Waziri Mwigulu: Wanaosema Rais Samia amekopa sana kuliko Awamu zote za nyuma waeleze pia mikopo hiyo inatokana na madeni ya nyuma

Waziri Mwigulu: Wanaosema Rais Samia amekopa sana kuliko Awamu zote za nyuma waeleze pia mikopo hiyo inatokana na madeni ya nyuma

Precious Diamond

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2023
Posts
593
Reaction score
1,376
Tarehe 30 Machi 2024, Waziri Mwigulu akiwa katika Mashindano ya 7 ya kuhifadhi Qur'aan Tukufu yaliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Kondoa, Waziri wa Viwanda na Biashara Ashatu Kijaji katika Viwanja vya Shule ya Msingi Lembo-Masawi, amerusha kijembe kwa wanaosema Rais Samia amekopa sana ndani toka aingie madarakni kuliko awamu zote za nyuma kwa pamoja. Amesema;

"Hivi majuzi nilimsikia ndugu yangu mmoja akiwa Babati, akisema Rais wa Awamu ya 6 ana miaka mitatu na ameshakopa trilioni 30 wakati waliotangulia walikaa miaka 60 na kukopa trilion 60 lakini akasahau kuwafafanulia watu kwamba kwenye hizi trilioni 30 trilioni tatu amegeuza deni la thamani la wazee akatoa fedha kwa njia ya hati fungani ili walipwe wazee, ambao walikopwa zamani miaka ya 93, kwa huruma yake kwa wazee amebadilisha deni lile na kutoa fedha deni lile likaingia kwenye deni la taifa

"Lakini pia amebadilisha madeni ya zamani ya TANESCO, TIPA/TPDC takribani trilioni 3 ili zipate mtaji, madeni yao hayo yakaingizwa pia katika deni la taifa.

"Kutokana na Dunia inavyoenda kuna badiliko la bei ya kubadilisha fedha pamoja na riba kwenye madeni ya zamani, hili tu ni lina thamani ya trilioni 5 mpaka 6. Karibia Trilioni 12 ni za madeni ya zamani sio Rais Kakopa.

"Kwenye trilioni 30 zimebaki trililioni 18, lakini Rais kaachiwa bwawa ambalo lilikuwa limetekelezwa kwa 37%, kaachiwa reli haijavuka Morogoro, reli peke yake ni dola bilioni 10 lakini haijakamilika mpaka mwisho, ambayo imeshachukuliwa ni takribani dola bilioni 6 (takribani trilioni 12 nyingine.

"Sasa ukisema Mwl. Nyerere hakuwa amekopa sana, Hayati Mwinyi hakuwa amekopa sana, Hayati Mkapa hakuwa amekopa sana, pamoja na Awamu ya 4 na ya 5, sasa walikuwa wamejenga reli wapi? Ndio hii Rais Samia amejenga."



 
Baelezeee papaaa, tomboka malamu.

Pia wakumbuke, miradi kama SGR na Bwawa la Mwalimu haikuwa imepata mkopo wa mradi wote, ilikuwa inakopewa kidogo sana, kama robo tu, mfano reli ilikopewa mpaka sijui kibaha, mama kaifikisha Dodoma mpaka mwanza, sasa ulitaka mtu aliyejenga mara kumi ya JPM aonekane katumia fedha kidogo?

Bwawa la Mwalimu Nyerere, JPM aliacha watu bado wanafyeka majani, leo bwawa lipo, kazi ya nani hiyo? SSH
 
Baelezeee papaaa, tomboka malamu.

Pia wakumbuke, miradi kama SGR na Bwawa la Mwalimu haikuwa imepata mkopo wa mradi wote, ilikuwa inakopewa kidogo sana, kama robo tu, mfano reli ilikopewa mpaka sijui kibaha,
Taratibu mnajirudi na miuzushi.
mama kaifikisha Dodoma mpaka mwanza, sasa ulitaka mtu aliyejenga mara kumi ya JPM aonekane katumia fedha kidogo?
🤔👇👇
Bwawa la Mwalimu Nyerere, JPM aliacha watu bado wanafyeka majani, leo bwawa lipo, kazi ya nani hiyo? SSH
👉Mtaja sema yooote! Kuwa mmekuwa mkizusha ya J.P.M kwamba ametumia fedha nyingi(wakati wake) kwenye mradi huo?

Ati walifanya kufyeka majani.
 
Tarehe 30 Machi 2024, Waziri Mwigulu akiwa katika Mashindano ya 7 ya kuhifadhi Qur'aan Tukufu yaliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Kondoa, Waziri wa Viwanda na Biashara Ashatu Kijaji katika Viwanja vya Shule ya Msingi Lembo-Masawi, amerusha kijembe kwa wanaosema Rais Samia amekopa sana ndani toka aingie madarakni kuliko awamu zote za nyuma kwa pamoja. Amesema;

"Hivi majuzi nilimsikia ndugu yangu mmoja akiwa Babati, akisema Rais wa Awamu ya 6 ana miaka mitatu na ameshakopa trilioni 30 wakati waliotangulia walikaa miaka 60 na kukopa trilion 60 lakini akasahau kuwafafanulia watu kwamba kwenye hizi trilioni 30 trilioni tatu amegeuza deni la thamani la wazee akatoa fedha kwa njia ya hati fungani ili walipwe wazee, ambao walikopwa zamani miaka ya 93, kwa huruma yake kwa wazee amebadilisha deni lile na kutoa fedha deni lile likaingia kwenye deni la taifa

"Lakini pia amebadilisha madeni ya zamani ya TANESCO, TIPA/TPDC takribani trilioni 3 ili zipate mtaji, madeni yao hayo yakaingizwa pia katika deni la taifa.

"Kutokana na Dunia inavyoenda kuna badiliko la bei ya kubadilisha fedha pamoja na riba kwenye madeni ya zamani, hili tu ni lina thamani ya trilioni 5 mpaka 6. Karibia Trilioni 12 ni za madeni ya zamani sio Rais Kakopa.

"Kwenye trilioni 30 zimebaki trililioni 18, lakini Rais kaachiwa bwawa ambalo lilikuwa limetekelezwa kwa 37%, kaachiwa reli haijavuka Morogoro, reli peke yake ni dola bilioni 10 lakini haijakamilika mpaka mwisho, ambayo imeshachukuliwa ni takribani dola bilioni 6 (takribani trilioni 12 nyingine.

"Sasa ukisema Mwl. Nyerere hakuwa amekopa sana, Hayati Mwinyi hakuwa amekopa sana, Hayati Mkapa hakuwa amekopa sana, pamoja na Awamu ya 4 na ya 5, sasa walikuwa wamejenga reli wapi? Ndio hii Rais Samia amejenga."


Trump ajengewe sanamu,, Africa a shit hole
 
Baelezeee papaaa, tomboka malamu.

Pia wakumbuke, miradi kama SGR na Bwawa la Mwalimu haikuwa imepata mkopo wa mradi wote, ilikuwa inakopewa kidogo sana, kama robo tu, mfano reli ilikopewa mpaka sijui kibaha, mama kaifikisha Dodoma mpaka mwanza, sasa ulitaka mtu aliyejenga mara kumi ya JPM aonekane katumia fedha kidogo?

Bwawa la Mwalimu Nyerere, JPM aliacha watu bado wanafyeka majani, leo bwawa lipo, kazi ya nani hiyo? SSH

Zumbukuku wewe
 
Huu ujinga utamweleza nani aelewe?? Swala ni kipindi chaka mikopo imekithiri!! Kwamba analipa Nini sjui aliachiwa Nini sisi haituhusu serikali ni ya SISIEMU na mikopo wamechukuwa waoo wasijidai kama niwatu tofautii!!
 
Huu ujinga utamweleza nani aelewe?? Swala ni kipindi chaka mikopo imekithiri!! Kwamba analipa Nini sjui aliachiwa Nini sisi haituhusu serikali ni ya SISIEMU na mikopo wamechukuwa waoo wasijidai kama niwatu tofautii!!
Unashangilia ujenzi wa reli na bwawa la mwalimu nyerere bila kujua chanzo cha fedha? Nyie ndio mnaacha nyumbani hela ya dagaa, unakuta mkeo kapika kuku, unashangilia
 
W
Unashangilia ujenzi wa reli na bwawa la mwalimu nyerere bila kujua chanzo cha fedha? Nyie ndio mnaacha nyumbani hela ya dagaa, unakuta mkeo kapika kuku, unashangilia
We jinga hakuna sababu kukopa kwa kupitiliza ili ujisifu umejenga sana, kwani hao walopita hawakujua kuhusu SGR? Walijua si mudawake kukopa hovyo kutafuta sifa za ujenzi!! Sasa TRC wanakula hasara,gutreni gwenyewe haguna spidi hiyo mlomezeshwa,midege hasara Sasa tusubiri bwawa tuuone huo umeme jinga ninyi
 
W

We jinga hakuna sababu kukopa kwa kupitiliza ili ujisifu umejenga sana, kwani hao walopita hawakujua kuhusu SGR? Walijua si mudawake kukopa hovyo kutafuta sifa za ujenzi!! Sasa TRC wanakula hasara,gutreni gwenyewe haguna spidi hiyo mlomezeshwa,midege hasara Sasa tusubiri bwawa tuuone huo umeme jinga ninyi
Ulitaka Samia abebe risk ya kiuchumi na kisiasa kwa kuiacha reli ifikie hapo mkoa wa pwani? Kaza mataya hayo, lazima ulipe hilo deni la taifa
 
U.S.A wenyewe mpaka leo wanaongoza kwa kudaiwa, plus China, Uingereza
Kwa mantiki hiyo tufanye tu kama watu wa U.S. na Uingereza kwasababu wao wanaongoza?

Itoshe, ni kwamba tunakuwa tunalipa madeni tu, yaani fedha nyingi zinaelekezwa huko wakati watu (wazawa) wanashida zao lukuki?
Deni likiwa siyo himilivu maana yake we are perpetuating poverty-tunaondoka vipi kwenye cycle of poverty?

Sasa na upigaji huu wa "kuupiga mwingi' unaonyeshwa kwenye miradi, hata kama fedha zinakopwa kwaajili ya kumalizia miradi hiyo tatizo linakuwa pale pale-miradi haikamiliki-tunaendelea kukopa!.

Niseme, hatuwezi kufanya kama US or Uk. Kwasababu kwao vianzio vya mapato ni vingi, masoko yao(finacial markets) ni bora, itoshe wana taasisi madhubuti kusimamia madeni yao.

Vilevile, uwezo wao ni mkubwa kulipa na kukopa kwasababu mapato yao ya kodi za ndani ni kubwa kulinganisha na kwetu sie.

Chiembe, unapuuza tofauti kubwa katika miundo yao ya kiuchumi na uwezo wao wa kitaasisi-simply tuna ulazimu wa kuwa na mikakati kulingana na muktadha na mustakabali wa nchi yetu, uwezo wetu na malengo mengine ya maendeleo.
 
Back
Top Bottom