Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo amefanya ziara ya kushtukiza kituo cha mwendokasi eneo la gerezani na kukuta mfumo wa kusoma tiketi haufanyi kazi, mtendaji mkuu alisema mfumo haufanyi kazi baada ya kutokea mgogoro kati ya supplier na alieununua. Meneja huyo amesema mfumo mpya unajengwa na waziri mkuu kumuhoji inatumia miaka mingapi kukamilika?
Majaliwa amesema wanaibiwa mapato kwani wao wanatumia mtambo na wengine wanatumia mtambo mwingine na hawana namna ya ku-check.
Pia Meneja amehojiwa tangu aingie amenunua mabasi mangapi baada ya serikali kununua mabasi 140 huku mabasi yanayokadiriwa kuwa barabarani ni wastani wa 100.
Mtoa huduma ya mwendokasi aliagiza mabasi 70 ambayo yamekwama kuingia barabarani kutokana na mgogoro na waziri mkuu akasema anaenda kuyaona. Majaliwa amesema wananchi wanalalamika mabasi hayatoshi akitolea mfano Kimara watu wanaingilia dirishani na kuhoji mapato wanayokusanya wanapeleka wapi kama wanashindwa kununua mabasi.
Pia waziri mkuu amepita karakana ya Jangwani na sasa anaelekea Ubungo kuangalia mabasi yenye mgogoro
==========
UBUNGO: Kinachoendelea waziri mkuu anauliza hatua zinazoweza kuchukuliwa kwa mabasi yaliyokwama ambapo mtu TRA anasema sheria inamruhusu kamishna kuya-donate au kuyaharibu na waziri mkuu amesema hawezi kupewa Shabiby kwasababu hayamfai kwenda Dodoma kwani ni kwaajili ya barabara za mwendokasi na sasa anauliziwa mwanasheria
Pia waziri mkuu anawaambia forodha waendelee kufanya minada ya mizigo iliyokaa kupita kiasi mara kwa mara ili kusafisha nafasi ya kuagiza mizigo mingine na kuwataka wabadilike kwani baadhi ya wateja wanalalamika process zinachukua muda mrefu
Kassim Majaliwa anasema pesa zilizotumika zimekopwa world bank na zinalipwa na mabasi yameletwa na mjasiriamali laiki ameshindwa ku-comply na sheria na sheria zimechukua mkondo wake tangu 2018 na kutaka kesho wakae waamue
Majaliwa amesema serikali inao uwezo wa kununua mabasi lakini tatizo ni usimamizi na hawawezi kumsimamia msimamizi ambae hawezi na leo amemuweka pembeni mkurugenzi wa fedha na mwingine anamuachia Rais kwani yuko kwenye mamlaka yake.
Ngoja kwanza naona hapa kuna jambo la kijinga sana, kwahiyo tulikopa pesa ya kununua mabasi hatukukopa pesa ya kulipa tra? tunauza mabasi kwa mnada baada ya kukaa miaka minne na mkopo na riba ziko palepale, sasa huo mkopo anaulipa nani?
Hayo mabasi yamenunuliwa shs ngapi? na kodi ni shs ngapi? kama kanunua bus 60m mnamwambia alipe kodi 180m na bado ana deni la world bank hatamie nigeyaterekeza.
Yarudi kutoka wapi? Yalikuwapo humo humo. Jiulize mbona hawajawahi kununua mabasi? Kwanini hawataki kulipia Kodi yaliyoko bandarini ambayo hayauziki kwenye minada?
Jongoo Ni huyo mkurugenzi.
Upigaji haujawahi kukoma; ila ulikuwa unafanyika gizani. Awamu ya 5 ilizima taa ili raia wasione yanayofanyika. Tusubiri kuona maajabu ya miradi ya Chato.
Kuna mheshimiwa mmoja aliambiwa na Mkuu wa Nchi kuwa amenunua gari la kifahari bila kufuata utaratibu. Akasimamishwa yeye na wenzake ili kupisha uchunguzi. Kumbe muda wote huo alipewa kibali na Ofisi ya WM. Hili asingeweza kusema mbele ya kadamnasi maana angeonekana kama anamtupia lawama WM.
Katika suala hili kuna mikataba imevunjwa ( hatuambiwi tatizo liko wapi na uamuzi wa kuivunja alifanya nani), Mkurugenzi anaulizwa kwa nini hajanunua magari mapya bila kuulizwa kama huo uwezo anao. Haya yote yangefanyika ofisini na kama kweli ataonekana ni mzembe na mpigaji basi angeondolewa kwenye nafasi yake mara moja. Hapa kama tatizo ni la kimfumo ( upatikanaji wa mikataba, upangaji wa nauli n.k) hata akija mwingine tutarudi hapa hapa.
Mràdi ulikosewa tangu awali. Mràdi huo ulitakiwa utumie train za umeme za kuzunguka kwà kutumia barabara hizo hizo. Matokeo yake wakaenda kumtoa mchina shida kwà kununua mabasi ya kichina.pia train ya umeme nauli ingekuwa kidogo, pia uharibifu ni kidogo, kuzitawala ni rahisi pia,
Kama mtoa huduma bado ni samson group mjue hatuendi popote. Hao watapeli hawawezi kuaminika kutoa huduma nzuri. Kwanza sifa ya mwekezaji hawana wanategemea waibie serikali kwaza ndio wawekeze.
Lengo lao kuu ni kupata mali kwa kuiba mali ya umma kujitajirisha. Uwekezaji ni kuleta mtaji na ujuzi sio ubabaishaji mtu huna kitu.
Tulia wew! Wapigaj gan wanataka kurudi? Hicho anachokihoji wazir mkuu ni cha leo au jana? Wazir anamaanisha mwendokas imeshindwa kujiendesha ikiwemo kununua magari mengine zaid ya yaleyale yaliyonunuliwa na serikali. Kama wapigaj wanataka kurudi bas walisharud tang enzi ndo maana wazir mkuu kashangaa hata hela ya kununua magari mengine hawana.
Wachangiaji 90% kwenye huu uzi wanatamani zile enzi za kwapuaaaa, piga cha juu, nk zirudi!
Kassim Majariwa hata marehemu jiwe alikuwa anamgwaya,,,,subiri nione mziki wake!
Tunarudi kule kule. Haya mambo si ya kuulizana jukwaani. Angemwita yeye na viongozi wake ili wakae waone tatizo liko wapi. Kama ni uongozi lingeonekana tu. Na kama ni serikali ingeonekana tu maana Meneja angeweza kusema kweli yake bila kuonekana kuwa anamdhalilisha WM hadharani. Inabidi viongozi wakuu wabadilike.
Tungekuwa serious; Nyumbu ilitakiwa iwe ndio supplier and maintainer wa mabasi ya mwendokasi. Tungekuwa tumekuza uchumi wa ndani; ajira kwa watanzania; na kuongeza uwezo wa teknolojia.
Tunawaza tu kuagiza kutoka nje; hatuwazi ku-innovate na kuwa na vya kwetu no matter how ugly they might be, but gradually will be improved to modern ones!
Upigaji haujawahi kukoma; ila ulikuwa unafanyika gizani. Awamu ya 5 ilizima taa ili raia wasione yanayofanyika. Tusubiri kuona maajabu ya miradi ya Chato.
Chato inarudi katika hali yake ya zamani ya Kijiji Cha ujamaa.
Aiseeh Mungu mkubwa. Ilibaki kidogo tu ujengwe uwanja wa mpira Kama kirumba pale.
Ile benki sijui Kama total deposit kwa siku inaingiza milioni.
Haina haja ya waziri mkuu kwenda kwa kushtukiza,angetuma wakaguzi wakague wampe ripoti then awapige fire. Kwa Tanzania hii atatembelea ofisi ngapi kwa kushtukiza?
Leo ni siku ya furaha kubwa kwangu toka tuondokewe na Jemedari wetu mpendwa mzalendo wa nchi yetu, Mfalme na mtetezi wa wanyonge, Hayati Rais John Joseph Pombe Magufuli, kuona waziri wetu mkuu Majaliwa Majaliwa kwa mara nyingine akichukua hatua ya kufanya ziara ya kushitukiza kwenye shirika la Mabasi ya Mwendo Kasi jijini Dar es salaam.
Pamoja na kuwa ziara ya waziri mkuu huyo kuchelewa toka nilipo toa malalamiko yangu juu ya mtindo na mwenendo wa ukataji tickets kwenye hivyo vituo vya mabasi ya mwendo kasi humu JF mwaka jana, ni kitu bado mimi nashukuru kwa kuona serikali inatimiza wajibu wake wa kusimamia mashirika ya umma.
Naam! Naipongeza serikali ya ndugu zetu wakenya kwa kutambua umuhimu wa kuondoa kero za wananchi wao wanazopata kila siku ya Mungu kwenye misongamano ya magari barabarani kwa ku-introduce Commuter Rail Network mjini Nairobi. Uamuzi huu ni kitendo ambacho kinatakiwa kuigwa na kila serikali ya...
www.jamiiforums.com
Furaha yangu ingekuwa kubwa na ya kupindukia kupita kiasi kama ningeona mfumo mzima wa watu au watumishi walio husika na uchakachuaji wa mlolongo mzima wa ubadilifu na wizi wa fedha na mali za umma, mpaka wale wachapishaji na wauzaji wa hizo tickets na ma-engineer na mafundi wote wa magari ukiondolewa na kuajiliwa watu wapya ili liwe fundisho kwa watumishi wengine kwenye mashirika mengine ya umma ambayo nayo yana watendaji wa sampuli hiyo.
Haitakuwa haki wezi na wadokozi wanao shirikiana na viongozi wao wenye mamlaka katika kuliua shirika la umma, wakaendelea na kazi kwenye shirika hilo tena, kwani ikumbukwe kuwa mwizi ni mwizi tu na haitakuwa rahisi kwake kuacha tabia hiyo ya udokozi na ufujaji wa mali za umma kama ataendelea kuwa katika position hiyo hiyo.
Watu wenye fikra za namna hii ni watu ambao maendeleo ya ustawi wa jamii yetu kwao haijalishi. Ni watu ambao wameweka mbele maslahi yao binafsi kuliko maendeleo ya pamoja ya nchi yetu. Watu kama hao wanatakiwa kwanza waadhibiwe vibaya sana kiasi kwamna hata wengine watakao pata nafasi zao baada ya wao kung'olewa, isiwe rahisi kufikiria kufanya maovu ya aina hiyo. Majina yao yawekwe kwenye records za serikali ili wasipate tena nafasi za ajira kwenye mashirika ya umma.
Hali kama hii itakuwa pia ni fundisho kwa vizazi vyao nao watakapo kuja pata nafasi kwenye positions kama hizo ili itapo fikia wakati wa kutaka kutekeleza maovu hayo hayo ya ubadilifu wa mali za umma, kumbukumbu za mateso ya maisha waliyo yapata wakati wazazi wao walipo pata pigo la aina hiyo ziwajie na kuchukua mamamuzi ya kutotenda uhaini huo. Vinginevyo itakuwa ni matatizo ambayo yatakuwa yana jirudiarudia kila mara na hivyo kuchangia kufa kwa mashirika ya umma kama ilivyo kuwa huko nyuma.
Hili gonjwa la utumbuaji Jiwe ametuachia janga baya sana.Kwani ni lazima kujipausha kisiasa kutumbua watu,kwanini utawala wa sheria usichukue mkondo wake?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.