Waziri Mkuu Kassim Majaliwa: Rais Magufuli ni mzima na anachapa kazi. Wanataka atoke, atoke aende wapi? Kariakoo au Magomeni?

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa: Rais Magufuli ni mzima na anachapa kazi. Wanataka atoke, atoke aende wapi? Kariakoo au Magomeni?

Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa, amewataka watanzania wawapuuze Wapotoshaji wa mitandaoni wanaotaka kuleta taharuki juu ya Afya ya Rais Magufuli "Rais ana shughuli nyingi, Wanataka atoke aende wapi, Kariakoo au Magomeni tangu lini?"

Leo Asubuhi wakati nakuja huku nimeongea nae kwa simu na ameniagiza niwaambie wana Njombe kuwa anawapenda sana na anawashukuru sana kwa kura nyingi mlizompigia

Kuna wenzetu hawaishi hapa nchini, wao kazi yao ni kutuombea mabaya tu, kupandikiza chuki tu. Sasa unamuombea mwenzako kufa hiyo ni akili kweli?. Nawatoa hofu watanzania, Rais wenu yuko imara anafanya kazi zake kama kawaida za ofisini

Tuhakikishe tunamuabudu Mungu, tunamuomba Mungu katika kila jambo, tunamtegemea Mungu katika kila jambo, hata asubuhi nilivyokuwa natoka Dodoma nimempigia kumjulisha ratiba yangu, hata juzi alikuwa anajua ninakuja akanituma, wasalimie wana Njombe na nilitoa Salam.

Naomba nirudie, kwa salam alizotupa leo kweli wana Njombe, mheshimiwa Rais anawasalimia sana wana Njombe, mheshimiwa Rais anawashukuru wana Njombe.

Chanzo: Jamvi la Habari
Kama mlisema corona hamna kwani mna shindwa nini kusema Jiwe ni mzima?
Subirini arudishwe kwenye box ndiyo mtuambie ana afya njema.
 
Kama ni kweli kwanini Raisi ,wenyewe asitoke na kusimama ikulu mpaka tunafika huku. Wanataka wamlete akipata nafuu kama vile hajaondoka wakati waganga wa Nairobi ndiyo walisema yupo pale. Huu ni utamaduni wa uongo uliopo kwenye uongozi huu. Haya ni mapungufu makubwa ya serikali

Hivi nyinyi mnao mbishia hata Waziri mkuu mna lengo gani?
 
Kwani mangapi mlishasema na mwisho anatoka mzima na mnakosa kulejesha taarifa zenu?
Wote mnao ongea hamna uwezo wa kwenda ikuru ila mnajifanya mna taatifa za mtu wa ikuru kwa mtizamo wenu.

Kama mnampenda basi anzeni kumpa heshima yake na sio vijembe vyenu.
Kwanza kabisa ni kurejesha sio kulejesha, taarifa na sio taatifa, ikulu sio ikuru. Hivi ulipata wapi elimu yako?
Pili, hivi wewe ukiwacha mapenzi yako ya ccm, tuseme uko sasa jembe amesingiziwa kuwa anaumwa sasa kwa nini anashindwa kuja hadharani kukanusha? Hivi wewe rais wako hajahudhuria mkutano wa EAC, hajaonekana kanisani (ambako anakwenda kila jumapili bila kukosa) jumapili mbili, hajahudhuria hafla yeyote ile kwa wiki tatu (si kawaida yake) na bado unaona kuwa ni kosa watu kuuliza cha mno?

Tumia bongo lako! utabaki hadi lini kufanya jinga la mji?
 
Mjomba wako ni tapeli mchunguze vizuri utagundua
Mjomba wangu ni afisa kipenyo mwandamizi kuna jambo zito kaniambia.

Waziri mkuu kama anabisha amwambie Magufuli anyooshe kidole juu ama afanye kama anajikuna halafu apigwe picha.
 
Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa, amewataka watanzania wawapuuze Wapotoshaji wa mitandaoni wanaotaka kuleta taharuki juu ya Afya ya Rais Magufuli "Rais ana shughuli nyingi, Wanataka atoke aende wapi, Kariakoo au Magomeni tangu lini?"

Leo Asubuhi wakati nakuja huku nimeongea nae kwa simu na ameniagiza niwaambie wana Njombe kuwa anawapenda sana na anawashukuru sana kwa kura nyingi mlizompigia

Kuna wenzetu hawaishi hapa nchini, wao kazi yao ni kutuombea mabaya tu, kupandikiza chuki tu. Sasa unamuombea mwenzako kufa hiyo ni akili kweli?. Nawatoa hofu watanzania, Rais wenu yuko imara anafanya kazi zake kama kawaida za ofisini

Tuhakikishe tunamuabudu Mungu, tunamuomba Mungu katika kila jambo, tunamtegemea Mungu katika kila jambo, hata asubuhi nilivyokuwa natoka Dodoma nimempigia kumjulisha ratiba yangu, hata juzi alikuwa anajua ninakuja akanituma, wasalimie wana Njombe na nilitoa Salam.

Naomba nirudie, kwa salam alizotupa leo kweli wana Njombe, mheshimiwa Rais anawasalimia sana wana Njombe, mheshimiwa Rais anawashukuru wana Njombe.

Chanzo: Jamvi la Habari
Angempigia Hapo hapo kumjulia hali. Mbona kwenye kampeni walikuwa wakiongea mubashara.
Kauli ya leo imetoa taarifa Rais anaumwa. Siku wakija kusema anaumwa tujue kuwa atakuwa amefariki.
 
Very clear bila hata chenga, mmepata picha kamili kuna chuki kubwa dhidi ya serikali yetu. Mnaweza mkadhania mtego wenu kujua nani anawachukia umefanikiwa lakini ukweli utabaki kuwa mnachukiwa.

Mnachukiwa na waliojeruhiwa na vyombo vya dola, walionyimwa haki ya nyongeza ya mishahara, wapo wanaodai kuporwa uchaguzi. Wapo ambao ndugu zao wameuliwa bila makosa. Wapo ambao wamebaki kuwa vilema.

Ukweli ni kuwa mnachukiwa tena chuki mbaya sana. Msidhani ni chuki za walio nje ya nchi tu. Bali wengi walio ndani hapa Tanzania wanawachukia.

Sidhani kama mna muda wa kujirekebisha, labda.
 
Back
Top Bottom