Waziri Mkuu wa Sweden akataa wito wa upinzani wa kutaka Sweden ijiunge NATO, asema hilo litaleta machafuko na kuharibu amani

Hili baba linaogopa nini wenzie wasijiunge na nato
Asichotaka Russia NATO kuja kuweka kambi zao na makombora ya USA Ukraine kwa usalama wa nchi yake na sababu hyo ndio iliyomfanya usa akatae pia Russia pia kuweka makombora yake Cuba na mgogoro ulikuwa mkubwa hila ulitatuliwa kabla ya vita kuanza
 
Mkuu upo mjini Moscow katika kitongoji gani hapo, wenye akili wanajua NATO ndio kuna usalama.
 
Sweden wanapaswa kujiamini kwa hali ya sasa ya NATO ni kimbilio, Ukrain sasa wanapiga mzigo wakishinda vita watakuwa wamejikombo kutoka kwa dikteta Putini, nchi yao itakuwa huru zaidi na watakuwa na uwezo wote kujilinda kwa amani zaid
 
Asichotaka Russia NATO kuja kuweka kambi zao na makombora ya USA Ukraine kwa usalama wa nchi yake na sababu hyo ndio iliyomfanya usa akatae pia Russia pia kuweka makombora yake Cuba na mgogoro ulikuwa mkubwa hila ulitatuliwa kabla ya vita kuanza
Na kwa nini tanganyika tunaogopa kuvunja muungano wa tanganyika na zanzibar
 
Watengeneza scania na volvo kumbe wanaogopa makombora.
Hata watengeneza Nokia finland nao wapo kwenye kitimoto.
Mi naona hapo ulaya wangeunda umoja wao wa kujihami bila kuwepo marekani maana marekani ndo mrusi hamtaki
Wana hadi ndegevita zao kitambo hawategemei USA wala Russia
 
Sweden wanapaswa kujiamini kwa hali ya sasa ya NATO ni kimbilio, Ukrain sasa wanapiga mzigo wakishinda vita watakuwa wamejikombo kutoka kwa dikteta Putini, nchi yao itakuwa huru zaidi na watakuwa na uwezo wote kujilinda kwa amani zaid
Nimesikia umasema "Ukraine akishinda vita" au?
 
Hao Sweden na Finland asilimia kubwa ya wananchi wao wanataka nchi zao zijiunge na Nato kwani hata wenyewe wameshaelewa usalama wao utakuwepo tu kama watajiunga na Nato.

Hao Estonia, Latvia na Lithuania ambao huko nyuma walikuwa kwenye muungano wa Kisovieti tayari walishaliona hilo na kujiunga na Nato.

Ikumbukwe kwamba nchi za Finland na Sweden hata kijamii hawako karibu na warusi kwani wakati wafinland ni Ural Altai na wasweden ni Teutons, warusi ni jamii ya Slavs hivyo wako mbalimbali kabisa.

Kama ni ukaribu basi warusi jamii ambao wako nao karibu kabisa ni wabelarus, waukraine, wapoland, waczech, waslovakia, waboznia, waslovenia, wamacedonia, waserbia na wacroatia kwani wote ni jamii ya wa-slavs na hata lugha zao na tamaduni zinashabihiana mno.

Itakumbukwa kwamba jamii hizo ambazo ziko karibu na warusi kuna wengine tayari walishajiunga na Nato na hata hao wengine ambao bado hawajajiunga kama hao wa iliyokuwa Yugoslavia ya zamani karibu wote wameshatuma maombi kuomba kujiunga na Nato.

Kitu ambacho Russia inapaswa kujiuliza sana ni kwa nini mataifa karibu yote ya Ulaya yanapenda kujiunga na Nato na kwa nini wenyewe wanabaki na wabelarus tu..??!! Lazima kuna tatizo kubwa sana kwa upande wa Russia ndio maana wenzake wanamuona kama Pariah.

Kuna mataifa mengi tu ya Ulaya mashariki ambayo wakati wa vita baridi walikuwa upande wa Urusi na muungano wao ukijulikana kama Warsaw Pact lkn baada ya Marekani kuisambaratisha USSR na Warsaw Pact kufa hayo mataifa yalitengana na USSR na ndipo wengi wao wakaamua kujiunga na Nato na kuachana na ubabe wa warusi kitu ambacho Putin anakipinga hadi leo. Tutaendelea.
 
Wivu wa nini?! Kama vipi Russia naye ajiunge NATO aache wivu wa kike.
 
Marekani kamwambia sweden Bonyeza *100*01# kujiunga na NATO😂😂


Russia Kamtumia sms sweden kamwambia hio huduma itakugharimu😜😜Jiunge nikupasue
 
Na zanzibar ijiamini isitake muungano uone itakavyokuwa kama ukraine
Sweden wanapaswa kujiamini kwa hali ya sasa ya NATO ni kimbilio, Ukrain sasa wanapiga mzigo wakishinda vita watakuwa wamejikombo kutoka kwa dikteta Putini, nchi yao itakuwa huru zaidi na watakuwa na uwezo wote kujilinda kwa amani zaid
 
Marekani kamwambia sweden Bonyeza *100*01# kujiunga na NATO[emoji23][emoji23]


Russia Kamtumia sms sweden kamwambia hio huduma itakugharimu[emoji12][emoji12]Jiunge nikupasue
Atapigana na Nchi ngapi¿????????
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…