Waziri Mkuu Kassim Majaliwa: Rais Magufuli ni mzima na anachapa kazi. Wanataka atoke, atoke aende wapi? Kariakoo au Magomeni?

Hata kama mtu unamchukia kikubwa lakini kumvumishia kifo ni ushetani kabisa. Tena Rais wa nchi? Tuwe waungwana.
Kwani kifo ni ushetani ama ni adhabu?

Binadamu tuliopo hapa Duniani lazima tutafariki Dunia.

Kwenye sala zangu kila siku namwomba Mungu anipe maisha marefu hapa Duniani hadi uzeeni nikiwa na nguvu zangu, siku yangu ikifika anipe kifo chema na roho yangu aipumzishe mahala pema peponi Mbinguni.


Sent from my HTC U12 life using JamiiForums mobile app
 
Hata kama mtu unamchukia kikubwa lakini kumvumishia kifo ni ushetani kabisa. Tena Rais wa nchi? Tuwe waungwana.
Ndugu yangu kaa kimya acha kuwasaidia wajinga. Kuna watu wanajitabiria vifo vyao wao wenyewe na vitatokea muda siyo mrefu. Kaa kimya, waache
 
Duuu. What???

Aisee. Naona Mimi niko nje ya media. Mtu unathubutuje kuandika hizi propaganda? Kwa hiyo wakae na maiti mpaka leo Jumatatu 15 March? Aibu zenu
Zenu nani? Mimi nimekupa taarifa tu.

Pia, kwani nani kakwambia wamekaa na maiti?
 
Watoto: Mama baba yupo wapi?

Mama: Baba yenu yupo, anawasalimia sana anasema msome kwa bidii.

Watoto: Yupo wapi, mbona hatumuoni hata sebuleni wakati wa kula!

Mjomba: Mnamtaka baba yenu ashinde anazurula kama nyie au muende nae shule kila siku aache kiwatafutia chakula na ada?

Mama: Atakayeniuliza hilo swali tena ntamchapa fimbo na nitamnyima chakula

Watoto: [emoji848][emoji848][emoji847]

Mama & Mjomba: [emoji53][emoji29][emoji25][emoji21]

This is Hadrianus


Hivi nyie Moderator kwanini mmeunganisha uzi wangu na mambo ya Kassim Majaliwa?
 
Duuu. What???

Hivi Mr Mzungu nadharia ya Nairobi & India haiadvoketi tena, maana naona now kahamia Halotel --- stroke and sijui what what hukooo!??? Mr Confusion-in-Chief!!! Ama kweli ukianzisha uzi mmoja wa uongo lazima tu uanzishe uzi mwingine na mwingine na mwingine tena ili kila uzi ufunike ule uliotangulia, but where!

Yaani uzi wa uongo unakuwa mreeeeefuuuuu kama urefu wa reli & treni yetu ya umeme & mwendokasi. Asante na heko kubwa awamu ya 5 maana sasa Tanzania inakuwa zaidi ya Ulaya. Lazima Borris Johnson this time aje apangishe Ghetto Kigamboni ama Tanga!
 
wana jf ukifuatilia mitandao ya kijamii kwa sasa issue kubwa ni juu ya mpendwa wetu JPM lakini nimekuja kugundua kuwa wapinzani hapa nchini wanampenda zaidi raisi wetu maana hawalali wanakesha kusikiliza atazungumza muda gani.

Niwatoe hofu tu kwambakama mama yetu Samia na Waziri mkuu walivtotuambia mpendwa wetu yupo salama na tusiwenahofu ambayo wapinzani kwa upendo wao kwa rais mengine wanazushayakipuuzi

Nawasilisha
 
Ukiona mtu anazungumziwa sana jua kuna mawili

Anapendwa sana au anachukiwa sana....

Je unayemzungumzia anaangukia kwenye kundi gani?
Kama anachukiwa huwezi kumzungumzia kiasi hicho huyu ni kipenzi cha watu ndiyo maana wapinzani wanahaha tena walikuwaga wanajifanya eti hawamtambui leo hii wanamuita Rais wetu yuko wapi yaani wamemkubali
 
Watu wanachotaka kujua ni kitu kimoja tu! Yuko wapi? Na kama anaumwa, dhambi iko wapi Watanzania na dunia ikifahamu jambo hilo?
Tatizo mnakiherehere sana, Rais wetu mpendwa ni mzima hana tatizo kama viongozi wanavyosema sasa nyinyi mnataka taarifa kutoka kwa nani hebu sema wewe unataka nani atokee akuambie?
 
tatizo mnakiherehere sana rais wetu mpendwa ni mzima hana tatizo kama viongozi wanavyosema sasa nyinyi mnataka taarifa kutoka kwa nani hebu sema wewe unataka nani atokee akuambie?
Kwani siku zote ni nani aliyekuwa akimsemea? Si ni yeye mwenyewe!! Kama hao wapinzani wanasema uongo, si ajitokeze basi akiwa ni mzima wa afya ili wapatwe na aibu?

Lakini kwa aina hii ya ukimya, iwapo atajitokeza baada ya wiki 3, watu wataamini kile kilichosemwa na wapinzani. Na kama kweli haumwi, kwanini wananchi wanao hoji wakamatwe?
 
Hivi hata wewe ukiamua kupumzika, hutaki mawasiliano na mtu kwa uamuzi wako mwenyewe majukumu ukawaachia wasaidizi wako nani atakutafuta, acheni kiherehere yaani mnakuja kuumbuka vibaya nyau nyie.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…