Hivi punde
JF-Expert Member
- Apr 1, 2017
- 2,554
- 8,587
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage amesema nchi ina sukari ya kutosha na kilichojitokeza ni propaganda ya watu wasioitakia mema.
Akihitimisha hoja ya bajeti ya wizara yake ya mwaka 2018/19 leo Mei 11, 2018 bungeni, Mwijage amesema tayari ameagiza Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na Mamlaka ya Chakula la Dawa Tanzania (TFDA) kuiondoa sukari yote iliyopo bandarini.
Amesema yeye ni mcha Mungu na asingependa kuona Waislamu wanaotarajia kuingia katika mfungo wa Ramadhani wanapata shida ya kupata sukari.
Waziri Mwijage amesema hakuna tatizo la sukari kwani kuna akiba ya sukari tani 43,000 iliyopo katika stoo.
“Lakini Tanzania tunatumia tani 40,000 kwa mwezi,” amesema.
Amesema amewaagiza mameneja wa TBS na TFDA kuhakikisha tani 20,000 ya sukari iliyopo bandarini inaondolewa.
“Viwanda vya sukari vyote bado kama wiki tatu vinaanza kuzalisha. Suala la sukari lilikuwa ni propaganga na mimi ni ‘propagandist’ niliyesomea China,” amesema.
Kuhusu mazingira ya uwekezaji, Mwijage amesema amekuwa akipigania kuyafanya kuwa rafiki na kuwaomba wabunge wanapobaini kuwapo kwa changamoto zozote waziwasilishe kwake na hatua zitachukuliwa.
Pia, amesema amepokea maoni na ushauri wote uliotolewa na wabunge na kuahidi kuufanyia kazi.
Akihitimisha hoja ya bajeti ya wizara yake ya mwaka 2018/19 leo Mei 11, 2018 bungeni, Mwijage amesema tayari ameagiza Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na Mamlaka ya Chakula la Dawa Tanzania (TFDA) kuiondoa sukari yote iliyopo bandarini.
Amesema yeye ni mcha Mungu na asingependa kuona Waislamu wanaotarajia kuingia katika mfungo wa Ramadhani wanapata shida ya kupata sukari.
Waziri Mwijage amesema hakuna tatizo la sukari kwani kuna akiba ya sukari tani 43,000 iliyopo katika stoo.
“Lakini Tanzania tunatumia tani 40,000 kwa mwezi,” amesema.
Amesema amewaagiza mameneja wa TBS na TFDA kuhakikisha tani 20,000 ya sukari iliyopo bandarini inaondolewa.
“Viwanda vya sukari vyote bado kama wiki tatu vinaanza kuzalisha. Suala la sukari lilikuwa ni propaganga na mimi ni ‘propagandist’ niliyesomea China,” amesema.
Kuhusu mazingira ya uwekezaji, Mwijage amesema amekuwa akipigania kuyafanya kuwa rafiki na kuwaomba wabunge wanapobaini kuwapo kwa changamoto zozote waziwasilishe kwake na hatua zitachukuliwa.
Pia, amesema amepokea maoni na ushauri wote uliotolewa na wabunge na kuahidi kuufanyia kazi.