana na mgogoro na waziri mkuu akasema anaenda kuyaona. Majaliwa amesema wananchi wanalalamika mabasi hayatoshi akitolea mfano Kimara watu wanaingilia dirishani na kuhoji mapato wanayokusanya wanapeleka wapi kama wanashindwa kununua mabasi.
Pia waziri mkuu amepita karakana ya Jangwani na sasa anaelekea Ubungo kuangalia mabasi yenye mgogoro
==========
UBUNGO: Kinachoendelea waziri mkuu anauliza hatua zinazoweza kuchukuliwa kwa mabasi yaliyokwama ambapo mtu TRA anasema sheria inamruhusu kamishna kuya-donate au kuyaharibu na waziri mkuu amesema hawezi kupewa Shabiby kwasababu hayamfai kwenda Dodoma kwani ni kwaajili ya barabara za mwendokasi na sasa anauliziwa mwanasheria
Pia waziri mkuu anawaambia forodha waendelee kufanya minada ya mizigo iliyokaa kupita kiasi mara kwa mara ili kusafisha nafasi ya kuagiza mizigo mingine na kuwataka wabadilike kwani baadhi ya wateja wanalalamika process zinachukua muda mrefu
Kassim Majaliwa anasema pesa zilizotumika zimekopwa world bank na zinalipwa na mabasi yameletwa na mjasiriamali laiki ameshindwa ku-comply na sheria na sheria zimechukua mkondo wake tangu 2018 na kutaka kesho wakae waamue
Majaliwa amesema serikali inao uwezo wa kununua mabasi lakini tatizo ni usimamizi na hawawezi kumsimamia msimamizi ambae hawezi na leo amemuweka pembeni mkurugenzi wa fedha na mwingine anamuachia Rais kwani yuko kwenye mamlaka yake.
kama ungekuwa mmoja wa anaetumia huu usafiri usingesema haya maana haujawahi kuwa bora hata siku mojaMtamkumbuka JPM
Upigaji haujawahi kukoma; ila ulikuwa unafanyika gizani. Awamu ya 5 ilizima taa ili raia wasione yanayofanyika. Tusubiri kuona maajabu ya miradi ya Chato.Yarudi kutoka wapi? Yalikuwapo humo humo. Jiulize mbona hawajawahi kununua mabasi? Kwanini hawataki kulipia Kodi yaliyoko bandarini ambayo hayauziki kwenye minada?
Jongoo Ni huyo mkurugenzi.
Kuna mheshimiwa mmoja aliambiwa na Mkuu wa Nchi kuwa amenunua gari la kifahari bila kufuata utaratibu. Akasimamishwa yeye na wenzake ili kupisha uchunguzi. Kumbe muda wote huo alipewa kibali na Ofisi ya WM. Hili asingeweza kusema mbele ya kadamnasi maana angeonekana kama anamtupia lawama WM.Kaulizwa wameshashakaa vikao vingapi na hawasemi chochote. Kiukweli mwendokasi kuna upigaji sana
Mràdi ulikosewa tangu awali. Mràdi huo ulitakiwa utumie train za umeme za kuzunguka kwà kutumia barabara hizo hizo. Matokeo yake wakaenda kumtoa mchina shida kwà kununua mabasi ya kichina.pia train ya umeme nauli ingekuwa kidogo, pia uharibifu ni kidogo, kuzitawala ni rahisi pia,kama ungekuwa mmoja wa anaetumia huu usafiri usingesema haya maana haujawahi kuwa bora hata siku moja
samson sialikamatwa kwa uhujumu uchumi, sasa atalipaje kodi yuko jela? halafu kwani lazima tuweke msimamizi binafsi? situajiri DG wenyewe ili akituzingua tuzinguane!Kama mtoa huduma bado ni samson group mjue hatuendi popote. Hao watapeli hawawezi kuaminika kutoa huduma nzuri. Kwanza sifa ya mwekezaji hawana wanategemea waibie serikali kwaza ndio wawekeze.
Lengo lao kuu ni kupata mali kwa kuiba mali ya umma kujitajirisha. Uwekezaji ni kuleta mtaji na ujuzi sio ubabaishaji mtu huna kitu.
Hujui kama jamaa wana mkopo mkubwa....Tulia wew! Wapigaj gan wanataka kurudi? Hicho anachokihoji wazir mkuu ni cha leo au jana? Wazir anamaanisha mwendokas imeshindwa kujiendesha ikiwemo kununua magari mengine zaid ya yaleyale yaliyonunuliwa na serikali. Kama wapigaj wanataka kurudi bas walisharud tang enzi ndo maana wazir mkuu kashangaa hata hela ya kununua magari mengine hawana.
Tunarudi kule kule. Haya mambo si ya kuulizana jukwaani. Angemwita yeye na viongozi wake ili wakae waone tatizo liko wapi. Kama ni uongozi lingeonekana tu. Na kama ni serikali ingeonekana tu maana Meneja angeweza kusema kweli yake bila kuonekana kuwa anamdhalilisha WM hadharani. Inabidi viongozi wakuu wabadilike.
Amandla...
Mnashauri yakifanyika utasikia private sector inanyanyaswa.Tungekuwa serious; Nyumbu ilitakiwa iwe ndio supplier and maintainer wa mabasi ya mwendokasi. Tungekuwa tumekuza uchumi wa ndani; ajira kwa watanzania; na kuongeza uwezo wa teknolojia.
Tunawaza tu kuagiza kutoka nje; hatuwazi ku-innovate na kuwa na vya kwetu no matter how ugly they might be, but gradually will be improved to modern ones!
Chato inarudi katika hali yake ya zamani ya Kijiji Cha ujamaa.Upigaji haujawahi kukoma; ila ulikuwa unafanyika gizani. Awamu ya 5 ilizima taa ili raia wasione yanayofanyika. Tusubiri kuona maajabu ya miradi ya Chato.
Public sector hawapigi?Mnashauri yakifanyika utasikia private sector inanyanyaswa.
Private sectors ya kitanzania wapigaji tu