Waziri Nchemba: Utoaji risiti za kielektroniki imekuwa kama punguzo la bei, mteja asipopewa risiti anapunguziwa bei

Waziri Nchemba: Utoaji risiti za kielektroniki imekuwa kama punguzo la bei, mteja asipopewa risiti anapunguziwa bei

Mtazame jinsi anavyosoma karatasi...hakuna element yoyote kwamba yupo serious.
Hayo mambo anayosoma hivi kweli kabisa kwa mtu mwenye PHD anahitaji kukodolea macho mstari kwa mstari?...vitu obvious ambavyo vinajulikana...
Usimuonee jamaa kana kwamba hukupata kuona summary ya thesis yake ya hiyo ndigrii. Msamehe bure.
 
"Matumizi ya mashine za kielekroniki kwa ajili ya kodi na kutoa risiti bado imekuwa ni changamoto kwa wananchi, kwasasa utoaji wa risiti umekuwa kama punguzo la bei manake mtu asipopewa risiti anapunguziwa bei tofauti na akidai risiti jambo ambalo linasababisha bidhaa nyingi kuuzwa nje na bei inayofahamika na TRA na hapa nataka niwakumbushe watanzania kuwa suala la kodi sio la TRA peke yake ni jambo la watanzania wote"
Na waziri naye analalamika badala ya kuja na solution!!!
 
NINGELIKUWA KIONGOZI, MADUKA YA KARIAKOO NINGEYATENGENEZEA MFUMO ULE WA ZAMANI, KUYAKADIRIA KODI, KUYAPA NAMBA MAALUM ITAKAYOKUWA INAAMBATANA NA SIMU YA MUHUSIKA, NID, N. K, MADUKA YA KARIAKOO YAKADIRIWE KODI,
°HATUKOSI MADUKA, MIL 3, YA KIWANGO AMBAYO YATAKADIRIWA MIL 10 KWA MWAKA, HII INGESAIDIA KUTOKUKWEPA KULIPA MAANA WATAKUWA WAKO COMMITED KWA HILI, TATIZO LA KARIAKOO, WAJANJA NI WENGI MNO AND ARE SO BRIGHT.
N. B, biashara kubwa iliyopo kariakoo ni chukua hapa, uza kule!, yaani mwenye duka anachukuwa bidhaa duka lingine analetea mteja lakini anafremu!
 
Unaposikia CAG akisema Mabilioni yamepigwa na hakuna hatua zozote zinazochukuliwa hivi unakuwa na hamu tu ya kulipa kodi?

👆 naombeni majibu tafadhali.
 
"Matumizi ya mashine za kielekroniki kwa ajili ya kodi na kutoa risiti bado imekuwa ni changamoto kwa wananchi, kwasasa utoaji wa risiti umekuwa kama punguzo la bei manake mtu asipopewa risiti anapunguziwa bei tofauti na akidai risiti jambo ambalo linasababisha bidhaa nyingi kuuzwa nje na bei inayofahamika na TRA na hapa nataka niwakumbushe watanzania kuwa suala la kodi sio la TRA peke yake ni jambo la watanzania wote"

View attachment 2918088

Yeye na wnamCCM wenzake wangeanza kwa kuonyesha mfano.

Kwa vile CCM wameamua kula kwa urefu wa kamba zao na wananchi nao huo ndiyo urefu wa kamba zao.

Siku wakibadilika na sisi wananchi tutabadilika.
 
Serikalini hakuna usiriaz kwenye matumizi.

Matumizi makubwa kwenye magari ya anasa ni sababu pekee miongoni mwa nyingi zinazonichochea kukwepa Kodi.

Watumishi wa wilayani akiwemo DC watumie magari chini ya cc2000, isipokuwa polisi wao waendelee na mashine zenye kifua kipana!

Ni big 6 pekee ndo wapewe vxr
Kabisa. Pia kusafiri kwenye ndege, wasafiri kwenye madaraja ya kawaida. Wabunge wapunguzwe idadi, hawa wa viti maluum waondolewe pia. Kuna areas nyingi sana kupunguza matumizi ya serekali. Bila hivyo. mwananchi endelea kukwepa kodi kadiri uwezavyo.
 
"Matumizi ya mashine za kielekroniki kwa ajili ya kodi na kutoa risiti bado imekuwa ni changamoto kwa wananchi, kwasasa utoaji wa risiti umekuwa kama punguzo la bei manake mtu asipopewa risiti anapunguziwa bei tofauti na akidai risiti jambo ambalo linasababisha bidhaa nyingi kuuzwa nje na bei inayofahamika na TRA na hapa nataka niwakumbushe watanzania kuwa suala la kodi sio la TRA peke yake ni jambo la watanzania wote"

View attachment 2918088
Mfumo wa kodi wa kwetu ni wa kijinga sana kadri unavyoongeza lulipa kodi ndo unawekewa makadirio makabwa mafano 10% ya nyumba ya 1000000 sio sawa na 10 % ya 200, 000 sasa nani anataka

Sent from my SM-A037F using JamiiForums mobile app
 
Hakuna mtanzania asietamani kulipa kodi na sio kodi tu hata ingekuwa kuchangia bajeti yetu kwa hela za mfukoni tungechangia, shida ni matumizi mabovu ya pesa za kodi, ufujaji na wizi wa viongozi wetu, ndio hapo unapoona kulipa kodi ni ujinga, kitu cha laki 3, akikwambia na risiti 350000 bila risiti 300000, unaona hii 50000 bora niwanunulie kuku na basmati nyumbani watoto wafurahie.

Serikali inapaswa ibadilike(japo najua haiwezi badilika)
Na ukijifanya kutoa risiti kaam wanavyotaka nakuhakikishia baada ya 3month unafunga hiyo biashara

Sent from my SM-A037F using JamiiForums mobile app
 
nikifikiriaga habari za Cag na icho anachokisoma waziri naona kama vile kichekesho cha Joti na Mpoki
 
Mara zote CAG anaposoma taarifa ya mahesabu ya serikali hua kuna ufisadi na ujambazi mkubwa hua unatajwa wa mabilioni ya fedha lakini hakuna yoyote ambae amewahi kushikwa na kufungwa kwa wizi huo na kinachoibwa ni Kodi zetu sisi, sasa ya nini kulipa Kodi na nikijua kabisa itaibwa na mwizi mtamficha hatochukuliwa hatua yoyote 🤔🤔si bora nikwepe tuu Kodi tukose wote
 
Ni kichekesho kuona waziri akilalamika wananchi kuiba Kodi lakini hashangai viongozi wenzake kukwapua Kodi za watanzania hivi niulize nyie viongozi wa ccm ni lini mtaacha ubinafsi? Akiiba mwanachi mnaumia mkiiba nyie ni sawa pumbafu kabisa
 
NINGELIKUWA KIONGOZI, MADUKA YA KARIAKOO NINGEYATENGENEZEA MFUMO ULE WA ZAMANI, KUYAKADIRIA KODI, KUYAPA NAMBA MAALUM ITAKAYOKUWA INAAMBATANA NA SIMU YA MUHUSIKA, NID, N. K, MADUKA YA KARIAKOO YAKADIRIWE KODI,
°HATUKOSI MADUKA, MIL 3, YA KIWANGO AMBAYO YATAKADIRIWA MIL 10 KWA MWAKA, HII INGESAIDIA KUTOKUKWEPA KULIPA MAANA WATAKUWA WAKO COMMITED KWA HILI, TATIZO LA KARIAKOO, WAJANJA NI WENGI MNO AND ARE SO BRIGHT.
N. B, biashara kubwa iliyopo kariakoo ni chukua hapa, uza kule!, yaani mwenye duka anachukuwa bidhaa duka lingine analetea mteja lakini anafremu!
Tatizo ni matumizi makubwa ya Serikali kaka.
 
Ukipata nafasi ya kukwepa kodi, kwepa tu

1709041486022.png
 
Back
Top Bottom