Waziri Sophia Simba - Mwenyekiti Mpya UW-CCM (Taifa)

Waziri Sophia Simba - Mwenyekiti Mpya UW-CCM (Taifa)

Nauliza,hoja ya mama kahama,JK juu ya rushwa ya mama simba aliishughulkia vp?ok,alisema itachnugzwa,yes,lini?na nani?na kama ikigundulika she is corrupt,atamfanya nini?kwanini uchaguzi usingelisitishwa hadi uchunguzi wa hoja ya kahama zidi ya sophia ukamilike?
Huu ndio msumali mkali dhidi ya uchaguzi huu, ni wazi haki ya kusikilizwa ya mgombea mmoja imepuuzwa kwani malalamiko yake yaliwasilishwa kabla hata ya wajumbe wa mkutano kuanza safari. Ilikuwa busara kusitisha taratibu za maandalizi na kuruhusu uchunguzi hata kama mtuhumiwa angeendelea na wadhifa wake wa uwaziri. 'Of course' mtu anaweza kusema itakuwa vipi kama itatokea 'series of' rufaa, lakini busara ni vizuri itumike kuepusha manung'uniko ya baadhi ya wanachama. Busara iliyotumika kwenye uchanguzi wa UVCCM ilikuwa mfano mzuri; haikuwa lazima kutumia 'same approach' lakini CC walipaswa kutafuta majibu ili baada ya uchaguzi isitokee pande itayolalamika. Tengeneza picha kama hao wajumbe 383 (tena viongozi wenye ushawishi kwenye maeneo yao) wataamua kutumia ajenda hii kujenga taswila ya upendeleo dhidi ya Mh. Simba. Definitely huo utakuwa mwanzo wa mmeng'enyeko ndani ya chama.

FMES, nashukuru kwa uchambuzi mkuu. Taratibu Chama kinaanza kuweka mazingira tata kwa wanachama wake. Lakini mwisho wa siku M/kiti ndiye mwenye jukumu la kukiokoa chama. Kwa hili naona kama anaongeza mpasuko maana alikuwa ameanza kuwachota watu wenye mlengo wa kimwakyembe, lakini hii inazua maswali mengi zaidi.
 
...........................................chukua jembe ukalime,............. halafu jiandae kuchukua kapu tayari kwa kuvuna.

Si afadhali kungekuwa na shamba la kulima.Hao hao wenye nazo wamenunua ardhi na iliyobaki kidogo haina rutuba,hailimiki,hakuna mvua tumesubiri hata ile tuliyoahidiwa na mh.Lowassa kipindi kile ile mvua ya kutengeneza nayo bado haijanyesha.Nilatimaje sasa????na nitavuna kipi??
 
Huu ndio msumali mkali dhidi ya uchaguzi huu, ni wazi haki ya kusikilizwa ya mgombea mmoja imepuuzwa kwani malalamiko yake yaliwasilishwa kabla hata ya wajumbe wa mkutano kuanza safari. Ilikuwa busara kusitisha taratibu za maandalizi na kuruhusu uchunguzi hata kama mtuhumiwa angeendelea na wadhifa wake wa uwaziri. 'Of course' mtu anaweza kusema itakuwa vipi kama itatokea 'series of' rufaa, lakini busara ni vizuri itumike kuepusha manung'uniko ya baadhi ya wanachama. Busara iliyotumika kwenye uchanguzi wa UVCCM ilikuwa mfano mzuri; haikuwa lazima kutumia 'same approach' lakini CC walipaswa kutafuta majibu ili baada ya uchaguzi isitokee pande itayolalamika. Tengeneza picha kama hao wajumbe 383 (tena viongozi wenye ushawishi kwenye maeneo yao) wataamua kutumia ajenda hii kujenga taswila ya upendeleo dhidi ya Mh. Simba. Definitely huo utakuwa mwanzo wa mmeng'enyeko ndani ya chama.

FMES, nashukuru kwa uchambuzi mkuu. Taratibu Chama kinaanza kuweka mazingira tata kwa wanachama wake. Lakini mwisho wa siku M/kiti ndiye mwenye jukumu la kukiokoa chama. Kwa hili naona kama anaongeza mpasuko maana alikuwa ameanza kuwachota watu wenye mlengo wa kimwakyembe, lakini hii inazua maswali mengi zaidi.


CCM imegeuka kapu la wahuni tu. Watu wa busara waliobaki kule ni wale walioianzisha na wanaona vigumu kuiacha kwa vile wao ndio walioianzisha; wanakubali kubeba mzigo wa aibu wasizostahili kwa sababu za kihistoria tu. Wenye busara wanaoinga kule hufyekwa kwa njia mbalimbali na kuishia kusikojulikana
 
Simba amzima Kahama UWT
Martha Mtangoo, Dodoma
Daily News; Thursday,January 08, 2009 @21:15

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Simba, ameibuka kidedea na kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), baada ya kuwabwaga wagombea wenzake Janeth Kahama na Joyce Masunga.

Katika uchaguzi uliofanyika juzi usiku na matokeo kutangazwa jana jioni katika Ukumbi wa Kilimani na msimamizi mkuu wa uchaguzi huo, Muhammed Seif Khatib, Simba alishinda baada ya kupata kura 470 sawa na asilimia 54.4 ya kura halali 862 zilizopigwa na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Uchaguzi.

Kahama ambaye ni mwenyekiti wa zamani wa UWT Mkoa wa Dar es Salaam, alipata kura 383 sawa na asilimia 48.4, katika mchuano huo mkali ulioshuhudia kampeni za kila aina kwa wagombea hasa wawili hao. Masunga ambaye kama Kahama ni Mbunge wa Viti Maalumu, aliambulia kura 10 kati ya kura 862 zilizopigwa sawa na asilimia 1.1.

Simba pia ni Mbunge akiwa miongoni mwa wabunge wa Kuteuliwa. Kwa upande wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa UWT Taifa, Asha Bakari Makame aliyekuwa mgombea pekee na hivyo kupigiwa kura za ndiyo na hapana, alishinda kwa kura za ndiyo 736 kati ya kura halali 815 sawa na asilimia 90.3.

Naye Ofisa Uhusiano wa Benki ya NMB, Shy-Rose Bhanji aliibuka mshindi kwa kuukwaa uwakilishi katika Jumuiya ya Umoja wa Vijana (UVCCM), baada ya kuwabwaga wenzake watano kwa kupata kura 499 kati ya kura 807 zilizopigwa huku Mbunge wa Viti Maalumu, Martha Mlata akiibuka mshindi wa kuwakilisha katika Jumuiya ya Wazazi.

Kwa upande wa nafasi za Baraza Kuu, walioshinda kutoka Bara ni Margreth Mkanga, Betty Machangu, Elina Magoha, Amina Masenza na Sifa Swai. Kwa upande wa Zanzibar, washindi ni Zulekha Yunus Haji, Lilian Grace Limo, Catherine Nao, Subira Mohamed Ali na Latifa Nassor Ahmed. Akizungumza baada ya matokeo hayo kutangazwa, Kahama alisema uchaguzi huo ulikuwa mgumu na kwamba ulikuwa na rafu nyingi na matusi yalitawala.

Alisema uchaguzi uko duniani na mbinguni hakuna uchaguzi hivyo ni vyema akinamama wakakubali kuwa wao ni wazazi na walezi na hivyo ni lazima wakawa wastaarabu kwa kuwa wengi wao wameshazeeka ni lazima wawe na cha kuwafunza vijana ambao baadaye watakuwa viongozi wa umoja huo.

Alisema kama wanawake wa umoja huo wataendeleza tabia hiyo, UWT haitakuwa na mwelekeo mzuri na kuongeza kuwa katika uchaguzi huo, amepata matusi mengi ambayo yanaweza kuweka makundi ndani ya UWT. “Mimi sina ugomvi na mtu ila ninamwomba radhi sana mume wangu kwa matusi ambayo nilikuwa natukanwa kupitia simu… nisamehe sana mzee mwenzangu,” alisema Kahama, mke wa waziri wa zamani, Sir George Kahama. Aliwaomba wanachama wa umoja huo kumwunga mkono mwenyekiti mpya kwa kuwa bila wanachama hakutakuwa na UWT imara na kuongeza kuwa atakuwa tayari muda wowote ambapo mwenyekiti mpya atamhitaji.
 
.....................................................watajiju
 
...hivi jumuiya kama hizi zina faida gani kwa nchi? kwanini wasijiite jumuiya ya wanawake wa CCM kuliko Tanzania,zinaonekana ni jumuiya za kukuza mafisadi tuu

Hizi jumuiya zina "faida" kubwa sana kwa vyama husika - (viwe vya kisiasa ama vya kidini). jUMUIYA hizi zina mchango mkubwa sana katika ku mobilise siyo tu watu kwa ajili ya uchaguzi bali hata nyenzo/rasilimali ikiwemo fedha.Fikiria idadi ya wanawake na nguvu waliyo nayo ya kufanya mambo mbalimbali.Mwanamke akidhamiria kufanya kitu kinafanikiwa.Rejea mchango wa wanawake katika harakati mbalimbali ziwe za uhuru ama vinginevyo.Fikiria ni jinsi gani wanawake wanafanikisha hata mabo madogo kama sherehe ( harusi n.k) Kwa hili la UWT kama ulisikiliza hotuba ya Rais wakati akifungua rasmi mkutano wa UWT juzi basi utanielewa nina maana gani.
Dont under rate the power and strength of women!
 
Yaani,

Pesa iliyomwaga Dodoma ni kufuru,I was talking na Mhariri mmoja wa gazeti la kila siku hapo bongo nimeshtushwa sana na pesa waliyokuwa wakiwapa watu.

Yaani waziri anakuwa na pesa nyingi kiasi hiki au kuna pesa za EPA zinafanya kazi.
 
Hujui unachokisema ni MDINI mkubwa wewe. Kwa taarifa yako Sofia Simba sio Muislamu ni MKRISTO wa MISHENI KOTA.
Hivi kuishi/kuzaliwa misheni kota basi automatically unageuka mkristo eh??
Wakaazi wote wa misheni kota ni wakristo kumbe?
Unamjua vizuri Sophia au unakurupuka tu?
 
Hizi jumuiya zina "faida" kubwa sana kwa vyama husika - (viwe vya kisiasa ama vya kidini). jUMUIYA hizi zina mchango mkubwa sana katika ku mobilise siyo tu watu kwa ajili ya uchaguzi bali hata nyenzo/rasilimali ikiwemo fedha.Fikiria idadi ya wanawake na nguvu waliyo nayo ya kufanya mambo mbalimbali.Mwanamke akidhamiria kufanya kitu kinafanikiwa.Rejea mchango wa wanawake katika harakati mbalimbali ziwe za uhuru ama vinginevyo.Fikiria ni jinsi gani wanawake wanafanikisha hata mabo madogo kama sherehe ( harusi n.k) Kwa hili la UWT kama ulisikiliza hotuba ya Rais wakati akifungua rasmi mkutano wa UWT juzi basi utanielewa nina maana gani.
Dont under rate the power and strength of women!

Umesema jumuia zina mchango mkubwa, lakini katika kufananua umejikita sana kwa wanawake are a gender biased? unawatetea wanawake au jumuia?
 
Hizi jumuiya zina "faida" kubwa sana kwa vyama husika - (viwe vya kisiasa ama vya kidini). jUMUIYA hizi zina mchango mkubwa sana katika ku mobilise siyo tu watu kwa ajili ya uchaguzi bali hata nyenzo/rasilimali ikiwemo fedha.Fikiria idadi ya wanawake na nguvu waliyo nayo ya kufanya mambo mbalimbali.Mwanamke akidhamiria kufanya kitu kinafanikiwa.Rejea mchango wa wanawake katika harakati mbalimbali ziwe za uhuru ama vinginevyo.Fikiria ni jinsi gani wanawake wanafanikisha hata mabo madogo kama sherehe ( harusi n.k) Kwa hili la UWT kama ulisikiliza hotuba ya Rais wakati akifungua rasmi mkutano wa UWT juzi basi utanielewa nina maana gani.
Dont under rate the power and strength of women!

alaaah kumbe ndio maana wale wabunge wa upendeleo wakiamka kuongea wao ni kuinamia upande mmoja wa shilingi bila kujadili mustakabari wa taifa hili na watu wa jinsia zote kwa UJUMLA. KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
 
Humu ndani niliwahi soma mmoja wetu akisema kambi ya mkapa imempa back up mama kahama, na kuhakikisha hilo ilimlazimu anna mkapa ashiriki ktk sehemu ya mchakato wa kumpatia ushindi janet sasa leo wakuu mnasema eti washindi ni ben,lowasa,jk na wengineo!!! Nisaidieni kunipa ufafanuzi wa kina, mkuu wa medani amesema kulikuwepo false pretenders ila sijalipata somo vizuri
 
To me sophia mnyambi simba alistahiki kukalia kiti hiyo. Bravo madam sophy
 
Katika nchi yenye viongozi wenye maadili mazuri huwezi kuwa na waziri mwenye dhamana ya utawala bora na yeye mwenyewe akawa mtoa RUSHWA; Sophia Simba hata kama ni mpambe wa Jakaya hana intergrity ya kuwa kiongozi wa serikali inayoheshimika na watu wake. Jakaya should learn to walk the talk, amekuwa mnafiki kwa muda mrefu sana.
 
Feld Marshall mkuu, heshima mbele masahihisho kidogo ya data zako, Sophia Simba hakuwa chuo kikuu wakati mmoja na Jakaya!! Jakaya ni graduate wa mwaka 1975 na Sophia ameingia chuo kikuu mature age baadae sana isipokuwa Mzee Kitwana Kondo alikuwa Chuoni wakati wa Jakaya akijaribu kusoma sheria lakini hakufanikwa!!
 
- Mkuu check vizuri dataz zako Sophia, amesoma pale kwa muda mrefu sana in and out for many years mpaka kumaliza.
 
CHADEMA, CUF, TLP, NCCR-MAGEUZI,... igeni mfano huu wa CCM wa kuwa na JUMUIA zenye nguvu na ushawishi kiasi hiki. Vinginevyo endeleeni kujikusanyia nguvu na ushawishi wa mtu mmojammoja mwone kama mtafika mbali.
 
Hivi kuishi/kuzaliwa misheni kota basi automatically unageuka mkristo eh??
Wakaazi wote wa misheni kota ni wakristo kumbe?
Unamjua vizuri Sophia au unakurupuka tu?

Tulia mama, soma vizuri na jitahidi kufikiri kabla ya kuandika. Sijasema kuishi misheni kota automatically unakuwa mkristo. Hivi mtu akisema Jaji Mkuu Augostino Ramadhani ni mristu wa Zanzibar ina maana wazanzibari wote ni wakristu?

Uliekurupuka ni wewe namjua Sophia vizuri sana na I still stand to my earlier post Sophia ni mkristu wa misheni kota. Get it?
 
- Lets cut the chase hapa, Sophia hajawahi kuwa mke wa Idd Simba, never! na wala sio Mu-Islam, Sophia ni Mkatoliki na amekua girlfriend wa Kitwana Kondo kwa muda mrefu sana lakini sio mkewe wa ndoa, na amefikia hata kuzaa naye watoto, mmoja wao yupo jela kwa muda mrefu sana kule Carlifornia. Sophia amesoma sheria Mlimani wakati mmoja na muungwana, na Lowassa.

- Connection yake kwenye power na hasa na muungwana, inakuja through Kitwana Kondo former meya wa Dar na mbunge wa zamani Kigamboni, a very influencial man toka hata wakati wa Mwalimu kutokana na his knowhow na ishus za Waisilamu, hasa jijini Dar. Yeye ndiye the go to guy kwa marais wote since Mwalimu, kwenye kuzima na kuziwahi ishus tata za Wa-Isilamu mjini Dar, hasa kwenye kuzima maandamano na utata wa never ending kwenye Bakwata.

- Kwenye huu uchaguzi kumetokea ishus nyingi sana ambazo zinatatanisha sana, kwa mfano in public Muungwana hakuwa mkweli na exactly nani aliyemtaka hapa kushinda, lakini kumbe it was very clear in private aliyemtaka ni Sophia, Mafisadi fearing the public blacklash kama ya uchaguzi wa Uv-CCM na wao pia wamecheza un-ugly game ya kutoa signal kwa wahusika wengi wa uchaguzi kuwa wanam-support Mama Janet, huku wakimpa Sophia kitita cha hela zisizo na mfano kwa siri ili kushinda. At one point during uchaguzi jana, hela zilikuwa zinagawiwa openly huku maa-agent wa idara wakiwazuia watoa hela wa Mama Janet na kuruhusu wa Sophia tu kutoa mapesa hayo ya rushwa, sasa the small picture hapa ni kwamba kwenye vita vya ufisadi, tumepiga hatua mbili nyuma.

- Lakini the big picture ni je Muungwana ameamua kurudi tena kwa marafiki zake, yaani mafisadi? Na je aliwahi kuachana nao for real? I mean sio siri kua hapa wote wamemsaidia mgombea mmoja, sasa was it co-ordinated au ilikuwa kila mmoja ki-vyake? Huu uchaguzi ni kama zile chaguzi mbili za huko nyuma kuelekea kwenye uchaguzi wa mwisho wa rais, yaani Nchimbi na UV-CCM na mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma, ambapo ndipo hasa mafisadi walipoanza kuonyesha makucha yao rasmi kama vile huu uchaguzi wa jana uwt. Huu uchaguzi sasa sio siri tena kuwa ulikuwa ni agenda ya urais 2010 na pia 2015 na the number one looser jana alikuwa ni Membe, namba mbili ni lile kundi la wapiganaji kina Mwakyembe na the likes, namba tatu mpiganaji Mengi, nne ni sisi wananchi ambao tumekuwa mstari wa mbele sana baada ya kutiwa nguvu na uchaguzi wa UV-CCM, ingawa kwa wanaomjua vizuri Muungwana wanasema this is him kumridhisha kila mtu na kuendeleza popularity yake, maana nasikia aliposema tu anataka mgombea msomi meaning Sophia, basi uchaguzi ukaisha pale pale na infact ilikuwa ni marudio ya maneno ya Mkapa kwenye uchaguzi wa rais uliopita, tuchague rais kijana.

- Walioshinda jana tena big time ni Lowassa, Mkapa, Makamba, Nchimbi, na hasa Masha, maana sasa the hope is back tena na urais. Uchaguzi huu wa UWT unaweka pabaya sana ile operation Kisutu I mean itaenda vipi forward wakati waziri wa utawala bora yaani TAKUKURU na Usalama, anapohusika kwenye this very ugly rushwa na the very abuse of power?

- I mean talking about abuse of power ya kina Mramba na yona mbona wanakuwa cha mtoto kulinganisha na what waziri wetu did here, tena akiwa na support ya rais na hizi instituion mbili muhimu za dola tunazoziaminia kwenye vita ya kusafisha mafisadi? Unajua nitawashangaa sana wanaopelekwa Kisutu, kama hawata cite ishus kama hizi za abuse of power kwenye huu uchaguzi katika kujitetea kwao against serikali, kwa sababu serikali inapata wapi hapa moral na legal authority kuwa-prosecute on abuse of power wakati na wao wanafanya hayo hayo na hasa kwenye huu uchaguzi? Sisemi kwamba sasa kina Mramba wawe off the hook, no way hao bado tunakomaa nao tu mpaka kieleweke lakini hapa serikali imetuchanganya kama haikujichanganya yenyewe.

- Again, kama demokrasia inavyotaka tunamtakia heri Auntie Sophia na ushindi wake, lakini hivi ni kweli the end in this uchaguzi unaweza uka-justify the means? Na ni under nani's expense? Wote wawili Auntie Sophia na Mama Janet, hawakufaa kuruhusiwa kugombea huu uchaguzi, kwa sababu wametumia rushwa kubwa sana tena isiyo mfano kwa nafasi ndogo sana ya uwt, sasa urais ujao itakuwaje?

Mungu Ibariki Tanzania.

FMES, Asante kwa ufafanuzi wa yaliyotokea.

Wengi wanachanganya UWT na UW-CCM, Sasa hivi hakuna kiti kinaitwa UWT, ni UW - CCM. Vinginevyo akinamama wataandamana kupinga yaliyotukia pale kwenye uchaguzi kama kweli, ingekuwa ni UWAKILISHI WA WANAWAKE WA TANZANIA!!. Heading ya thread iko sahihi.
 
Jakaya katika hotuba yake ya kufungua mkutano wa wanawake wa CCM aliwaasa wachague viongozi wasomi!! Sasa cha kushangaza ni kwamba katika wote waliochaguliwa hakuna hata msomi wa haja hata mmoja.Pengine siwafahamu lakini wakina Amina Masenza, Margareth Mkanga na Muimbaji wa nyimbo za dini Martha Mlata hao ndio wasomi wa Jakaya na CCM yake!!
 
Uchaguzi wa UWT wa CCM umemalizika kwa Mh. Sophia Simba kuibuka mshindi wa uenyekiti. Hata hivyo kuna maswali ambayo bado yanaendelea kubakia bila majibu. Tangu kwenye kampeni kulijitokeza malalamiko ya matumizi ya rushwa kwaajili ya kuwarubuni wajumbe wa mkutano kwaajili ya kujipatia kura. Na hata siku ya uchaguzi wenyewe, Mwenyekiti aliyemaliza muda waku Mh. Anna Abdala alieleza juu ya wagombea kutumia rushwa katika kampeni. aidha aliongeza suala la matumizi ya kampeni chafu na za kupakana matope na pia wagombea kuendekeza makundi. Lakini pia Mwenyekiti wa CCM Taifa aliongeza kitu kingine-Unafiki-. Achana na habari ya kampeni za kupakana matope na suala la makundi; tulikuwa na wagombea watatu wa nafasi ya Mwenyekiti wa UWT ambao wote ni wabunge na mmoja wao pia ni waziri, je;

1) Ni nani huyu mtoa rushwa kati ya hawa waheshimiwa watatu?
2) Ni nani huyu mnafiki?
3) Wajumbe wa Mkutano wa UWT waliwezeshwaje kumtambua asiyekuwa mtoa rushwa wala mnafiki ili kutomchagua?
4) Kuna uhakika gani kuwa aliyechaguliwa si miongoni mwa hao wawili hapo juu?

Wana JF ukumbi uko wazi kwenu
 
Back
Top Bottom