Waziri Mkuu Kassim Majaliwa: Rais Magufuli ni mzima na anachapa kazi. Wanataka atoke, atoke aende wapi? Kariakoo au Magomeni?

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa: Rais Magufuli ni mzima na anachapa kazi. Wanataka atoke, atoke aende wapi? Kariakoo au Magomeni?

Kiswaswadu mwongo sana mbaya zaidi anasema uongo akiwa msikitini
Eti Kiswaswandu😁😁🤣🤣😅,dah watu mna maneno jamani,kweli inatakiwa ukiwa mwanasiasa hutakiwi kuwa na hasira,maana na kazi yangu hii halafu uniite hilo jina wallah zitawaka ngumi sio za nchi hii...
 
Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa, amewataka watanzania wawapuuze Wapotoshaji wa mitandaoni wanaotaka kuleta taharuki juu ya Afya ya Rais Magufuli "Rais ana shughuli nyingi, Wanataka atoke aende wapi, Kariakoo au Magomeni tangu lini?"

Leo asubuhi wakati nakuja huku nimeongea naye kwa simu na ameniagiza niwaambie wana Njombe kuwa anawapenda sana na anawashukuru sana kwa kura nyingi mlizompigia

Kuna wenzetu hawaishi hapa nchini, wao kazi yao ni kutuombea mabaya tu, kupandikiza chuki tu. Sasa unamuombea mwenzako kufa hiyo ni akili kweli? Nawatoa hofu watanzania, Rais wenu yuko imara anafanya kazi zake kama kawaida za ofisini.

Tuhakikishe tunamuabudu Mungu, tunamuomba Mungu katika kila jambo, tunamtegemea Mungu katika kila jambo, hata asubuhi nilivyokuwa natoka Dodoma nimempigia kumjulisha ratiba yangu, hata juzi alikuwa anajua ninakuja akanituma, wasalimie wana Njombe na nilitoa Salamu.

Naomba nirudie, kwa salam alizotupa leo kweli wana Njombe, mheshimiwa Rais anawasalimia sana wana Njombe, mheshimiwa Rais anawashukuru wana Njombe.

Aise,uovu ni kitu kibaya sana,unafiki ni mbaya sana.Yaani jamaa macho makavu kabisa,wala hajisikii vibaya hata kidogo,anatafuna uketo tu.Duh!So hawa ndio wanaotaka tuwaamini kwenye zengwe la DP World.Eti mtuamini,tuwaamini ninyi Mungu.Kama mlitudanganya kwenye kifo cha Magufuli,hamna ukomo wa kudanganya ninyi,we cannot believe you in anything.
 
"Kuanzia Juzi hata leo asubuhi nimeona Watanzania wenzetu wenye husda, tena hawako ndani ya Nchi wako huko, wanashawishi Vyombo vya Kimataifa viseme ‘Rais wa Tanzania anaumwa, kajifungia’, tena hawako hapa, wapo huko, tulioko ndani tuko kimya, ni husda”-Waziri Mkuu Majaliwa akiwa Njombe leo

"Watanzania mtulie uongozi wenu upo,Rais Magufuli anaendelea vizuri, kumzushia ugonjwa ni chuki tu, inawasaidia nini?, ‘atoke’, atoke aende wapi?, ‘aje’ aje afanye nini?, umeshamkuta Rais siku moja anazurura kariakoo?, Rais ana mipango yake ya kazi sio Mtu wa kuzurura”-MAJALIWA

"Juzi tu Rais alikuwa Chato akatoka akaenda Kahama, Tabora, Dodoma, akarudi DSM, juzi kaapisha mnataka tena azunguke Nchi nzima, sisi tunafanya nini?, nini umuhimu wa kuwa na Wasaidizi!, azunguke yeye tena Nchi nzima kweli?”- MAJALIWA

#MillardAyoUPDATES

Mie siongezi chochote....
 

Attachments

  • IMG-20231012-WA0172.jpg
    IMG-20231012-WA0172.jpg
    38 KB · Views: 1
Back
Top Bottom