Waziri Nape: Hatujaibania starlink kutoa huduma ya intaneti, Elon Musk bado hajakidhi vigezo tulivyomuwekea

Ndugu waziri unge mruhusu Kwanza uone iyo huduma anatoaje kama ni magumashi ungepiga chini na kufatilia maswala ya ofisi lakini sio ivyo unavyo fanya.

Mheshimiwa umemwekea jamaa vikwazo Sana nchi jirani hapa huduma zimeanza unge communicate kujua wanapataje huduma tafazali umeshindwa kutusaidia kwenye mb Kwa sasa bei Kali na hazikai kabisa,
Basi tusaidie hapa walau panaweza kua na unafuu tunaumia wananchi wako
Imagine gb 1 2000+.🙉🙉🙉 Na ndani ya dakika 15 kwishnei uja download hapo.
 
Hahaaa!!mkuu mimi ni mgonga nyundo tu mwenzako huku mtaani!!?ila nimesema tu kulingana na sheria zilizopo sasa!!kama nia ipo ni kuzibadiri tu,ila sasa wenye hisa kwenye makampuni hayo ndio wanaotuongoza je watakubali?!?TTCL ndio wenye mkongo wa taifa ni serikali,huko airtel karibu 51 % ni ya serikali!!
 
Mkuu lala naona sasa umeishiwa hoja!!iphone au sumsung ni huduma?hiyo internet inaletwa na iphone?
Sasa unaleta double standard, kwamba ili huduma ya Instagram ipatikane tunahitaji internet ya Airtel, si tunahitaji na device pia? Au 🤷🏽‍♂️
 
Mbona ameshindwa kulinda haki za walaji(watumiaji wa internet) kwa makampuni ya nchini?

Leo amekuwa na huruma sana ya kulinda wateja, hiyo huruma kaitoa wapi?

Baada ya kelele za mabando kupigwa kila sehemu, akasema mwezi wa pili (Februali), gharama za mabado zitaangaliwa upya!

Mpaka mwezi wa pili umeisha hajasema lolote na hakuna hata raia aliyekumbushia kauli hiyo ya Waziri!

Ndiyo kusema walishatuona sisi waTz wepesi sana kusahau na ni wapumbaf!

Huyu Waziri ni mtetezi mkubwa sana wa makampuni ya simu kuliko raia, Bungeni tulimuona jinsi anavyozikingia kifua.

Jambo lolote linalohusu unyonyaji wa makampuni ya simu kwa walaji, lazima asimame kidete kutetea bila ya soni.

Na hili la kumnyima kibali Star link, vimewekwa vigezo vya hila ili asiwekeze nchini ili tuendelee kukamuliwa na hizo kampuni za simu mumiani ambazo yeye ni mnufaika wake.
 
Mambo ya internate toka lini yakahitaji physical address!!??
acheni ujima. Tz tunapitwa mno.
Wanajua fika Muski akija na intenate. Airtel Tigo Voda hawa wenye monopolistic power watakuwa wanapata a normal profit. Manake sshv wanapata supernormal profit kwa ukwanguzi wa bando zetu
 
Ofisi ina faida gani. Mtandao ndio shughuli zao, ukiwataka wanaptikana kila saa. Ofisi moja kwa dunia nzima. Hawa tatizo wanataka mambo ya kuzima data, na pia hawa wengine ie. Vod., airte., na wengine hawataki ushindani hapo.
Wanatafuta visngizio, Nape lazima mfuko umejaa kwa kutetea maswahiba wake
 
Je,
Facebook, Google, Twitter, Whatsapp, Canal+, Ebay, Amazon, Aliexpress wana ofisi Tanzania?

Watumiaji wa hizo kampuni tajwa hapo juu huwa hawapati shida na zikatatuliwa pasipo uwepo wa ofisi? Watumiaji wamewahi kwenda kwa NAPE au TCRA kulalamika?

Kweli hapa ni uzembe tu wa watanzania kupata wanachostahili
 
Afadhali umeona mkuu. Viongozi tulionao hawajali kabisa Maslahi ya Wtz
 
Sio rahisi yaani serikali inakimeo chake mkonge wa taifa ambao tulipigwa kwa hela ndefuu na haujaleta tija yyte then wamkaribishe huyo starlink bongo.!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…