Waziri Mkuu Kassim Majaliwa: Rais Magufuli ni mzima na anachapa kazi. Wanataka atoke, atoke aende wapi? Kariakoo au Magomeni?

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa: Rais Magufuli ni mzima na anachapa kazi. Wanataka atoke, atoke aende wapi? Kariakoo au Magomeni?

Sio Kila ukweli ni wa kutamka hadharani.
Hata kama hilo ni kweli, bado halimaanishi ilikuwa lazima adanganye kijinga kwa namna ambayo inawezekana kujulikana kirahisi kwamba alidanganya.

Uongo ule unaonesha kuwa Majaliwa akili yake fupi, hafikirii vitu tofauti vinavyoweza kutokea na yeye atakavyoonekana.

Viongozi kama hawa ndio wanatuingiza kwenye mikataba mibovu kwa sababau hawana uwezo wa kuchart all possible scenarios na kuchukua the best course of action.

Kwani Majaliwa angekaa kimya mpaka muda useme angepungukuwa nini? Kulikuwa na ulazima gani wa kudanganya vile pale msikitini?

Sasa hivi kila kauli atakayotoa Majaliwa ya kutaka kujionesha anatuasa kiukweli naiwekea shaka, najisema huyu ndiye mtu aliyetuambia Magufuli yuko mzima anachapa kazi Ikulu, wakati ni mgonjwa mahututi anajifia. Kama kadanganya kwenye hili, tena yeye Muislamu, akiwa msikitini, anatudanganya kwenye mangapi mengine?

Amana, trust, ni kitu kigumu sana kuki maintain, na kikiharibiwa kurudi ni kazi sana.

Kwenye nchi ya watu wanaotumia mantiki na akili Majaliwa alitakuwa kujiuzulu kwa kauli ile.

Bahati yake Tanzania watu wengi hawatumii mantiki wala akili, wanakwenda kwa wanachokiita kudura za Mungu tu.
 
Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa, amewataka watanzania wawapuuze Wapotoshaji wa mitandaoni wanaotaka kuleta taharuki juu ya Afya ya Rais Magufuli "Rais ana shughuli nyingi, Wanataka atoke aende wapi, Kariakoo au Magomeni tangu lini?"

Leo asubuhi wakati nakuja huku nimeongea naye kwa simu na ameniagiza niwaambie wana Njombe kuwa anawapenda sana na anawashukuru sana kwa kura nyingi mlizompigia

Kuna wenzetu hawaishi hapa nchini, wao kazi yao ni kutuombea mabaya tu, kupandikiza chuki tu. Sasa unamuombea mwenzako kufa hiyo ni akili kweli? Nawatoa hofu watanzania, Rais wenu yuko imara anafanya kazi zake kama kawaida za ofisini.

Tuhakikishe tunamuabudu Mungu, tunamuomba Mungu katika kila jambo, tunamtegemea Mungu katika kila jambo, hata asubuhi nilivyokuwa natoka Dodoma nimempigia kumjulisha ratiba yangu, hata juzi alikuwa anajua ninakuja akanituma, wasalimie wana Njombe na nilitoa Salamu.

Naomba nirudie, kwa salam alizotupa leo kweli wana Njombe, mheshimiwa Rais anawasalimia sana wana Njombe, mheshimiwa Rais anawashukuru wana Njombe.

Ukisoma katikati ya mistari unaona kabisa kulikuwa na jambo sema wakawa wanapambana kulificha ndiyo maana wakatumwa mikoa ya mbali wasijue mipango mingine.
 
Back
Top Bottom