Waziri Silaa awaomba Walutheri kutumia Sikukuu ya Pasaka kumwombea Rais Samia

Waziri Silaa awaomba Walutheri kutumia Sikukuu ya Pasaka kumwombea Rais Samia

Precious Diamond

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2023
Posts
593
Reaction score
1,376
1711921083570.png

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa amewataka waumini wa Kanisa la Kiinjili na Kilutheri Tanzania (KKKT) kuhakikisha wanamuombea Rais Samia katika kazi yake ya kuliongoza taifa.

Silaa ameyasema hayo leo Jumapili, Machi 31, 2024 alipofungua harambee ya kuchangia upanuzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Chanika jijini Dar es Salaam.

Kauli yake hiyo inatokana na kile alichoeleza, Rais Samia alishiriki sherehe za kumsimika Mkuu wa KKKT, Dkt. Alex Malasusa, hatua ambayo inathibitisha upendo wa mkuu huyo wa nchi kwa waumini wa kanisa hilo.

"Nawaomba sana washarika wenzangu tumuombee Rais wetu, Mungu ampe nguvu, hekima na busara ya kuliongoza taifa letu. Nakuomba ufikishe salamu zangu kwa Baba Askofu na washarika wenzangu, kutumia Pasaka, maombi na Ibada zetu kumuombea Rais wetu, Samia Suluhu Hassan," amesema.

Jambo TV
 
Kwani yeye hawez kujiombea mwenyewe?
Yaani KKKT isaidie ktk kutunga mapambio, yaimbwe makanisani, mahubiri yaingize jina la Rais na waumini waitikie AAMEN!! Hadi xaxa ktk Liturgia kuna kipengere cha kuliombea taifa na wachungaji hua wanakitumia kuliombea taifa na viongozi wake. Huyu waziri kaona hakitoshi!? Kuendelea kuwa na viongozi wa sampli hii wasiotumia ubongo kufikiri, maendeleo tutayaskia kw wenzetu tu
 
Rais mwenyewe sijawahi msikia akitaka kuombewa...
 
Tutegemee Ibada zetu nyingi kutembelewa na Wanasiasa nyakati hizi ili kutafutwa kuungwa mkono 🙌
 
Back
Top Bottom