Waziri Ndumbaro Ahimiza Mabadiliko Chuo cha Michezo Malya

Waziri Ndumbaro Ahimiza Mabadiliko Chuo cha Michezo Malya

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

WAZIRI NDUMBARO AHIMIZA MABADILIKO CHUO CHA MICHEZO MALYA

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amewataka watuishi wa Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya wafanye mabadiliko katika utendaji kazi wao ili waendane na kasi ya mabadiliko ya sekta hiyo hapa nchini.

Mhe. Ndumbaro amesema hayo alipofanya ziara chuoni hapo Julai 1, 2024 kukagua maendeleo ya taaluma na miundombinu ya chuo hicho.

Ammkizungumza na watumishi wa chuo hicho amewataka wabadilike katika utendaji kazi wao na kuepuka kufanya kazi kwa mazoea ili waongeze thamani ya kile wanachokifanya.

Aidha, katika ziara hiyo Waziri Ndumbaro ametembelea na kukagua ujenzi wa Akademia ya michezo ambapo ameagiza mshauri elekezi ahakikishe anamsimamia vizuri Mkandarasi ili kazi hiyo ifanyike kwa ubora.

Katika hatua nyingine Waziri Ndumbaro ametembela ujenzi wa hosteli mpya za wanafunzi ambazo ujenzi wake umefikia asilimia 84% pamoja na kuzungumzo na Wanachuo. @chuochamaendeleoyamichezo
 

Attachments

  • GRd6FBBWgAAJeU6.jpg
    GRd6FBBWgAAJeU6.jpg
    170.7 KB · Views: 7
  • GRd6EyJW8AAu-wQ.jpg
    GRd6EyJW8AAu-wQ.jpg
    375.1 KB · Views: 2
  • GRd6FBsb0AIPpIB.jpg
    GRd6FBsb0AIPpIB.jpg
    341.2 KB · Views: 3
  • GRd6FBDW0AEJim_.jpg
    GRd6FBDW0AEJim_.jpg
    240.9 KB · Views: 2
Back
Top Bottom