Waziri Mwigulu: Serikali itakopa Tsh. Trilioni 8.69 kwaajili ya Bajeti ya mwaka 2024/25

Waziri Mwigulu: Serikali itakopa Tsh. Trilioni 8.69 kwaajili ya Bajeti ya mwaka 2024/25

Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema serikali inatarajia kukusanya na kutumia TZS trilioni 47.4 katika bajeti ijayo. Mapato ya ndani yanatarajiwa kuwa TZS trilioni 34.4, washirika wa maendeleo wanatarajiwa kuchangia TZS trilioni 4.29 na mikopo ni TZS trilioni 8.3.

Mwigulu amesema hayo bungeni akiwasilisha mapendekezo ya mwongozo wa maandalizi ya mpango wa bajeti ya mwaka 2024/25.
Naona Taratibu Serikali imeanza kupunguza kiwango Cha mikopo
 
Haya madeni yatatuua, yule Mgogo alisema ukweli hawa Wanyiramba hata huruma hawana.

Na sasa wanamshambulia Mpina na kwa taarifa yenu huo uchawi wa Kiomboi haufui dafu kwenye mizizi ya Gambosh.
Yaliwahi kumuua nani?
 
Unamsema hivyo waziri wa fedha
Na ndiyo maana nimeanza na simtusi!

Pengine kama una maneno mengine yenye ujumbe huo huo nipatie ndugu mtanzania mwenzangu. Nita edit tu! Ila dhumuni langu ni kufikisha ujumbe wa namna hiyo!
 
Bila chuki wala hiyana, huyu Mh. anayeitwa Mwigulu Nchemba sijawahi kumkubali.

Ukitazama kikao kilichofanyika baina ya serikali na wafanyabiashara wa Karia Koo huyu jamaa ana uelewa mdogo sana!

Yaani ni mtupu kabisaaaaa! Ni kiburi tu cha chama Tawala ndicho kinachomlinda.
Mbona hujaeleza huo uelewa wake mdogo ulivyo na uelewa wako mkubwa Ili tulinganishe?

Kutomkubali wewe Wala sio tatizo na sio lazima umkubali so long as amekuwa Waziri Bora zaidi qa Uchumi wa miaka ya karibuni
 
Kwa mtazamo wangu ,ipo haja kubwa sana Kwa serikali kibuni njia mbadala wa kupata fedha ambazo zitaweza kujitosheleza kwenye budget ya Taifa na si kukopa kila mara. Kwa sasa ianze kulipa deni la Taifa kwani limekuwa kubwa sana ili kuepusha ongezeko la kila mwaka.
Mbona tunvyo vyanzo vingi tu hapa kwetu ,mbuga za wanyama,maziwa,migodi,gesi,makaa ya mawe nk.
Kwanza hujui uchumi,Kwa taarifa Yako tuu Kwa Serikali kukopa ni lazima na Nchi zoooote Duniani zinakopa Kwa sababu kukopa ni tool ya economic regulation.

Kwa hiyo usitoe maoni ya mambo ya uchumi kama hujui ndio maana hata wenye surplus budget wanakopa.

Mwisho angalia mapato ya ndani yatakuwa zaidi ya 34T ,Ongezeko la 3T.

Hilo Ongezeko litatokana na vyanzo vipya za Kodi na sio Mikopo.
 
Kwa mtazamo wangu ,ipo haja kubwa sana Kwa serikali kibuni njia mbadala wa kupata fedha ambazo zitaweza kujitosheleza kwenye budget ya Taifa na si kukopa kila mara. Kwa sasa ianze kulipa deni la Taifa kwani limekuwa kubwa sana ili kuepusha ongezeko la kila mwaka.
Mbona tunvyo vyanzo vingi tu hapa kwetu ,mbuga za wanyama,maziwa,migodi,gesi,makaa ya mawe nk.
Unajua changamoto tuliyonayo ni kuwa ni lazima tukubali tuna viongozi wenye walakini wa kutumia akili zao vizuri.

Mimi ninachokiona wanendesha nchi kimazoea. Hawana akili ya kufikiria kabisa bali ni mazoea tu ndiyo yanayowafanya kuendesha nchi! Kwamba tutakopa! Tutakopa! Tutakopa!
 
Hao washirika wa maendeleo waliwaambia watatoa hicho kiasi, au ni wishful thinking ya Mwigulu na Samia?

Kama wasipotoa tunarudi kule kwenye nakisi ya bajeti, matokeo yake pesa hazitafika mawizarani kama ambavyo wizara husika ziliomba..

Baada ya hapo ni mkwamo, miradi kadhaa haitasogea, licha ya serikali hiyo hiyo kuwa tayari ilishakopa trilioni kadhaa kwa ajili ya kuongezea kwenye bajeti hiyo hiyo..

Umaskini ni mbaya asikwambie mtu, unaweza kuwa na shida ya kiasi fulani cha pesa, ukaomba ukaomba lakini bado usipate kile ulichohitaji, bado ukaamua na kukopa kabisa, lakini bado kuna baadhi ya mambo yako hayatasogea!.

Lakini ajabu ya karne sasa, utakuta viongozi hao hao wanaoshuhudia huo mkwamo, bado wanatoa pesa nyingi kwaajili ya kununua v8 zenye viyoyozi ili ziwape raha wakiwa safarini, hapa ndipo utatambua kama taifa tu maskini wa akili pia.
Machadema Huwa ni majinga sana.Juzi tuu hapo mumesikia taarifa ya IMF kuongezea Serikali Dola mil.150 na kufanya budget support kutoka imf pekee kuwa Dola Milioni 452 sawa na zaidi ya 1Tr na Kila mwaka wanatoa Kwa sababu ni commitment ya lazima.

Na kama umesikiliza taarifa ya serikali Bajeti iliyoishia wahisani wametoa 97% ya ahadi zao huku makusanyo ya serikali yakiwa 93% ya lengo.

Commitments za wahisani sio lazima zije in terms of cash Bali huja Kwa support ya program Moja kwa Moja.

Mwisho Nchi zooote bazo ziko kwenye kundi la Lower Middle Income zinasaidiwa na wahisani ikiwemo Kenya zaidi ya 15% ya Bajeti Yao ni wahisani.
 
naombeni nieleweshwe kidogo,hivi deni la ndani mkopeshaji anakuwa ni nani?,na deni la nje mkopeshaji ni nani?
Nje mkopeshaji zinakuwa taasisi eg WB,Imf, AFDB,Mabenki ya kibiashara,Nchi mbalimbali mfano Tanzania Ina deni kubwa zaidi na Iran.

Mkopeshaji wa ndani ni kama umewahi sikia Serikali inauza bonds pale taasisi za Fedha eg banks na mifuko ya pensions ndio hukopesha Ili baadae wake kupata faida.
 
Unajua changamoto tuliyonayo ni kuwa ni lazima tukubali tuna viongozi wenye walakini wa kutumia akili zao vizuri.

Mimi ninachokiona wanendesha nchi kimazoea. Hawana akili ya kufikiria kabisa bali ni mazoea tu ndiyo yanayowafanya kuendesha nchi! Kwamba tutakopa! Tutakopa! Tutakopa!
Wewe mwenye akili tuwekeeni hapa mawazo yako tuone hizo akili zako na Ili Serikali ijifunze.
 
Aisee hata Burundi watatukataa sasa,haya chama letu ni ile ilee ameen👐
 
Mbona hujaeleza huo uelewa wake mdogo ulivyo na uelewa wako mkubwa Ili tulinganishe?
Ndugu mtanzani, kwanza tufahamu kukosoa si dhambi, kukosoa si chuki, kukosoa si jinai!

Na sijamtusi, kama uwasilishaji wangu unaona wenye kukwaza nipatie maneno yaliyo bora zaidi lakini yaliyobeba ujumbe huo huo.

Tukirudi kwenye suala uliliuliza majibu yake yapo dhahiri kabisa! Ukweli mwepesi ni kile kikao kilichofanyika baina ya serikali na wafanyabiashara wa Karia Koo.

Tafuta video za mkutano huo zipo youtube kisha utapata taswira kamili.
 
Ndugu mtanzani, kwanza tufahamu kukosoa si dhambi, kukosoa si chuki, kukosoa si jinai!

Na sijamtusi, kama uwasilishaji wangu unaona wenye kukwaza nipatie maneno yaliyo bora zaidi lakini yaliyobeba ujumbe huo huo.

Tukirudi kwenye suala uliliuliza majibu yake yapo dhahiri kabisa! Ukweli mwepesi ni kile kikao kilichofanyika baina ya serikali na wafanyabiashara wa Karia Koo.

Tafuta video za mkutano huo zipo youtube kisha utapata taswira kamili.
Sasa kwani majibu yake yalikuwa na shida gani kwako? Ukisema huyu hamna kitu lazima utuoneshe kitu chako Bora kushinda yeye tofauti na hapo ni chuki binafsi.
 
Wewe mwenye akili tuwekeeni hapa mawazo yako tuone hizo akili zako na Ili Serikali ijifunze.
Ndugu, mimi ni mtanzania pia! Ni raia wa hii nchi. Na nalipa kodi! Nachangia pato la ujenzi wa Taifa letu.

Sipo kwa utimu, sipo kwa mechi! Nipo kitaifa.
 
Sasa kwani majibu yake yalikuwa na shida gani kwako? Ukisema huyu hamna kitu lazima utuoneshe kitu chako Bora kushinda yeye tofauti na hapo ni chuki binafsi.
Huo ni mtazamo wako na siupingi.

Kipi kinifanye niwe na chuki na Mwigilu?!

Mimi ni muslim ndugu! Kwetu ukosoaji ni suala la kawaida. Kama kwenu ukosoaji una hesabika ni chuki, kwetu mantiki yake ni kuupata usawa!
 
Huo ni mtazamo wako na siupingi.

Kipi kinifanye niwe na chuki na Mwigilu?!

Mimi ni muslim ndugu! Kwetu ukosoaji ni suala la kawaida. Kama kwenu ukosoaji una hesabika ni chuki, kwetu mantiki yake ni kuupata usawa!
Kipi ulichokosoa na kuonesha njia mbadala zaidi y kuja na conclusion Yako?
 
Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema serikali inatarajia kukusanya na kutumia TZS trilioni 47.4 katika bajeti ijayo. Mapato ya ndani yanatarajiwa kuwa TZS trilioni 34.4, washirika wa maendeleo wanatarajiwa kuchangia TZS trilioni 4.29 na mikopo ni TZS trilioni 8.3.

Mwigulu amesema hayo bungeni akiwasilisha mapendekezo ya mwongozo wa maandalizi ya mpango wa bajeti ya mwaka 2024/25.
Lazima tukope vinginevyo utashindwa kuendesha Singida big stars
 
Ndugu, mimi ni mtanzania pia! Ni raia wa hii nchi. Na nalipa kodi! Nachangia pato la ujenzi wa Taifa letu.

Sipo kwa utimu, sipo kwa mechi! Nipo kitaifa.
Weka mawazo Yako Bora badala ya kuishia kutukana na kulaumu.

Wapi nimesema wewe ni Mzambia? Shida ya Wabongo ndio hii mdomo ila solution zero.

Ndio maana mara nyingi Huwa nasema chama Cha Upinzani Cha ukweli hapa Tanzania ni ACT,sio tuu wanakosoa bali they offer an alternative,nyie wengine ni wapiga domo tuu.
 
Hayo madeni bila shaka yanajumulisha na yale matrilioni wanazotudai akina IPTL na wale tuliowatimua kwa sababu ya mikataba mibovu. Tutegemee ongezeko la tozo zaidi kuchangia bajeti hiyo ya nchemba. Nchemba lazima aendelee kutuchemba.
 
Nje mkopeshaji zinakuwa taasisi eg WB,Imf, AFDB,Mabenki ya kibiashara,Nchi mbalimbali mfano Tanzania Ina deni kubwa zaidi na Iran.

Mkopeshaji wa ndani ni kama umewahi sikia Serikali inauza bonds pale taasisi za Fedha eg banks na mifuko ya pensions ndio hukopesha Ili baadae wake kupata faida.
nashukuru kwa kunipa uelewa
 
Back
Top Bottom