Waziri Mkuu Kassim Majaliwa avamia mwendokasi, ahoji mapato yalipo kama wanashindwa kununua mabasi. Mkurugenzi wa fedha atumbuliwa

Mradi huo hapo awali kabla ya uliyemtaja hapo, ulikuwa ni Mradi wa serikali Jina tu,

Tanzania nchi ngumu hii
 
Mama amesema yeye na Magufuli ni kitu kimoja.
Ila ataendeleza yale mema.
Tutegemee mwendo kasi kufufuka.
 
Reactions: BAK
Aliyewabatiza Chadema nyumbu aliona mbali ni mijitu mijinga isiyojitambua kabisa
 
Vitu vingi tu ambavyo vilikuwa ni Vya serikari Jina tu, Ila mwenyewe ni mtu Ka watu wengine,

Hahahahaaa!! Kama bandarini pale Ile floor meter ilikuwa ni Mali ya serikali Jinaa!! Kwamba mafuta yanaingia pale, badala ya mita kuhesabu Lita ngapi zimepita hapo!! Kumbe yalishachepushwa na yanapita tu bila Kodi, ni Kwa miaka mingapi, haijulikani

Kama Hilo liliwezekana, ni kipi kisichowezekana kuwa mikononi mwa watu badala ya serikalini?
 
Ndio maana sa hivi ukienda kupanda unapewa tiketi ishachanwa tayari ina maana umepewa used ni vile tuu na sisi wabongo hatuna utaratibu wa kuhakiki muda na tarehe huenda tumeliwa sana mae ma zao
 
Hamna tapeli mkubwa kama huyo kisena,shukran kubwa ujio wa magu bila hivyo tungepanda hizo bus kwa elfu 2,huyo kisena fisadi aliuua gari za kwenda ferry akawa anaenda peke yake na route yake ilikua inaanzia mnazi mmoja,ingekua china kisena ashanyongwa kitambo tu
 
Haukupaswa kuwa mradi serikali kabisa.
Ilpaswa iwe ni biashara ya sekta binafsi.
Mradi huo hapo awali kabla ya uliyemtaja hapo, ulikuwa ni Mradi wa serikali Jina tu,

Tanzania nchi ngumu hii
 
Kisena alikuwa kwenye mradi kifisadi. Hivyo ilikuwa sawa kumuondoa. Labda tuseme hakutafuta solution nzuri.
 
Huu mradi walioua ni UDART wenyewe, DART kama msimamizi na NMB kama Fund Manager.

1. UDART alitakiwa kumlipa mwenye mfumo,Maxmalipo hakulipa. Yale mageti yakawa hayana kazi tena maana UDART alikuwa hana access ya kufanya chochote ndio maana akasema ataunda mfumo wake mpya wa tiketi kupitia TTCL nadhani au eGa.

2. DART kama mamlaka ya serikali alikubalije UDART kupiga u-turn na kusema atakuja na mfumo mpya na kuanza kukusanya nauli kweny ndoo (cash) na zikawa haziendi Bank

3. NMB kama fund manager alikubalije kuona account zilizofunguliwa kuendesha mradi zikiwa hazina miamala. Zile account ndio zilikuwa zinatumika kugawa revenues kwa stakeholders wote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…